Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa leo ataanza ziara ya kichama kwenye jimbo la Karatu.
Ziara ya Dr Slaa ni ya kawaida ya kuimarisha chama na kuwanadi wagombea wa Serikali za mitaa,vijiji na vitongoji.
Kama inavyokuwa siku zote kiongozi huyo anapozuru Karatu ni kwamba mapokezi makubwa sana yameandaliwa na inatarajiwa shughuli katika mji wa Karatu na viunga vyake kusimama walau kwa masaa 6 kupisha ujio wa kiongozi huyo maarufu zaidi Tanzania.
Katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Jumapili Chadema inatarajiwa kushinda mitaa,vijiji na vitongoji vyote jimboni Karatu kutokana na jimbo hilo kuwa ngome kuu ya Chadema kwa kipindi cha miaka 20 sasa.
Dr Slaa ni mzaliwa wa Karatu na ameongoza jimbo hilo kwa miaka 15 akiwa mbunge hivyo anaporejea nyumbani wanaKaratu wanasema ni mtoto amerudi nyumbani huku vijiji kadhaa vikitoa mbuzi na ngombe kuchinja na kufanya sherehe kwa heshima ya Kiongozi huyo wa kipekee.
Mapokezi katika picha:
Ziara ya Dr Slaa ni ya kawaida ya kuimarisha chama na kuwanadi wagombea wa Serikali za mitaa,vijiji na vitongoji.
Kama inavyokuwa siku zote kiongozi huyo anapozuru Karatu ni kwamba mapokezi makubwa sana yameandaliwa na inatarajiwa shughuli katika mji wa Karatu na viunga vyake kusimama walau kwa masaa 6 kupisha ujio wa kiongozi huyo maarufu zaidi Tanzania.
Katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Jumapili Chadema inatarajiwa kushinda mitaa,vijiji na vitongoji vyote jimboni Karatu kutokana na jimbo hilo kuwa ngome kuu ya Chadema kwa kipindi cha miaka 20 sasa.
Dr Slaa ni mzaliwa wa Karatu na ameongoza jimbo hilo kwa miaka 15 akiwa mbunge hivyo anaporejea nyumbani wanaKaratu wanasema ni mtoto amerudi nyumbani huku vijiji kadhaa vikitoa mbuzi na ngombe kuchinja na kufanya sherehe kwa heshima ya Kiongozi huyo wa kipekee.
Mapokezi katika picha: