PostGE2025 Manyerere Jackton: Tatizo si Mabeberu, ni sisi wenyewe!

PostGE2025 Manyerere Jackton: Tatizo si Mabeberu, ni sisi wenyewe!

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
11,798
Reaction score
18,037
Miaka 63 iliyopita, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliandika kijitabu Tujisahihishe, akionya tabia ya kutafuta mchawi nje ya nchi kila tukipatwa na matatizo tuliyoyasababisha sisi wenyewe.

Mwalimu alisema ni rahisi kulaumu “mabeberu” au “watu kutoka nje” kuliko kujitazama na kukiri ukweli kwamba chanzo cha matatizo yetu ni uamuzi na mifumo tunayoitengeneza.

Mwalimu alisema, “Kuna tabia imekita mizizi katika siasa na jamii ya Tanganyika [Tanzania]—tabia ya kutafuta mchawi nje ya mipaka ya nchi yetu kila tunapokutana na matatizo tuliyoyazalisha sisi wenyewe. Ni rahisi sana kulaumu ‘mabeberu,’ ‘makaburu,’ au ‘watu kutoka nje,’ lakini ni vigumu sana kujikagua, kujiangalia kwenye kioo na kusema, ‘Tatizo ni sisi.’

Leo, zaidi ya nusu karne baadaye, ukweli wa maneno hayo unajidhihirisha. Matatizo mengi ya Tanzania, kuanzia KATIBA dhaifu, mfumo mbovu wa uongozi, matumizi mabaya ya madaraka, rushwa, ubaguzi kwenye elimu, misafara ya kifahari, hadi tume za uchaguzi zisizoaminika, si maagizo ya mabeberu. Beberu gani ameagiza vyombo vya habari viminywe? Ni uamuzi wa viongozi wetu wa CCM na mfumo walioujenga kwa mikono yao wenyewe.

Sasa baada ya UDINI kukwama, tunahamasishwa tuamini kuwa madhila yetu yanasababishwa na MA BEBERU ! Kama yapo, ni kidogo sana. Mengi ni matokeo ya kazi ya akili, matamanio na ubinafsi wa watawala wetu CCM...

Katiba tuliyonayo haikuandikwa Ulaya. Hakuna mzungu aliyeweka vifungu vinavyompa Rais mamlaka makubwa au vinavyokataza wananchi kuhoji matokeo ya uchaguzi mahakamani. CCM wenyewe walikataa mchakato wa KATIBA MPYA kwa UBINAFSI wao wenyewe na Raisi wa wakati ule Jakaya Mrisho KIKWETE...

Vile vile, sheria ya mafao kwa wenza wa viongozi, ukubwa wa Bunge, ongezeko la posho na safari, na matumizi makubwa ya magari ya kifahari; vyote hivi ni uamuzi wa watawala wetu CCM. Wananchi wakilalamika, wanaambiwa wametumwa na mabeberu. Huku ni kukwepa UWAJIBIKAJI kwa CCM.

Hata ubaguzi wa elimu—watoto wa viongozi kusoma shule bora na watoto wa wananchi kusukumwa kwenye shule za kata zisizo na miundombinu, si maagizo ya nje. Ni mfumo uliojengwa na CCM , unaochochea hasira na kukatisha tamaa vijana. Vivyo hivyo, tume ya uchaguzi iliyojaa shaka, misafara mikubwa ya viongozi, barabara kufungwa ili mkubwa wa CCM apite, na matumizi mabaya ya vyombo vya dola si kazi ya mataifa ya nje. Ni CCM walioamua kuunda utamaduni wa kuwatukuza viongozi kuliko nchi yao.

