Mapambano dhidi ya corona na matumizi ya simu

nusuhela

JF-Expert Member
Jan 26, 2014
5,736
6,972
Nikiwa nimekaa kwenye daladala huku nawaza kuhusu hatma ya taifa letu kutokana na janga la corona, nikajikuta nafikiria kuhusu usalama wa wasafiri kwa kutumia usafiri huo wa uma.

Watu bado wanashika vyuma kule juu, watu bado wanashika viti, watu bado wanashika madirisha.

Najiuliza, kwa siku huwa ni watu wangapi hushika sehemu hizo.

Mbali na kushika vyuma, viti na vioo vya daladala, watu wanatumia simu wawapo ndani ya daladala na wawapo nje ya daladala.

Issue yangu ipo kwenye matumizi ya simu. Baada ya kushika chuma, viti na vioo tunashika simu zetu. Ikumbukwe, kinachonawa ni mikono peke yake huku tukiacha virus kwenye simu zetu ambazo baada ya kunawa tunazitumia.

Je, tutaweza kushinda hii vita maana naona matumizi ya simu ni moja kati ya vinavyoweza kuwa sababu kubwa ya kusambaa kwa virus hawa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunaomwamini Mungu tumuombe tu. Juzi nimesoma post moja wanasema ukifika nyumbani kabla hujafanya chochote pitiliza bafuni uoge na ufue nguo ulizovaa, kwa hiyo hapa wanaotoka kila siku watakuwa na kazi ya kufua nguo.

Sawa hilo sio gumu ukizingatia ni hali ya dharura ila nikajiuliza vipi kuhusu simu, pochi, bahasha, begi n.k utafuaje? Kitu kama begi bila shaka huwezi kuosha kila siku
 
Ndio maana maombi yanahitajika. Kunawa tu na barakoa havitoshi kabisa.
Hapo kwenye kusali nina swali kidogo.unasali usiupate ugonjwa au unasali chanjo ipatikane au unasali ugonjwa upotee wenyewe au unasali vipi.
 
Sioni huu ugonjwa ukiisha hivi karibuni hasa kwa kutegemea hizi tahadhari TU, tufanye hivyo ili angalau kupunguza hatari zaidi, yaani unakwepa huku unapigwa kule, na kuna uwezekano kuna njia nyingne za usaambaji hazijulikani,life span yao pengne sio km tulovyoaminishwa...

Tukumbuke Mwazo hao hao wanasayansi walisema hausambazwi kutoka kwa binadamu mmoja kwenda mwingne,
Wakaja tena kutuambia hawaishi kwenye joto kali,
Mara ooh pombe inasaidia..

Ukiniuliza leo kipi unatamani kiwe cha kwanza kupatikana kati ya Kinga au Tiba.
Nitaomba Kinga.

Huu ugonjwa kuisha Ni Mungu tuu aamue aupitishe.
Kinyume na hapo inakuja picha ya miili iliyooza mitaani.
 
Yasalie yote hayo. Ujumbe ni kwamba mwombe Mungu kwa kila kitu na zingatia usafi, kaa nyumbani, epuka misongamano... It is a package.
Hapo kwenye kusali nina swali kidogo.unasali usiupate ugonjwa au unasali chanjo ipatikane au unasali ugonjwa upotee wenyewe au unasali vipi.
 
Back
Top Bottom