Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,014
- 9,883
Magari ya kivita yakiwa katika mitaa kadhaa
Magari ya kivita yametanda katika mitaa ya miji kadhaa nchini Myanmar huku kukiwa na ishara kwamba wanajeshi wanaandaa msako dhidi ya wale wanaopinga mapinduzi yaliyofanywa Februari 1.
Mtandao wa interneti umezimwa nchi nzima licha ya juhudi za kimataifa kupinga hatua hiyo.
Katika jimbo la kaskazini la Kachin, vikosi vya usalama vimefyatua risasi katika siku ya tisa ya maandamano ya kupinga mapinduzi nchini kote.
Afisa wa maalum wa umoja wa mataifa nchini humo amewashutumu wanajeshi kwa kile walichokiita kutangaza vita dhidi ya raia wasio na hatia.
Tom Andrews, mwandishi maalum wa umoja wa mataifa kuhusu Myanmar inayojulikana pia kama Burma, amesema majenerali walikuwa wakionesha dalili za kukata tamaa na kuwajibika.
Balozi mbalimbali za nchi za Magharibi zimehimiza jeshi kuonesha weledi wake wakati huu ambapo nchi hiyo ipo katika wakati mgumu.
Kote nchini humo, mamia ya maelfu ya waandamanaji wameendelea kujikusanya katika miji kadhaa ikiwa ni siku ya tisa mfululizo kupinga mapinduzi hayo.
Katika mji wa Myitkyina, katika jimbo la Kachin, risasi zilisikika wakati vikosi vya usalama vikipambana na waandamanaji.
Haikufahamika ikiwa ni risasi za mpira au ama moto zilizotumika kuwatawanyisha waandamanaji hao.
Waandishi wa tano ni miongoni mwa waliokamatwa.
Mapinduzi nchini Myanmar yaliondoa serikali ya raia iliyoongozwa na Aung San Suu Kyi.
Chama chake kilishinda kwa kishindo katika uchaguzi huo mnamo Novemba, lakini wanajeshi walisema ulikua uchaguzi uliojaa ulaghai
Huko Yangon, magari ya jeshi yalionekana kwa mara ya kwanza tangu mapinduzi yaanze.
Jumuiya za kidini na waandisi waliongoza maandamano maeneo hayo , wakati waendesha pikipiki wakiwa wakiendesha katika mitaa ya mji mkuu wa Nay Pyi Taw.
Kampuni za simu nchini humo zimesema mawasiliano ya intaneti yamezimwa kuanzia saa saba mpaka saa tatu majira ya saa za huko.
Daktari mmoja katika hospitali ya Nay Pyi Taw ameiambia BBC kuwa vyombo vya usalama vilikuwa vinawavamia watu nyumbani kwao majira ya usiku.
"Bado nina wasiwasi kwasababu marufuku ya kutotoka nje yapo kuanzia saa mbili mpaka saa kumi alfajiri na ndio muda ambao polisi wanatumia mwanya wa kukamata watu kama sisi," alisema daktari, ambaye jina lake limehifadhiwa kwasababu za usalama.
"Jana waliiba nyumbani kwangu, waliwavamia watu kinyume na sheria, Ndio maana nina wasiwasi."
Afisa wa ubalozi wa Marekani mjini Yangon amewataka raia wa Marekani kutotoka nje wakati huo wa marufuku ya kutoka nje.