Kwa miaka mingi, rushwa imeota mizizi kuanzia juu hadi chini. Hakuna mkoloni aliyeagiza tuibe asilimia 10 kwenye miradi ya serikali, tuidhinishe mikataba mibovu, au tuoneane aibu tunapopaswa kuwajibishana. Huu ni udhaifu wa CCM na taasisi zake ilizoziunda, si njama za nje wala mabeberu..
Aidha, MAUAJI , UTESAJI , watu KUTEKWA na KUPOTEA, yamekuwa majeraha ya taifa LETU, yaliyosababishwa na CCM bila kushinikizwa na taifa lolote kubwa. Hakuna beberu aliyeagiza polisi wawapige raia wanaodai haki au waue watu kana kwamba wanaua nzige shambani.
Maafa ya Oktoba 29 hayakupangwa na mabeberu. Bunduki zilizoangamiza Watanzania zilishikwa na Watanzania wenyewe; mipango ya mashambulizi ilifanywa ndani ya CCM na mfumo wao wa kihalifu. Ni uamuzi wa Mwenyekiti wa CCM, si maagizo ya nje. Tukitafuta mchawi nje, tutakuwa tunazidi kukwepa ukweli unaotakiwa kutuokoa.
Mwalimu anasema kwenye TUJISAHIHISHE..., “Sababu moja ambayo ilituzuia sisi Waafrika kuendelea ni majibu ya urahisi kwa matatizo makubwa. Shamba letu kama halikutoa mavuno ya kutosha, jibu lilikuwa wazi; au limelogwa au ni amri ya Mungu. Watoto wetu walipokuwa wagonjwa daima, jibu lilikuwa rahisi; au walilogwa au ni amri ya Mungu. Nyumba yetu ilipopigwa radi ikaanguka, jibu lilikuwa rahisi; au ni uchawi au ni amri ya Mungu. Majibu ya namna hii huzuia binadamu kupata sababu za kweli za matatizo yao, na kwa hiyo yanazuia akili kutafuta njia za kweli za kuondoa matatizo hayo.”

Kwa hiyo, tusikimbilie kuwalaumu mabeberu. Matatizo ya Tanzania yametengenezwa na Watanzania wenyewe na CCM yao.., ukombozi wake uko mikononi wetu sisi WATANZANIA, kwa kuwa wakweli, KULAZIMISHA CCM kubadili mifimo, kurekebisha tabia, na kuunda KATIBA MPYA itakayotoa majibu ya kudumu.
Tanzania mpya itapatikana siku ile ambayo VIONGOZI wa CCM watawaheshimu Watanzania wote na nchi yao Tanzania.
Kama kuna urithi mkubwa Mwenyekiti wa CCM na Rais Samia Suluhu Hassan anaweza kutuachia watanzania, basi ni kutupatia KATIBA mpya, bora, shirikishi, itakayotupatia mihimili huru ya nchi, yaani BUNGE, MAHAKAMA, na SERIKALI itakayowajibika kwa watanzania.
Kwa KATIBA mpya, watanzania tutafumua na kujenga upya mifumo mibovu inayoliangamiza taifa.

Muda anao, afanye hivyo.

Manyerere J.N
Novemba 28, 2025
 
Chawa Balile na yule Prof. wa jalalani wakiona andiko hili sijui itakuwaje. Manyerere anaweza kufutiwa ithibati!

20251126_130825.jpg
 
Ameongea ukweli mchungu sana. I wish waandishi wote wa habari wangezitumia kalamu zao kwenye kuandika ukweli, badala ya kusifia tu hata mambo ya kijinga kutoka kwa watawala! Kwa malipo ya vijisenti vichache vilivyowekwa kwenye bahashaza kaki.
 
Mhariri mwenza wa Gazeti la Jamhuri, Manyerere Jackton, amedai chanzo kikuu cha matatizo ya Taifa la Tanzania si mabeberu wala mataifa ya kigeni, bali ni mifumo mibovu na maamuzi ya ndani yanayofanywa na Watanzania wenyewe, akisisitiza kuwa taifa haliwezi kupata suluhu ya kudumu bila kujitazama kwa uaminifu.

Katika makala yake ya Novemba 28, 2025, Manyerere amerejea maonyo ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere aliyoyatoa miaka 63 iliyopita kwenye kijitabu Tujisahihishe, akieleza kwamba Watanzania wameendeleza tabia ile ile ya kutafuta mchawi nje ya nchi badala ya kukiri makosa ya ndani. Anasema Mwalimu Nyerere alikwishaonya kuwa ni rahisi kulaumu “mabeberu,” “makaburu,” au “watu kutoka nje” kuliko kujikagua na kukubali kuwa “tatizo ni sisi.”

