Kunguru Mjanja
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 2,047
- 3,978
Wengi miongoni mwa watu watakaoomba viza za kuingia nchini Marekani wanaweza hivi karibuni kuanza kuombwa utambulisho wao katika mitandao ya kijamii, historia ya safari walizozifanya, namba zao za simu na anuani ya barua pepe.
Haya yanakwenda sambamba na mapendekezo ya Rais Donald Trump ya kuwachunguza kwa kina raia wa nchi za nje wanaoingia nchini humo. Kulingana na maelekezo ya wizara ya mambo ya nje, masharti hayo yatawahusu watu milioni 14.7 kila mwaka, ambao wataombwa taarifa zao za mawasiliano na safari katika muda wa miaka mitano kabla ya tarehe ya kuomba viza.
Waomba viza vile vile wataombwa kueleza ikiwa waliwahi kufukuzwa kutoka Marekani, au iwapo kuna mtu aliye na uhusiano nao ambaye aliwahi kuhusika katika vitendo vya kigaidi.
Nchi kama Ujerumani, Ufaransa na Uingereza, ambazo raia wake hawahitaji viza kuingia Marekani, hazitahusishwa katika utaratibu huo mpya, lakini China na India ni miongoni mwa nchi zinazolengwa.
Haya yanakwenda sambamba na mapendekezo ya Rais Donald Trump ya kuwachunguza kwa kina raia wa nchi za nje wanaoingia nchini humo. Kulingana na maelekezo ya wizara ya mambo ya nje, masharti hayo yatawahusu watu milioni 14.7 kila mwaka, ambao wataombwa taarifa zao za mawasiliano na safari katika muda wa miaka mitano kabla ya tarehe ya kuomba viza.
Waomba viza vile vile wataombwa kueleza ikiwa waliwahi kufukuzwa kutoka Marekani, au iwapo kuna mtu aliye na uhusiano nao ambaye aliwahi kuhusika katika vitendo vya kigaidi.
Nchi kama Ujerumani, Ufaransa na Uingereza, ambazo raia wake hawahitaji viza kuingia Marekani, hazitahusishwa katika utaratibu huo mpya, lakini China na India ni miongoni mwa nchi zinazolengwa.