Maoni ya katiba mpya – Na wewe sema lako ni haki yako

Sungurampole

JF-Expert Member
Nov 17, 2007
984
205
Katika uzi juu ya mada ya maoni juu ya katiba mpya(12.2.2012) for curiosity nilipoyapitia nilipata haya wewe unasemaje lako liko hapa?

Najua ni ngumu lakini fikiri, chekecha, weka lako moja.

  1. Katiba yenye zero tolerance kwa ufisadi!!!

  1. Ukikamatwa unatoa au kupokea rushwa, kuuza na kusafirisha madawa ya kulevya basi adhabu yake ni kunyongwa

  1. Azimio la arusha liingie kwa katiba

  1. Rais asiwe mwanasiasa

  1. Vyama vya siasa visidi vitatu -Wengine wawe wagombea binafsi.

  1. Vyama vipgiwe kura vitavyopata chini ya idadi fulani ya kura vifutiwa usajili hadi vibaki vitatu kama sio viwili

  1. Tutulieni kwanza tupigwe elimu ya uraia...

  1. Iwe marufuku kuuza mali ya umma

  1. Kupunguza madaraka ya RAIS

  1. Kurudisha kwa Tanganyika

  1. Teuzi za rais zote zithibitishwe na bunge kundoa nepotism

  1. Kusiwe na wakuu wa wilaya, wanaongeza mzigo wa gharama kwa serikali kuwalipa mishahara na marupurupu, wakurugenzi watosha.

  1. Mawaziri wasitokane na wabunge bali professionals

  1. Mgombea binafsi ni muhumu sana, kwa ngazi zote za uongozi wa kisiasa

  1. Muungano wa serikali moja

  1. Wakuu wa Mikoa na wakuu wa Wilaya wachaguliwe na wananchi kwa njia ya Kura

  1. Urais wa kifalme uondolewe

  1. Safari za rais za nje ya nchi ziwekwe kikomo- sizidi safari 20 kwa mwaka.

  1. Shule za secondary zote za kata zisizokuwa na waalimu wasiozidi 5 zifungwa kuepuka failures za aibu kila mwaka.

  1. Usalama wa taifa, majukumu yake yaelekezwe kwa taifa kweli na isiwe katika misingi ya kulinda viongozi wabovu na kufumbia maovu

  1. Ubunge uwe miaka 10 tu (vipindi viwili tu kama ilivyo uraisi)
 
Katika uzi juu ya mada ya maoni juu ya katiba mpya(12.2.2012) for curiosity nilipoyapitia nilipata haya wewe unasemaje lako liko hapa?

Najua ni ngumu lakini fikiri, chekecha, weka lako moja.
  1. Katiba yenye zero tolerance kwa ufisadi!!!
  1. Ukikamatwa unatoa au kupokea rushwa, kuuza na kusafirisha madawa ya kulevya basi adhabu yake ni kunyongwa
  1. Azimio la arusha liingie kwa katiba
  1. Rais asiwe mwanasiasa
  1. Vyama vya siasa visidi vitatu -Wengine wawe wagombea binafsi.
  1. Vyama vipgiwe kura vitavyopata chini ya idadi fulani ya kura vifutiwa usajili hadi vibaki vitatu kama sio viwili
  1. Tutulieni kwanza tupigwe elimu ya uraia...
  1. Iwe marufuku kuuza mali ya umma
  1. Kupunguza madaraka ya RAIS
  1. Kurudisha kwa Tanganyika
  1. Teuzi za rais zote zithibitishwe na bunge kundoa nepotism
  1. Kusiwe na wakuu wa wilaya, wanaongeza mzigo wa gharama kwa serikali kuwalipa mishahara na marupurupu, wakurugenzi watosha.
  1. Mawaziri wasitokane na wabunge bali professionals
  1. Mgombea binafsi ni muhumu sana, kwa ngazi zote za uongozi wa kisiasa
  1. Muungano wa serikali moja
  1. Wakuu wa Mikoa na wakuu wa Wilaya wachaguliwe na wananchi kwa njia ya Kura
  1. Urais wa kifalme uondolewe
  1. Safari za rais za nje ya nchi ziwekwe kikomo- sizidi safari 20 kwa mwaka.
  1. Shule za secondary zote za kata zisizokuwa na waalimu wasiozidi 5 zifungwa kuepuka failures za aibu kila mwaka.
  1. Usalama wa taifa, majukumu yake yaelekezwe kwa taifa kweli na isiwe katika misingi ya kulinda viongozi wabovu na kufumbia maovu
  1. Ubunge uwe miaka 10 tu (vipindi viwili tu kama ilivyo uraisi)
 
Hiyo ya kwanza juu ya adhabu...katiba si Penal Code.