Kwa mujibu wa Manyerere, matatizo mengi yanayoikabili Tanzania kuanzia Katiba iliyojaa mianya, mfumo dhaifu wa uongozi, matumizi mabaya ya madaraka, rushwa, misafara mikubwa ya viongozi, mpaka tume za uchaguzi zisizoaminika hayajaagizwa kutoka nje bali yamejengwa na mifumo na matamanio ya Watanzania wenyewe.

“Beberu gani ameagiza vyombo vya habari viminywe? Ni uamuzi wa viongozi wetu na mfumo tulioujenga kwa mikono yetu wenyewe. Sasa baada ya udini kukwama, tunahamasishwa tuamini kuwa madhila yetu yanasababishwa na mabeberu! Kama yapo, ni kidogo sana. Mengi ni matokeo ya kazi ya akili, matamanio na ubinafsi wa watawala wetu”, ameeleza.

Aidha, Manyerere anataja ubaguzi wa kielimu unaowatenga watoto wa wananchi wa kawaida, matumizi makubwa ya posho na misafara ya kifahari, pamoja na barabara kufungwa ili viongozi wapite, akisema hakuna hata moja lililoelekezwa na mkoloni au taifa lolote la kigeni. Ameongeza kuwa vitendo vya rushwa, mikataba mibovu, maamuzi yasiyoangalia maslahi ya taifa, pamoja na ukosefu wa uthubutu wa kuwajibishana ni matokeo ya mifumo dhaifu iliyojengwa na Watanzania wenyewe.

“Kwa miaka mingi, rushwa imeota mizizi kuanzia juu hadi chini. Hakuna mkoloni aliyeagiza tuibe asilimia 10 kwenye miradi ya serikali, tuidhinishe mikataba mibovu, au....".
 
Wakuu wa shule na walimu wakuu waligeuka kubwa wenyeviti wa hamasa wa CCM na wakawa wanavalisha watoto wetu sare za chama kwenda kwenye mikutano ya siasa. Taifa lilikuwa linaenda kuwa kituko duniani.
 
Miaka 63 iliyopita, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliandika kijitabu Tujisahihishe, akionya tabia ya kutafuta mchawi nje ya nchi kila tukipatwa na matatizo tuliyoyasababisha sisi wenyewe.
 
Wakuu wa shule na walimu wakuu waligeuka kubwa wenyeviti wa hamasa wa CCM na wakawa wanavalisha watoto wetu sare za chama kwenda kwenye mikutano ya siasa. Taifa lilikuwa linaenda kuwa kituko duniani.
Baba Wa Taifa Kambarage aliamini kw akujifunza siasa za Marx, Starlin wa Urusi zingeweza kuleta mabadiliko ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Sidhani kama ni sahihi kumlaum au la lakini alikosea sana. Alikipenda sana chama kuliko Taifa.
 
Mwalimu alisema, “Kuna tabia imekita mizizi katika siasa na jamii ya Tanganyika [Tanzania]—tabia ya kutafuta mchawi nje ya mipaka ya nchi yetu kila tunapokutana na matatizo tuliyoyazalisha sisi wenyewe. Ni rahisi sana kulaumu ‘mabeberu,’ ‘makaburu,’ au ‘watu kutoka nje,’ lakini ni vigumu sana kujikagua, kujiangalia kwenye kioo na kusema, ‘Tatizo ni sisi.’
Waleta matatizo hunificha kwa kusingizia Wazungu
 
Mhariri mwenza wa Gazeti la Jamhuri, Manyerere Jackton, amedai chanzo kikuu cha matatizo ya Taifa la Tanzania si mabeberu wala mataifa ya kigeni, bali ni mifumo mibovu na maamuzi ya ndani yanayofanywa na Watanzania wenyewe, akisisitiza kuwa taifa haliwezi kupata suluhu ya kudumu bila kujitazama kwa uaminifu.
Well
 
Miaka 63 iliyopita, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliandika kijitabu Tujisahihishe, akionya tabia ya kutafuta mchawi nje ya nchi kila tukipatwa na matatizo tuliyoyasababisha sisi wenyewe.

