Ndugu zangu hapa Tanzania Diploma ni miaka 2. Kwa ninavyo fahamu mimi, mwanafunzi aliyemaliza form 4 huanza na certificate. Kinachotokea ni kwamba vyuo hivyo ambavyo viko chini ya NACTE, hudaili wanafunzi kwa kuwaambia kuwa utaanza diploma 1-3, maana yake ni kwamba mwanafunzi huyo akimaliza mwaka wa kwanza ambao ni certificate asiondoke na badala yake aendelee mpaka amalize diploma ambayo itakuwa ni mwaka wa 3.
Kwa mujibu wa CBET mode of teaching ambayo ndio msingi wa ufundishaji wa vyuo vya NACTE, kila stage kwao ni exist kwa mfano Basic Technician Certificate (NTA Level 4) ni exit point, Technician Certificate (NTA Level 5 - Diploma yr 1) ni exit, lakini ili uwe na uwezo wa kusoma degree lazima umalizie na Ordinary Diploma (NTA Level 6 na ufaulu wa GPA 3 na zaidi). Na mtu aliyemaliza form 6 na bahati mbaya akakosa alama za kusoma degree anaanza na Diploma (NTA Level 5).
Kwa uchache ni hayo tu.