Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,175
- 829,132
Kuna kitu kinaitwa Closed Circuit Coup. Ama CCC. Mambo ni mengi muda mchache.
Teknolojia ya upashanaji Habari, mawasiliano, majadiliano na hata malumbano ya hoja sasa vinaweza kufanyika kwa ufanisi mkubwa bila watu kuonana wala kufahamiana kabisa....!!!
Hapo kabla taarifa za kaya nzima zilikuwa zinamfikia mtemi mkuu kupitia taratibu maalum za ngazi za kiuongozi toka chini mpaka juu kabisa.
Na taarifa za usalama wa kaya zinapaswa kufika juu kabisa kabla ya saa 5 asubuhi kila siku iendayo kwa Mungu
Mambo kwasasa yamebadilika mno.
Ndani ya kaya kubwa habari zake zinaweza kuenea kote ndani ya muda mchache na bila hata kuzingatia ule utaratibu rasmi. Kuna athari zake kwenye hili.
Kuna baadhi ya habari ama taarifa kaya inazipata mapema kabisa kabla bila hata kuhakikiwa, kuhaririwa ama kuchujwa. Kiusalama hili ni jambo hatari sana.
Zingatio la kwamba jamii ipate nini ama ilishwe nini kwa wakati gani lina umuhimu wake mkubwa sana.
Lakini kwa maendeleo haya ya upashanaji habari enzi hizi yamevunja taratibu na miiko mingi.
Ndio maana kwa wenzetu waliojiandaa wamedhibiti kwa kiasi kikubwa hili lakini bado wakizingatia haki ya msingi ya kupeana taarifa kwa wanakaya wote na kati ya mtu na mtu, mtu na kikundi na kinyume chake.
Ni kwa muktadha huo basi, mwaliko wa mtemi kwenye boma la kabumbu ama shughuli fulani ya kaya.
Unaweza kuwa kiama kikubwa kwa kujikuta nyie wote na mtemi wenu mnawekwa chini ya karantini na kushikiliwa mateka. Na wanakijiji waliochoka na wenye wenye kuchukua magumu....!!!!
Kwa jinsi dunia inavyokwenda kwa kasi na akili za kizazi kipya zinavyochanganya haraka na zenye maamuzi ya papo kwa papo.
Siku hizi hawasubiri kuvamia kizimba cha korokoroni wa kaya ili wajitwalie marungu pinde na mishale....!
Ama hawaendi kuzingira pale kwenye bango la habari na kuandika kwa maandiko makubwa.
KUANZIA SASA TUMESHIKA HATAMU, la hasha wala hawamvizia mtemi Chifu akiwa kwenye boma lake, wamtie kabari na kumlazimisha kutamka kuwa hataki tena kuwa chifu wa kaya.
Maboma na vizimba visivyo wazi pande zote vinaweza kutumika vibaya kwa nyakati hizi kuwalazimisha watemi na machifu wakimbie kaya zao huku wakikimbizwa na kutaabika hasa.
Hawa korokoroni na wasungusungu wetu wakichoka kutaabika na kukutana wale magangwe waganga njaa huko na huko.
Moyo wa mtu ni kiza kinene.
Teknolojia ya upashanaji Habari, mawasiliano, majadiliano na hata malumbano ya hoja sasa vinaweza kufanyika kwa ufanisi mkubwa bila watu kuonana wala kufahamiana kabisa....!!!
Hapo kabla taarifa za kaya nzima zilikuwa zinamfikia mtemi mkuu kupitia taratibu maalum za ngazi za kiuongozi toka chini mpaka juu kabisa.
Na taarifa za usalama wa kaya zinapaswa kufika juu kabisa kabla ya saa 5 asubuhi kila siku iendayo kwa Mungu
Mambo kwasasa yamebadilika mno.
Ndani ya kaya kubwa habari zake zinaweza kuenea kote ndani ya muda mchache na bila hata kuzingatia ule utaratibu rasmi. Kuna athari zake kwenye hili.
Kuna baadhi ya habari ama taarifa kaya inazipata mapema kabisa kabla bila hata kuhakikiwa, kuhaririwa ama kuchujwa. Kiusalama hili ni jambo hatari sana.
Zingatio la kwamba jamii ipate nini ama ilishwe nini kwa wakati gani lina umuhimu wake mkubwa sana.
Lakini kwa maendeleo haya ya upashanaji habari enzi hizi yamevunja taratibu na miiko mingi.
Ndio maana kwa wenzetu waliojiandaa wamedhibiti kwa kiasi kikubwa hili lakini bado wakizingatia haki ya msingi ya kupeana taarifa kwa wanakaya wote na kati ya mtu na mtu, mtu na kikundi na kinyume chake.
Ni kwa muktadha huo basi, mwaliko wa mtemi kwenye boma la kabumbu ama shughuli fulani ya kaya.
Unaweza kuwa kiama kikubwa kwa kujikuta nyie wote na mtemi wenu mnawekwa chini ya karantini na kushikiliwa mateka. Na wanakijiji waliochoka na wenye wenye kuchukua magumu....!!!!
Kwa jinsi dunia inavyokwenda kwa kasi na akili za kizazi kipya zinavyochanganya haraka na zenye maamuzi ya papo kwa papo.
Siku hizi hawasubiri kuvamia kizimba cha korokoroni wa kaya ili wajitwalie marungu pinde na mishale....!
Ama hawaendi kuzingira pale kwenye bango la habari na kuandika kwa maandiko makubwa.
KUANZIA SASA TUMESHIKA HATAMU, la hasha wala hawamvizia mtemi Chifu akiwa kwenye boma lake, wamtie kabari na kumlazimisha kutamka kuwa hataki tena kuwa chifu wa kaya.
Maboma na vizimba visivyo wazi pande zote vinaweza kutumika vibaya kwa nyakati hizi kuwalazimisha watemi na machifu wakimbie kaya zao huku wakikimbizwa na kutaabika hasa.
Hawa korokoroni na wasungusungu wetu wakichoka kutaabika na kukutana wale magangwe waganga njaa huko na huko.
Moyo wa mtu ni kiza kinene.