Mwalimu alisema ni rahisi kulaumu “mabeberu” au “watu kutoka nje” kuliko kujitazama na kukiri ukweli kwamba chanzo cha matatizo yetu ni uamuzi na mifumo tunayoitengeneza.

Mwalimu alisema, “Kuna tabia imekita mizizi katika siasa na jamii ya Tanganyika [Tanzania]—tabia ya kutafuta mchawi nje ya mipaka ya nchi yetu kila tunapokutana na matatizo tuliyoyazalisha sisi wenyewe. Ni rahisi sana kulaumu ‘mabeberu,’ ‘makaburu,’ au ‘watu kutoka nje,’ lakini ni vigumu sana kujikagua, kujiangalia kwenye kioo na kusema, ‘Tatizo ni sisi.’

Leo, zaidi ya nusu karne baadaye, ukweli wa maneno hayo unajidhihirisha. Matatizo mengi ya Tanzania, kuanzia KATIBA dhaifu, mfumo mbovu wa uongozi, matumizi mabaya ya madaraka, rushwa, ubaguzi kwenye elimu, misafara ya kifahari, hadi tume za uchaguzi zisizoaminika, si maagizo ya mabeberu. Beberu gani ameagiza vyombo vya habari viminywe? Ni uamuzi wa viongozi wetu wa CCM na mfumo walioujenga kwa mikono yao wenyewe.

Sasa baada ya UDINI kukwama, tunahamasishwa tuamini kuwa madhila yetu yanasababishwa na MA BEBERU ! Kama yapo, ni kidogo sana. Mengi ni matokeo ya kazi ya akili, matamanio na ubinafsi wa watawala wetu CCM...

Katiba tuliyonayo haikuandikwa Ulaya. Hakuna mzungu aliyeweka vifungu vinavyompa Rais mamlaka makubwa au vinavyokataza wananchi kuhoji matokeo ya uchaguzi mahakamani. CCM wenyewe walikataa mchakato wa KATIBA MPYA kwa UBINAFSI wao wenyewe na Raisi wa wakati ule Jakaya Mrisho KIKWETE...

Vile vile, sheria ya mafao kwa wenza wa viongozi, ukubwa wa Bunge, ongezeko la posho na safari, na matumizi makubwa ya magari ya kifahari; vyote hivi ni uamuzi wa watawala wetu CCM. Wananchi wakilalamika, wanaambiwa wametumwa na mabeberu. Huku ni kukwepa UWAJIBIKAJI kwa CCM.

Hata ubaguzi wa elimu—watoto wa viongozi kusoma shule bora na watoto wa wananchi kusukumwa kwenye shule za kata zisizo na miundombinu, si maagizo ya nje. Ni mfumo uliojengwa na CCM , unaochochea hasira na kukatisha tamaa vijana. Vivyo hivyo, tume ya uchaguzi iliyojaa shaka, misafara mikubwa ya viongozi, barabara kufungwa ili mkubwa wa CCM apite, na matumizi mabaya ya vyombo vya dola si kazi ya mataifa ya nje. Ni CCM walioamua kuunda utamaduni wa kuwatukuza viongozi kuliko nchi yao.

