Mpiga nyungu na heka heka zake za kuitukana fani yake baada ya kukosa ajira ya ualimu. Kuna waalimu wana mawe yaani wana pesa wewe ukiwaona utajua ni ma D.E.D au wabunge kwa chuma wanazosukuma. Tatzo una akili 2
 
Hata ombi la kuhama kwenyewe kutoka shule/wilaya moja kwenda shule/wilaya nyingine ndani ya mkoa huo huo mmoja ni kwa mbinde sana.

Wapitishaji wa maombi hayo huwabania sana tena kwa makusudi kabisa. Walimu pamoja na kwamba kuna watu wanawabeza lakini kwa yale mateso wanayopitia katika nchi hii kwa hakika wanastahili heshima na pongezi kwa uvumilivu walionao.
 
Wanastahil heshima zao tuwe wakwel kabisaa.
 
Hivi mkuu mwalimu aliyeanza kazi mwaka huu mpaka anastaafu miaka 30 ijayo anaweza kupata mafao mil 200 kweli
 
Katika nchi hii nimejifunza kuwaheshimu zaidi walimu hasa wa shule za msingi na pia wote wenye petty jobs. Mungu awasaidie.
  • Kwa mtu mwenye hekima ya kulelewa vyema lazima awe na mtazamo huu
  • kwa mtu aliyepitia mazingira magum sana ya upambanaji mpaka kufanikiwa ni rahis pia kuwa na mtazamo huu
  • kwa mtu anayejali utu wa mtu ni lazima awe na mtazamo huu
 
Hivi mkuu mwalimu aliyeanza kazi mwaka huu mpaka anastaafu miaka 30 ijayo anaweza kupata mafao mil 200 kweli
Inategemeana na factors nyingi sana mdogo angu.
  • Unalipwa mshahara kiasi gani? It matters
  • Sera au policy za serikal zina change pia, miaka 30 ni mingi.
  • Pia usisahau value for money inayotemeana na hali ya kiuchumi. Mil 200 ya leo sio milion 200 ya 30 years later, mind you that too.
 
Nakumbuka miaka ile wanaweka vigezo vya kupata mikopo ya chuo, course niliyochaguliwa sikupata sifa ya kupewa mkopo.

Nikapewa option nibadili course kwenda ualimu ili nipate mkopo, nikakataa.

Nikalazimika kukaa nyumbani mwaka mzima nikijipanga, mwaka uliofuata nikapata chuo course ile ile niliyochaguliwa mwaka jana. Kwa sababu ndio course nilikua napenda.

Najiuliza, hivi kwa principle zangu hizi, ningekua mwalimu si ningekua nishafukuzwa kazi ama kuacha kazi?

Ualimu bongo ni kazi inayotaka uwe na wito na uwe na moyo.
 
Nyakati zinabadikika kamanda, walimu wa mjini huwezi kuwaendesha endesha tuu unavyojisikia. Siku hizi watu ni wajeuri hawapendi kupelekeshwa. Wakishakusoma tu uko hiv bas hawatakusumbua.
 
Mpwayungu Mimi natamani ualimu jaman sijaajiriwa na degree yangu hii tangu 2015 hao waalimu wa cheti tuu hapa nyumbani wananidharau na ni ndugu zangu [emoji24][emoji24][emoji24] usiombe najuta hata kusoma
nimeona post zako nyingi hapa jf, hakika ningekua na uwezo ningekusaidia kupata kazi.

wakulungwa msaidieni huyu madam apate riziki sehemu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…