Mapandikizi ya CCM yarudi Bungeni

Mapandikizi ya CCM yarudi Bungeni

Mwiba

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
7,607
Reaction score
1,760
Kuna hatari ya mapandikizi yaliyochomekwa kwenye vyama vya siasa haswa vile vinavyounda UKAWA yakarejea kwenye Bunge Maalum la Katiba.

CCM huenda ikayapoteza mapandikizi hayo ambayo itachelewa kuwasiliana nayo kwa jinsi gani watawalipa lakitatu za bungeni. Mapandikizi hayo ambayo ni CCM itawawia vigumu kukaa nje wakiwa kama UKAWA wakati wanazitamani lakitatu.

Sasa kila atakaerudi fahamu kuwa ni pandikizi la CCM na halijatiliwa hela kwenye acc.yake na siku zinapita hesabu ya lakitatu aliyopiga inapungua kwa hiyo ni bora arudi bungeni.

Vyama vinavyounda UKAWA vitafaidika sana kwa kuwatambua na kutambua walikuwa wanaishi na chui alievaa ngozi ya kondoo. Tuzidi kuvuta subira.
 
Siyo mapandikizi ya ccm!, viongozi wa ukawa hawana haki ya kuwazuia wajumbe, wamechoka, hata wiki bado wamerudi 6 next week tutegemee zaidi.
 
Wenye uchungu na taifa hili wanarud bungen...walionunuliwa na wafitin kaen kando WaTZ wachape kaz


Sent from my iPhone using JamiiForums.🔩🔨uuuu
 
Wenye uchungu na taifa hili wanarud bungen...walionunuliwa na wafitin kaen kando WaTZ wachape kazi

Wenye uchungu na nchi hii ni wale walioionya CCM isitumie ubabe wataipeleka Nchi hii kwenye njia iliyo na gharama kurudi ,sasa hao wanao rudi hawana uchungu na nchi au Taifa hili hata tone ,tena ni bora wale wajumbe au CCM waliobakia ambao hawakutoka wakati UKAWA walipoamua kuingia mitini msimamo wao unajulikana wazi ,hawa wanaorudi ni wanafiki na dira wanayoionyesha si ya kuthaminiwa hata huko wanakorudi ,utawaamini vipi kama kura yao itakwenda kwenye hoja za CCM.
 
Siyo mapandikizi ya ccm!, viongozi wa ukawa hawana haki ya kuwazuia wajumbe, wamechoka, hata wiki bado wamerudi 6 next week tutegemee zaidi.

Kiongozi hana haki lakini Chama kina haki kwani kinaongozwa na misingi na kanuni walizojiwekea ,kiongozi just anafuata sheria na kanuni zake ,mbona kule Zanzibar CCM wanafukuzana wakati wakitumia demokrasia ya mawazo binafsi ?
 
naamini wote wamerudi ila wapo geshti wamejificha

Hao wapo standby ,na kitu kingine jamaa wanaweza kwenda wakaweka saini na kuchukua laki zao za wiki kisha wakahudhuria kama masanamu au furnitures za bungeni sasa sijui nani atakuwa amepotezwa maboya ,ila mapandikizi hayawezi kuvumilia kukaa pembeni ni lazima yachipue !
 
ndo kawaida yenu chama kinakufa nyie maneno maneno tu utafikiri waimba taarabu
 
Kweli mkuu mapandikizi ya ccm yapo kama kina Dovutwa, mrema, arfi, leticia nyerere, shibuda, cheyo na wenzake, hao sio wapinzani wa ukweli, bali ni wachumia tumbo na wanaccm walioko upinzani.
 
Wabunge wa ukawa wanatamani kurudi bungeni lakini viongozi wao wanawazuia hapo demokrasia iko wapi?
Ukawa ni genge la wahuni.
 
Kweli mkuu mapandikizi ya ccm yapo kama kina Dovutwa, mrema, arfi, leticia nyerere, shibuda, cheyo na wenzake, hao sio wapinzani wa ukweli, bali ni wachumia tumbo na wanaccm walioko upinzani.

Tatizo la Ukawa mnadhani kuwa mna akili kuliko wengine.
 
Khaa hivi hawa UKAWA wanawawakilisha wananchi gani?? Mbona mimi siwatambui??
 
Khaa hivi hawa UKAWA wanawawakilisha wananchi gani?? Mbona mimi siwatambui??
UKAWA wanawawakilisha wananchi waliotoa maoni yao mbele ya Tume ya Marekebisho ya Katiba. Kwa sasa Fisadi Sitta haongozi kikao cha BMLK, anaongoza kikao cha walafi wa posho, wanafiki na mafisadi ambao wako tayari kusaliti maoni ya Watanzania kwa kipande cha fedha cha laki tatu.
 
UKAWA wanawawakilisha wananchi waliotoa maoni yao mbele ya Tume ya Marekebisho ya Katiba. Kwa sasa Fisadi Sitta haongozi kikao cha BMLK, anaongoza kikao cha walafi wa posho, wanafiki na mafisadi ambao wako tayari kusaliti maoni ya Watanzania kwa kipande cha fedha cha laki tatu.

mbona nyie mlioona mfumo wa serikali tatu munajiimanisha kuwa ndiyo wananchi wa taifa hili kuliko wale ambao ndiyo wengi wanaoamini kwamba serikali mbili ndiyo bola?
 
Back
Top Bottom