Kwa miaka mingi, rushwa imeota mizizi kuanzia juu hadi chini. Hakuna mkoloni aliyeagiza tuibe asilimia 10 kwenye miradi ya serikali, tuidhinishe mikataba mibovu, au tuoneane aibu tunapopaswa kuwajibishana. Huu ni udhaifu wa CCM na taasisi zake ilizoziunda, si njama za nje wala mabeberu..
Aidha, MAUAJI , UTESAJI , watu KUTEKWA na KUPOTEA, yamekuwa majeraha ya taifa LETU, yaliyosababishwa na CCM bila kushinikizwa na taifa lolote kubwa. Hakuna beberu aliyeagiza polisi wawapige raia wanaodai haki au waue watu kana kwamba wanaua nzige shambani.
Maafa ya Oktoba 29 hayakupangwa na mabeberu. Bunduki zilizoangamiza Watanzania zilishikwa na Watanzania wenyewe; mipango ya mashambulizi ilifanywa ndani ya CCM na mfumo wao wa kihalifu. Ni uamuzi wa Mwenyekiti wa CCM, si maagizo ya nje. Tukitafuta mchawi nje, tutakuwa tunazidi kukwepa ukweli unaotakiwa kutuokoa.
Mwalimu anasema kwenye TUJISAHIHISHE..., “Sababu moja ambayo ilituzuia sisi Waafrika kuendelea ni majibu ya urahisi kwa matatizo makubwa. Shamba letu kama halikutoa mavuno ya kutosha, jibu lilikuwa wazi; au limelogwa au ni amri ya Mungu. Watoto wetu walipokuwa wagonjwa daima, jibu lilikuwa rahisi; au walilogwa au ni amri ya Mungu. Nyumba yetu ilipopigwa radi ikaanguka, jibu lilikuwa rahisi; au ni uchawi au ni amri ya Mungu. Majibu ya namna hii huzuia binadamu kupata sababu za kweli za matatizo yao, na kwa hiyo yanazuia akili kutafuta njia za kweli za kuondoa matatizo hayo.”

Kwa hiyo, tusikimbilie kuwalaumu mabeberu. Matatizo ya Tanzania yametengenezwa na Watanzania wenyewe na CCM yao.., ukombozi wake uko mikononi wetu sisi WATANZANIA, kwa kuwa wakweli, KULAZIMISHA CCM kubadili mifimo, kurekebisha tabia, na kuunda KATIBA MPYA itakayotoa majibu ya kudumu.
Tanzania mpya itapatikana siku ile ambayo VIONGOZI wa CCM watawaheshimu Watanzania wote na nchi yao Tanzania.
Kama kuna urithi mkubwa Mwenyekiti wa CCM na Rais Samia Suluhu Hassan anaweza kutuachia watanzania, basi ni kutupatia KATIBA mpya, bora, shirikishi, itakayotupatia mihimili huru ya nchi, yaani BUNGE, MAHAKAMA, na SERIKALI itakayowajibika kwa watanzania.
Kwa KATIBA mpya, watanzania tutafumua na kujenga upya mifumo mibovu inayoliangamiza taifa.

Muda anao, afanye hivyo.

Manyerere J.N
Novemba 28, 2025
Kwa hii CCM ya sasa, serikali(haramu) iliyopo, mashabiki na chawa wa huu utawala pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama hawawezi kulielewa wala kuliafiki hili bandiko.
 
Vile vile, sheria ya mafao kwa wenza wa viongozi, ukubwa wa Bunge, ongezeko la posho na safari, na matumizi makubwa ya magari ya kifahari; vyote hivi ni uamuzi wa watawala wetu CCM.
Nchi ikimbolewa haya yote yatabaki kuwa historia.
 
Wasije wakamwagia Tindikali . Wahariri kama huyu ni wa kupewa nafasi na kuwezeshwa watusadie kwenye maridhiano feki
 
Miaka 63 iliyopita, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliandika kijitabu Tujisahihishe, akionya tabia ya kutafuta mchawi nje ya nchi kila tukipatwa na matatizo tuliyoyasababisha sisi wenyewe.

Mwalimu alisema ni rahisi kulaumu “mabeberu” au “watu kutoka nje” kuliko kujitazama na kukiri ukweli kwamba chanzo cha matatizo yetu ni uamuzi na mifumo tunayoitengeneza.

Mwalimu alisema, “Kuna tabia imekita mizizi katika siasa na jamii ya Tanganyika [Tanzania]—tabia ya kutafuta mchawi nje ya mipaka ya nchi yetu kila tunapokutana na matatizo tuliyoyazalisha sisi wenyewe. Ni rahisi sana kulaumu ‘mabeberu,’ ‘makaburu,’ au ‘watu kutoka nje,’ lakini ni vigumu sana kujikagua, kujiangalia kwenye kioo na kusema, ‘Tatizo ni sisi.’

