Shedafa
JF-Expert Member
- May 21, 2008
- 802
- 173
Kwa wiki ya pili sasa eneo la Yombo Vituka limekuwa katika hali ngumu ya usalama, ni eneo kuanzia Buza hadi kufika Vituka Sigara. Kuna kikundi cha vijana ambacho kimeamua kupiga watu mapanga hovyo nyakati za jioni, cha kushangaza wakati mwingine hawachukui chochote. Inaonekana nia yao ni kuua tu kwani hadi kufikia leo asubuhi wamekwisha piga mapanga watu 18, na inasemekana kati ya hawa kuna waliopoteza maisha. Sina uhakika nalo kwa kuwa majeruhi wamekuwa wakichukuliwa na polisi kupelekwa hospitali, baada ya hapo tumekosa taarifa ya maendeleo yao. Tunajaribu kuweka sungu sungu maeneo yote haya lakini hatujafanikiwa kulizima hili wimbi ingawa mara 2 moja ya vikundi vya sungu sungu wamefanikiwa kupambana na hili kundi na kuwaua 3 wao, hali bado ni ngumu. Jana tu kijana mmoja jirani katokea tundu la sindano baada ya kufanikiwa kuwazidi mbio na hii ilikuwa majira ya saa 1 tu usiku.