Umri wa mbunge uwe si zaidi ya miaka 60
Mahakama ijitegemee
Raisi asiteue majaji wala mwanasheria mkuu
Madoctor wazembe wapewe adhabu kali na fidia kwa mwatjhirika
 
Na, Vijana wa Umoja wa Kitaifa – Zanzibar.
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, sheria namba 8, haiwezi kuwa juu ya Katiba ya Zanzibar.
Vipi sheria ya Mabadiliko ya Katiba iweze kufanya kazi Zanzibar wakati Zanzibar ni Nchi iliyo na mipaka yake Kikatiba? Katiba ya Zanzibar ya 1984, Toleo la 2010, inaeleza wazi wazi katika Sura ya Kwanza, Sehemu ya Kwanza kwamba: "Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar". Kama hivyo ndivyo, sheria ya mabadiliko ya Katiba kupitia kifungu chake cha 19-(1) kinachohusiana na makosa na adhabu kwa watakaotoa maoni nje ya hadidu rejea za rasimu ya Katiba: kifungu hicho pamoja na sheria yenyewe ya marekebisho ya Katiba, mwisho wake CHUMBE !!
Pili, kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya 1984, Toleo la 2010, inaeleza wazi kuwa, Katiba ya Zanzibar ndiyo yenye nguvu za kisheria nchini kote, ambapo ikitokezea sheria yo yote kutofautiana na Katiba ya Zanzibar, sheria hiyo itakuwa batili kwa kiwango kile ambacho kinahitilafiana. Hii ni kuonesha nguvu na uwezo iliyonayo Katiba ya Zanzibar mbele ya sheria namba 8 ya mabadiliko ya Katiba, na kwamba, Katiba ya Zanzibar ndio "(The Grundnorm, which is the highest form of validity, being of the highest authority, providing efficient and affordable legal representation).
Tatu, hata hiyo Mahakama ya Rufaa, nayo haina uwezo, wala mamlaka, wala haki Kikatiba ya kuitafsiri Katiba ya Zanzibar maana Katiba ya Zanzibar ya 1984, Toleo la 2010, inaeleza katika kifungu cha 99 kinachohusiana na kazi na uwezo wa Mahakama ya Rufaa kwamba Mahakama ya Rufaa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haiwezi kutafsiri Katiba ya Zanzibar. Kwa maneno mengine, Katiba ya Zanzibar inajitegemea, na kwa mantiki hiyo, Wazanzibari watahukumiwa kwayo tu, na si kwa sheria ya mabadiliko ya Katiba wala nyengine yo yote ile.
Nne, pamoja na vitisho vilivyomo kwenye kifungu cha makosa na adhabu ndani ya muswaada na sheria ya mabadiliko ya Katiba, bado sheria hiyo haiwezi kuwa JUU ya Katiba. Na sheria yo yote, itakayokwenda kinyume na Katiba, sheria hiyo pia inakuwa batili (unconstitutional). Tunakusudia kusema kwamba, hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, yenyewe, ambayo bado inatumika hadi sasa, inadhamini UHURU wa wananchi kutowa mawazo na maoni yao kwa uhuru kabisa. Kifungu cha 18, kinachohusiana na haki ya uhuru wa mawazo kinaeleza: "Kila mtu – (a) anao uhuru wa kuwa na maoni na kueleza fikra zake". Aidha, kifungu kinachofuata cha 19-(1) nacho kinaeleza: "Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo". Pia, Katiba hiyo hiyo ya Jamhuri ya Muungano, Sehemu ya Tatu, inayohusiana na haki na wajibu muhimu, inaeleza kwenye kifungu cha 13-(2) kuwa: "Ni marufuku kwa sheria yo yote iliyotungwa na mamlaka yo yote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lo lote ambalo ni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake". Neno ubaguzi, linatafsiriwa na Katiba hiyo hiyo ya Muungano kwenye kifungu cha 13-(5) kuwa ubaguzi ni pamoja na kunyima haki ya maoni ya kisiasa. Kama hivyo ndivyo, sheria ya mabadiliko ya Katiba inakwenda kinyume na Katiba kwa kuikana haki hiyo muhimu ya maoni ya kisiasa.
Tano, UHALALI wa sheria ya mabadiliko ya Katiba hauwezi kupatikana kwa kupitishwa na Bunge pekee. Ni LAZIMA sheria hiyo ya mabadiliko ya Katiba, pia ipitishwe na kuridhiwa na kukubaliwa na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar.
Baada ya hoja na maelezo hayo, ni ukweli usio na shaka kuwa, sheria ya mabadiliko ya Katiba, sheria namba 8, haiwezi kuwa juu ya Katiba ya Zanzibar, na kwa ajili hiyo, Wazanzibari Kikatiba, tunao uhuru na haki ya kutoa maoni yetu bila ya hofu wala woga; kama ambavyo Serikali yetu nayo kupitia Katiba ya Zanzibar, ina wajibu wa kudhamini uhuru huo. Ikiwa ni kuirudisha Jamhuri ya Watu wa Zanzibar itakayofuatiwa na Muungano wa Mkataba, na si ule Muungano wa Katiba pia ni haki yetu ya Kikatiba. Zama za kutishana na kupigana zimekwisha. Hata Rais Kikwete katika hotuba yake alilisema hilo, na namnukuu: "Kwa upande wa mchakato wa kupata Katiba mpya, nawasihi Watanzania tujiandae kwa maoni ya kutoa kwenye Tume ya Katiba mara itakapoanza kazi. Tutofautiane bila kupigana". Mwisho wa kunukuu. Tunamtaka Rais Kikwete atembee juu ya kauli yake hiyo kama ambavyo nasi tutatofautiana kwa misingi ya HOJA bila ya kupigana.
Jamhuri ya Watu wa Zanzibar KWANZA!
 
