Bikis
Member
- Feb 23, 2019
- 52
- 74
Juhudi za kimataifa zinaanza huku Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye binafsi aliagiza mauaji hayo ya Jenerali Soleimani, akiitishia Iran kwamba nchi yake itavishambulia vituo muhimu 52 kwa Iran endapo Jamhuri hiyo ya Kiislamu itaamuwa kulipiza kisasi.
Akitumia jukwaa lake maarufu la mtandao wa Twitter, Trump ameandika kwamba Marekani itajibu "kwa haraka na kwa nguvu sana", ikiwa Iran itachukuwa hatua za kulipiza kisasi.
Msururu huo wa twita za vitisho ulitanguliwa na Ikulu ya Marekani kuwasilisha rasmi mbele ya baraza la Congress ilani ya mashambulizi ya ndege isiyo rubani yaliyomuuwa Jenerali Soleimani.
Sheria za Marekani zinataka bunge lifahamishwe ndani ya kipindi cha saa 48 pale jeshi la Marekani linapotumwa kwenye mzozo unaohusisha silaha au hali inayoweza kupelekea vita.
Wachambuzi wengi wanasema kuwa kimsingi tayari Marekani imetangaza vita dhidi ya Iran, na iliyobakia ni juu ya Iran kama itaingia vitani au la.
Akitumia jukwaa lake maarufu la mtandao wa Twitter, Trump ameandika kwamba Marekani itajibu "kwa haraka na kwa nguvu sana", ikiwa Iran itachukuwa hatua za kulipiza kisasi.
Msururu huo wa twita za vitisho ulitanguliwa na Ikulu ya Marekani kuwasilisha rasmi mbele ya baraza la Congress ilani ya mashambulizi ya ndege isiyo rubani yaliyomuuwa Jenerali Soleimani.
Sheria za Marekani zinataka bunge lifahamishwe ndani ya kipindi cha saa 48 pale jeshi la Marekani linapotumwa kwenye mzozo unaohusisha silaha au hali inayoweza kupelekea vita.
Wachambuzi wengi wanasema kuwa kimsingi tayari Marekani imetangaza vita dhidi ya Iran, na iliyobakia ni juu ya Iran kama itaingia vitani au la.
