Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Rais wa Georgia Mikhail Saakashvili anatazamiwa kuiomba Marekani msaada wa silaha na wa kijeshi.
Urusi imeelezea kwamba hali ya nchi jirani ya Georgia kufanya jitihada katika kujihami ni jambo ambalo linatia wasiwasi, na kwamba itafanya juhudi zake katika kukatiza mipango hiyo.
Mwandishi wa BBC mjini Moscow anaelezea kwamba hali ambayo huenda ikazidisha uhasama kati ya mataifa hayo mawili.
Naibu wa waziri wa mashauri ya nje wa Urusi, Grigory Karasin, ameelezea kwamba Georgia inapanga kile alichosema ni uchokozi, hasa wakati nchi hiyo inajiandaa kukumbuka mwezi ujao, mwaka mmoja tangu vita kati ya nchi hizo mbili kufanyika.
Katika ziara yake katika mji mkuu wa Georgia, makamu wa rais wa Marekani, Joe Biden, amemuahidi Rais Mikhail Saakashvili kwamba nchi yake itaendelea kumsaidia.
Rais wa Georgia anatazamiwa kuomba msaada wa silaha na wanajeshi, katika kuilinda mipaka ya nchi hiyo.
Bw Biden amesema kwamba msaada wowote ule utatolewa kwa kuzingatia mifumo ya kidemokrasia.
Chanzo: BBC SWAHILI SERVICE.