Leo, zaidi ya nusu karne baadaye, ukweli wa maneno hayo unajidhihirisha. Matatizo mengi ya Tanzania, kuanzia KATIBA dhaifu, mfumo mbovu wa uongozi, matumizi mabaya ya madaraka, rushwa, ubaguzi kwenye elimu, misafara ya kifahari, hadi tume za uchaguzi zisizoaminika, si maagizo ya mabeberu. Beberu gani ameagiza vyombo vya habari viminywe? Ni uamuzi wa viongozi wetu wa CCM na mfumo walioujenga kwa mikono yao wenyewe.

Sasa baada ya UDINI kukwama, tunahamasishwa tuamini kuwa madhila yetu yanasababishwa na MA BEBERU ! Kama yapo, ni kidogo sana. Mengi ni matokeo ya kazi ya akili, matamanio na ubinafsi wa watawala wetu CCM...

Katiba tuliyonayo haikuandikwa Ulaya. Hakuna mzungu aliyeweka vifungu vinavyompa Rais mamlaka makubwa au vinavyokataza wananchi kuhoji matokeo ya uchaguzi mahakamani. CCM wenyewe walikataa mchakato wa KATIBA MPYA kwa UBINAFSI wao wenyewe na Raisi wa wakati ule Jakaya Mrisho KIKWETE...

Vile vile, sheria ya mafao kwa wenza wa viongozi, ukubwa wa Bunge, ongezeko la posho na safari, na matumizi makubwa ya magari ya kifahari; vyote hivi ni uamuzi wa watawala wetu CCM. Wananchi wakilalamika, wanaambiwa wametumwa na mabeberu. Huku ni kukwepa UWAJIBIKAJI kwa CCM.

Hata ubaguzi wa elimu—watoto wa viongozi kusoma shule bora na watoto wa wananchi kusukumwa kwenye shule za kata zisizo na miundombinu, si maagizo ya nje. Ni mfumo uliojengwa na CCM , unaochochea hasira na kukatisha tamaa vijana. Vivyo hivyo, tume ya uchaguzi iliyojaa shaka, misafara mikubwa ya viongozi, barabara kufungwa ili mkubwa wa CCM apite, na matumizi mabaya ya vyombo vya dola si kazi ya mataifa ya nje. Ni CCM walioamua kuunda utamaduni wa kuwatukuza viongozi kuliko nchi yao.

Kwa miaka mingi, rushwa imeota mizizi kuanzia juu hadi chini. Hakuna mkoloni aliyeagiza tuibe asilimia 10 kwenye miradi ya serikali, tuidhinishe mikataba mibovu, au tuoneane aibu tunapopaswa kuwajibishana. Huu ni udhaifu wa CCM na taasisi zake ilizoziunda, si njama za nje wala mabeberu..
Aidha, MAUAJI , UTESAJI , watu KUTEKWA na KUPOTEA, yamekuwa majeraha ya taifa LETU, yaliyosababishwa na CCM bila kushinikizwa na taifa lolote kubwa. Hakuna beberu aliyeagiza polisi wawapige raia wanaodai haki au waue watu kana kwamba wanaua nzige shambani.
Maafa ya Oktoba 29 hayakupangwa na mabeberu. Bunduki zilizoangamiza Watanzania zilishikwa na Watanzania wenyewe; mipango ya mashambulizi ilifanywa ndani ya CCM na mfumo wao wa kihalifu. Ni uamuzi wa Mwenyekiti wa CCM, si maagizo ya nje. Tukitafuta mchawi nje, tutakuwa tunazidi kukwepa ukweli unaotakiwa kutuokoa.
Mwalimu anasema kwenye TUJISAHIHISHE..., “Sababu moja ambayo ilituzuia sisi Waafrika kuendelea ni majibu ya urahisi kwa matatizo makubwa. Shamba letu kama halikutoa mavuno ya kutosha, jibu lilikuwa wazi; au limelogwa au ni amri ya Mungu. Watoto wetu walipokuwa wagonjwa daima, jibu lilikuwa rahisi; au walilogwa au ni amri ya Mungu. Nyumba yetu ilipopigwa radi ikaanguka, jibu lilikuwa rahisi; au ni uchawi au ni amri ya Mungu. Majibu ya namna hii huzuia binadamu kupata sababu za kweli za matatizo yao, na kwa hiyo yanazuia akili kutafuta njia za kweli za kuondoa matatizo hayo.”

