charles ndagulla
Senior Member
- Feb 18, 2016
- 168
- 110
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru)mkoani Kilimanjaro,inawashikilia Maofisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA) wakituhumiwa kushirikiana na matapeli wanaowaumiza wananchi kwa kuwauzia vitambulisho hivyo ambavyo kwa kawaida vinapaswa kutolewa bure.
Kwenye mtandao huo wa matapeli,Takukuru ikafanikiwa kumnasa Mwalimu wa shule ya sekondari ya kutwa ya Kiusa iliyopo Kata ya Kiusa Manispaa ya Moshi,Hemed Shaaban Adinan ambaye baada ya upekuzi amekutwa na rundo la vitambulisho ambavyo vilikuwa viuzwe kwa wananchi .
Kukamatwa kwa maofisa hao kunatokana na Taarifa ya mwananchi mmoja(jina kapuni) kwenda kulalamika takukuru kuwa anadaiwa atoe rushwa ya sh,100,000 na ofisa wa NIDA ili aweze kupewa kitambulisho chake jambo mbalo ni kinyume na kifungu cha 15 cha sheria na.11 ya mwaka 2007 ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
"Mtego uliandaliwa uliopelekea kukamatwa kwa Bw.Hemed Shaaban Adinan ambaye amekuwa akijitambulisha kuwa ni afisa wa NIDA na baada ya kupekuliwa bw,Hemed alikutwa na vitambulisho ambavyo havijawafikia walengwa",amesema Holle Makungu Mkuu wa Takukuru K'njaro katika taarifa yake kwa wanahabari.
Takukuru wanasema uchunguzi zaidi unaendelea ili kubaini watumishi wa NIDA wanaohusika kumpa mwalimu huyo vitambulisho hivyo kitendo ambacho ni kinyume na kifungu cha 31 cha sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Imesema mara uchunguzi utakapokamilika hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale watakaobainika kujihusisha na uvunjaji huo wa sheria na kutoa wito kwa wananchi kutambua kwa vitambulisho hivyo vinatolewa na NIDA bureeeee.
Takukuru imesisitiza wananchi watakaodaiwa rushwa na maofisa wa NIDA ili wapatiwe vitambulisho vya uraia wa Tanzania basi wasisite kutoa taarifa ama wapige simu ya bureeeeeeeeeeeee namba 113.
Kazi kwenu wananchi mtakaoombwa pesa ili mpatiwe vitambulisho ,piga simu hiyo buree ili kuwanasa waranguzi wa vitambulisho#Rushwa ni Adui wa Haki
Kwenye mtandao huo wa matapeli,Takukuru ikafanikiwa kumnasa Mwalimu wa shule ya sekondari ya kutwa ya Kiusa iliyopo Kata ya Kiusa Manispaa ya Moshi,Hemed Shaaban Adinan ambaye baada ya upekuzi amekutwa na rundo la vitambulisho ambavyo vilikuwa viuzwe kwa wananchi .
Kukamatwa kwa maofisa hao kunatokana na Taarifa ya mwananchi mmoja(jina kapuni) kwenda kulalamika takukuru kuwa anadaiwa atoe rushwa ya sh,100,000 na ofisa wa NIDA ili aweze kupewa kitambulisho chake jambo mbalo ni kinyume na kifungu cha 15 cha sheria na.11 ya mwaka 2007 ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
"Mtego uliandaliwa uliopelekea kukamatwa kwa Bw.Hemed Shaaban Adinan ambaye amekuwa akijitambulisha kuwa ni afisa wa NIDA na baada ya kupekuliwa bw,Hemed alikutwa na vitambulisho ambavyo havijawafikia walengwa",amesema Holle Makungu Mkuu wa Takukuru K'njaro katika taarifa yake kwa wanahabari.
Takukuru wanasema uchunguzi zaidi unaendelea ili kubaini watumishi wa NIDA wanaohusika kumpa mwalimu huyo vitambulisho hivyo kitendo ambacho ni kinyume na kifungu cha 31 cha sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Imesema mara uchunguzi utakapokamilika hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale watakaobainika kujihusisha na uvunjaji huo wa sheria na kutoa wito kwa wananchi kutambua kwa vitambulisho hivyo vinatolewa na NIDA bureeeee.
Takukuru imesisitiza wananchi watakaodaiwa rushwa na maofisa wa NIDA ili wapatiwe vitambulisho vya uraia wa Tanzania basi wasisite kutoa taarifa ama wapige simu ya bureeeeeeeeeeeee namba 113.
Kazi kwenu wananchi mtakaoombwa pesa ili mpatiwe vitambulisho ,piga simu hiyo buree ili kuwanasa waranguzi wa vitambulisho#Rushwa ni Adui wa Haki