LEVEL
Senior Member
- Jul 4, 2013
- 195
- 51
Nimekua nikitafakari sana kuhusiana na hii mikopo inayotolewa kama msaada kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kwa kweli imesaidia watu wengi kutokana na wengi wetu kutoka katika familia za kipato cha chini na hivyo kushindwa kumudu gharama hizi kwa hili naipongeza serikali kwa mipango mizuri ya kuinua kiwango cha elimu.
Ila pindi mtu anapomaliza chuo huwa na deni kubwa ambalo bodi ya mkopo hukata kidogo dogo ili kuweza kurudisha pesa hizi na hapa madeni hutofautiana kulingana na kiwango cha mkopo alichopewa mhusika unakuta mtu unamaliza chuo una deni la hadi 12 mil, hata kabla ya ajira.
Maoni yangu ni kwamba, kama serikali wanao uwezo wa kutoa mikopo hii kwa wanachuo wengi kiasi hiki ni kwanini wasifute au kupunguza ada za vyuo ili watu wajisomeshe wenyewe na hizo pesa wanazotoa mikopo zikapelekwa vyuoni kujenga miundo mbinu pamoja na kuwalipa walimu na wafanyakazi wengine wa vyuo kwa sababu inauma sana mtu unapewa mkopo sawa ila mwisho wa siku unaanza tu kazi salary slip ya kwanza tu inakuja na deni la milioni kadhaa.
Pili, hizo hela wanazotoa mikopo nyingi zinapotea kwa mfano kuna watu wana disco, kufa, kuacha chuo nk. Sasa kuliko serikali kuendelea kupata hasara ya hizo ela zinazo potea kwa sababu mbalimbali ni bora watupunguzie tu ada tujisomeshe lakini vyuo watoe hela hizo kuviendesha wao.
Ila pindi mtu anapomaliza chuo huwa na deni kubwa ambalo bodi ya mkopo hukata kidogo dogo ili kuweza kurudisha pesa hizi na hapa madeni hutofautiana kulingana na kiwango cha mkopo alichopewa mhusika unakuta mtu unamaliza chuo una deni la hadi 12 mil, hata kabla ya ajira.
Maoni yangu ni kwamba, kama serikali wanao uwezo wa kutoa mikopo hii kwa wanachuo wengi kiasi hiki ni kwanini wasifute au kupunguza ada za vyuo ili watu wajisomeshe wenyewe na hizo pesa wanazotoa mikopo zikapelekwa vyuoni kujenga miundo mbinu pamoja na kuwalipa walimu na wafanyakazi wengine wa vyuo kwa sababu inauma sana mtu unapewa mkopo sawa ila mwisho wa siku unaanza tu kazi salary slip ya kwanza tu inakuja na deni la milioni kadhaa.
Pili, hizo hela wanazotoa mikopo nyingi zinapotea kwa mfano kuna watu wana disco, kufa, kuacha chuo nk. Sasa kuliko serikali kuendelea kupata hasara ya hizo ela zinazo potea kwa sababu mbalimbali ni bora watupunguzie tu ada tujisomeshe lakini vyuo watoe hela hizo kuviendesha wao.