Mapishi Mbalimbali

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
Mapishi ya korosho na mahindi





Mahitaji:
2008413173252_1.jpg

Korosho gramu 100, mahindi gramu 50, figiri gramu 80, chumvi kijiko kimoja, chembechembe za kukoleza ladha nusu ya kijiko
Njia:
1. kata figiri iwe vipande. Chemsha maji, halafu tia mahindi na figiri kwenye maji, baada ya dakika moja, vipakue. Na weka vipande vya figiri
2.tia mafuta kwenye sufuria, tia korosho, korogakoroga, tia mahindi na vipande vya figiri, tia chumvi na chembechembe za kukoleza ladha korogakoroga kwa haraka. Chemsha pamoja kasha ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.




Mapishi ya supu ya paja la bata na mwani




Mahitaji:
200841216467_1.jpg

Mapaja mawili ya bata, mwani grami 20, mahindi gramu 50, maharagwe mabichi gramu 50, chumvi vijiko viwili
Njia:
1. osha mapaja ya bata, halafu chemsha maji ukisha tia mapaja ya bata kwenye maji, ili kuondoa damu, halafu yapakue.
2. osha mwani halafu ukate uwe vipande, kata maharagwe mabichi yawe vipande, kata mahindi yawe vipande.
3. chemsha maji, halafu tia mapaja ya bata, vipande vya mahindi, maharagwe mabichi, baada ya dakika 20, punguza moto, tia mwani, endelea kuchemsha kwa saa mbili, baadaye tia chumvi, korogakoroga. Ikiiva, ipua na hapo supu inakuwa tayari kwa kunywa.





Mapishi ya uji wa mchele na boga na choroko



2008118521121877807.jpg
Mahitaji: Mchele gramu 100, boga moja, choroko gramu 30, tende gramu 10
Njia:
1. osha tende. Kata boga uwe vipande, osha mchele na choroko.
2. chemsha maji kwenye sufuria, halafu weka vipande vya boga kwenye sahani halafu weka sufuria, funika kifuniko na kuichemsha kwa mvuke kwa dakika 30 mpaka viwe laani.
3. chemsha maji halafu tia mchele na choroko kwenye sufuria. Baada ya kuchemka, punguza moto, endelea kuchemsha kwa dakika 15, tia vipande vya maboga, tia tende. Mpaka hapo uji huo uko tayari kuliwa.


Mapishi ya maharagwe na kamba-mwakaje



Mahitaji
0053b301146c7f1a7aec2c46.jpg

Kamba-mwakaje gramu 200, maharagwe gramu 50, yai moja, chumvi kijiko kimoja, mvinyo wa kupikia vijiko viwili, mchuzi wa sosi kijiko kimoja, vipande vya vitunguu maji gramu 5 na tangawizi gramu 5
Njia
1. washa moto chemsha maji, baada ya kuchemka, tia maharagwe na chumvi, baada ya dadika 5 yaipue na uyapakue.
2. koroga kamba-mwakaje pamoja na ute wa yai.
3. weka sufuria jikoni, mimina mafuta mpaka yawe nyuzi joto 60, tia vipande vya vitunguu maji na tangawizi, korogakoroga, tia kamba mwakaje, korogakoroga, tia mchuzi wa sosi, mvinyo wa kupikia, chumvi, korogakoroga, mwisho tia maharagwe korogakoroga, ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

Mapishi ya supu ya uyoga, mboga na nyama ya paja la nguruwe



2008512154427_1.jpg
Mahitaji: Mboga ya majani gramu 50, uyoga gramu 100, nyama ya paja la nguruwe gramu 50, nyanya ndogo gramu 20, vitunguu maji gramu 5, tangawizi gramu 2, mvinyo wa kupikia kijiko kimoja, mafuta ya ufuta kijiko kimoja, chumvi kijiko kimoja
Njia:
1. chemsha maji, tia vipande vya tangawizi.
2. tia vipande vya uyoga, mimina mvinyo wa kupikia.
3. tia nyanya ndogo na nyama ya paja la nguruwe halafu koroga.
4. tia mboga, chumvi, mimina mafuta ya ufuta, tia vipande vya vitunguu maji. Acha ichemka kwa muda, mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.


 

Similar Discussions

Back
Top Bottom