Mapendekezo ya 'Ruti' mpya Dar

kwa sasa hamna maeneo ya dar yenye changamoto za usafiri kama ubungo watu wengi lakini barabara zote ni za vumbi
Yeah, wilaya ya ubungo ni majanga kwa kweli. Serikali ingeona umuhimu wa kujenga miundombinu ya ubungo.
 
tena kwa hali ya dharura
Manake ukiacha huko Sinza ambapo lami ilikuwepo mda, sehemu zingine zote hakuna lami. Goba Road, Wazo Road, morogoro Road na kinyerezi Road tu. Kuna maeneo mengi yanahitaji miundombinu. Nilienda Kijichi nikaona walivyopendezesha mji, kila mtaa ni lami.
 
sijui pande hizi tulikosea wapi, na mbunge tunaye
 
madale-nyuki, nyuki-morocco, morocco msasani. La nne lipi ndugu muongo!
 
1 na 2 Muhimu sana maana watu wanaenda kuunganisha safari Azania au Tegeta kwa ndevu, hvyo kupata gari ya moja kwa moja itakua poa

Madale makumbusho zilikuwepo

Hiyo njia ya kupitia kinyerezi/ segerea bonyokwa kimara, itaua watu, kwanza jinsi ya barabara yenyewe ilivyo ina milima mikali sana haswa hiki kipande cha kujia kimara kutoka bonyokwa, magari mengi si mazima pia hata madereva ni hovyo sana wataua wao

Njia nne to kimara via matosa nayo ina milima iliyo simamia kucha sana pia barabara hii na hiyo ya kimara to bonyokwa nadhani mpaka njia panda segerea/kinyerezi ni rough road

Madale makumbusho zilikuwepo ila kazi ni asubuhi kupeleka watu na jioni kuwarudisha mchana kazi hamna
pia route ya tegeta-nyuki_ mbezi ndio imeua kabisa
 
Wazo zuri sana na litakuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa maeneo hayo, Ila kuna changamoto za aina mbili hapo, ya kwanza ni ubovu wa hizo barabara mfano wa njia nne kimara na kupitia bonyokwa,
 
Mawazo mazuri kabisa ila tatizo ni hao wenye kupanga hizo route ndiyo wanufaika wa adha mnazopata sasa, wangekuwa wanasafiri kwa usafiri wa public wangeyaona hayo matatizo siku nyingi na kuyatafutia ufumbuzi wa haraka
 
Weka Bunju --- Kigamboni kupitia Daraja la Mwalimu Nyerere!!
 
Hakuna Boss atapeleka gari sehemu ya mbali afu abiria hakuna.

Bunju KKOO hiyo ruti hautatokea sababu ni mbali sana
 
Uko sahihi kabisa Chanika -Posta hii ianze hata kesho ziwepo tata kama 20 zitasaidia tena ziende hadi kivukoni na Chanika -Mawasiliano yani hii ianze Leo jioni ya Chanika Mbezi nayo ianze kesho asubuhi
Chanika mawasiliano mbona zipo.

Zimeandikwa BY/SOKONI - SIMU2000
 
Tegeta-Kimara via njia nne kupitia temboni njia ni nzuri kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…