1.Serikali Lazima isomeshe bure wanafunzi vyuo vikuu
2.Mifuko ya hifadhi ya jamii itoe %ya faida kwa wanachama wao na pia wakopeshe endapo wakichangia kwa mda wa mwaka miwili au waweze kutoa nusu ya michango yao kama wakichangia kwa mda wa miaka miwili,pia ukitaka kwenda kuchukua mafao yao isizid miezi miwili na pia wawafatilie waajiri wawe wanapeleka hela kila mwezi na sio wasubiri mpaka mwajiri apeleke!
 
-wastaafu wa jeshi wasiteuliwe kushika uongozi wa kisiasa ( wakuu wa mikoa,wilaya "kama nafasi hii zitaendelea kuwepo" nk)
-kama Tanganyika ilivyofutka znz nayo ifutike au kama znz ilivyo na Tanganyika nayo iwepo(serikali moja au tatu)
 
Hiyo ya kwanza juu ya adhabu...katiba si Penal Code.

Mimi nimeipenda - penal code ni nini na ni nani anajua kwangu ni kuwa mtanzania huyu ameonesha anvyochukia kitendo husika- hii inatosha kama mchango, wataalamu watajua katiba ikaeeje ili apate naye anachokitaka.
 
Katika kipindi hiki cha mchakato wa katika kila mtu atasema lake cha msingi ni kusubiri muda mwafaka ili maoni kama haya tuwapelekee wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri zetu. Nina imani yatafanyiwa kazi.
 
1. Serikali ya majimbo, itakayo angamiza kabisa wakuu wa wilaya na mikoa.
2. Marufuku mtu kuwa na utumishi pande mbili hasa wa umma na secta binafsi. Mfano mtu kuwa mbunge halafu mkuu wa mkoa/wilaya ni ushenzi wa serikali ya ccm
3. Viongozi wa majeshi wasiteuliwe na rais, bali wachaguliwe ndani ya majeshi wenyewe
4
 
Mimi nimeipenda - penal code ni nini na ni nani anajua kwangu ni kuwa mtanzania huyu ameonesha anvyochukia kitendo husika- hii inatosha kama mchango, wataalamu watajua katiba ikaeeje ili apate naye anachokitaka.
A criminal code (or penal code) is a document which compiles all, or a significant amount of, a particular jurisdiction's criminal law. Typically a criminal code will contain offences which are recognised in the jurisdiction, penalties which might be imposed for these offences and some general provisions.[SUP]http://en.wikipedia.org/wiki/Criminal_code#cite_note-0[/SUP]
 
Mimi nimeipenda - penal code ni nini na ni nani anajua kwangu ni kuwa mtanzania huyu ameonesha anvyochukia kitendo husika- hii inatosha kama mchango, wataalamu watajua katiba ikaeeje ili apate naye anachokitaka.

duh, kweli katiba itoe offences na provisions? Hapa labda angesema kwamba kiwepo kifungu kinachokataza unyonyaji wa rasilimali za nchi na kikataze viongozi kujihusisha na vitendo vya rushwa na matumizi mabaya ya ofisi.
 
  1. Cheo cha PM kiondolewe tuwe na RAIS na VP
  2. Wabunge na madiwani wa viti maalum waondolewe
  3. Ma-meya na miji/Majiji wachaguliwe direct na wananchi sio madiwani
  4. Idadi ya wizara na mawaziri itamkwe wazi kwenye katiba
  5. Wabunge wasiteuliwe kuwa mawaziri ma-RC (after hatutakuwa na ma-RC)
  6. Wananchi tuweze kumuwajibisha Rais aliyeshindwa kazi hata kama atakuwa hajamaliza term yake.
  7. Muungano wetu uwe wa Serikali 3
  8. Serikali ifute ruzuku kwenye vyama vya Siasa
  9. Mali zote zilizopatikana kwa wananchi kuchangia ambazo CCM imejimilikisha zirudishwe kwa wananchi
  10. Rais asiteue CDF, IGP, CJ, watu hao wachaguliwe na wana taalama wenyewe
 
A criminal code (or penal code) is a document which compiles all, or a significant amount of, a particular jurisdiction's criminal law. Typically a criminal code will contain offences which are recognised in the jurisdiction, penalties which might be imposed for these offences and some general provisions.

Fred -that i agree, all i am saying is if we are to let it be people's constitution the process should allow us 'lay people' from 'mandeny' to say our likes and dislikes in the most 'crude and raw' way while alowing refinement, allignment to happen under facilitation of our learned brothers and sisters
 
Back
Top Bottom