Kwa hiyo, tusikimbilie kuwalaumu mabeberu. Matatizo ya Tanzania yametengenezwa na Watanzania wenyewe na CCM yao.., ukombozi wake uko mikononi wetu sisi WATANZANIA, kwa kuwa wakweli, KULAZIMISHA CCM kubadili mifimo, kurekebisha tabia, na kuunda KATIBA MPYA itakayotoa majibu ya kudumu.
Tanzania mpya itapatikana siku ile ambayo VIONGOZI wa CCM watawaheshimu Watanzania wote na nchi yao Tanzania.
Kama kuna urithi mkubwa Mwenyekiti wa CCM na Rais Samia Suluhu Hassan anaweza kutuachia watanzania, basi ni kutupatia KATIBA mpya, bora, shirikishi, itakayotupatia mihimili huru ya nchi, yaani BUNGE, MAHAKAMA, na SERIKALI itakayowajibika kwa watanzania.
Kwa KATIBA mpya, watanzania tutafumua na kujenga upya mifumo mibovu inayoliangamiza taifa.

Muda anao, afanye hivyo.

Manyerere J.N
Novemba 28, 2025
Tatizo ni sisi wenyewe na mabeberu pia wanachangia, haya mambo si Tanzania tu, ni sura pana ya bara zima. Lakini ili kuelewa “tatizo ni nani?” tunahitaji kuangalia mambo kwa upana zaidi kuliko lawama za haraka kwa mtu mmoja au kundi moja. Tatizo la Afrika ni mchanganyiko wa mambo ya nje na ya ndani, na mara nyingi haya mambo yanashikana kama nyuzi za kamba moja.

Kwa sababu mataifa mengi ya Afrika yalijengwa juu ya msingi mmoja mmbovu:
  • Mipaka ya kibeberu ya kugawa makabila bila mantiki,
  • uchumi wa kuuza malighafi badala ya kuzalisha bidhaa,
  • mifumo ya utawala iliyotengenezwa kulinda maslahi ya nje,
  • na kutegemea misaada badala ya kujitegemea.
Hivyo nchi 54 tofauti zina historia tofauti lakini tatizo la msingi ni moja: zilianza safari ya uhuru zikiwa zimefungwa mikono kiuchumi, kielimu na kiteknolojia.

Si kwamba Waafrika ni dhaifu kiakili—hapana. Tatizo ni:
  • mifumo ya elimu inayofundisha kutii, si kutengeneza,
  • uchumi ambapo mwenye malighafi si tajiri, bali anayezisindika,
  • siasa zinazolinda madaraka, si ufanisi,
  • na ukosefu wa taasisi huru zinazoweka uwajibikaji.
Mtu anaweza kuwa mwerevu binafsi, lakini mfumo mbovu wenyewe unazaa matokeo mabovu.

Nyerere alikuwa na nia, falsafa na uzalendo wa kweli. Lakini:
  1. Alipambana na mfumo wa kikoloni ambao ulikuwa bado una nguvu baada ya uhuru.
  2. Aliongoza taifa maskini bila miundombinu madhubuti na wataalamu wachache.
  3. Alikumbana na vikwazo vya nguvu kubwa za kimataifa wakati wa Vita Baridi—mataifa makubwa yalidhibiti misaada, biashara, silaha, mikopo, bei za mazao, kila kitu.
  4. Jaribio la ujamaa liligongana na uhalisia wa uchumi mdogo na ukosefu wa teknolojia.
Kwa lugha rahisi: Nyerere alikuwa na nia, lakini dunia aliyoishi ndani yake haikumruhusu kutekeleza yote aliyotamani.

Mchawi wa nje (External Factor)
  • Makampuni makubwa ya kimataifa yanayodhibiti madini, mafuta, nishati, mazao.
  • Mifumo ya kifedha ya kimataifa (IMF, World Bank) yenye masharti mazito.
  • Bei za kimataifa zinazoamuliwa na wengine.
  • Utandawazi unaoweka Afrika kama soko, si kama mtengenezaji.
  • Taarifa na teknolojia kudhibitiwa na mataifa yenye nguvu.
️ Mchawi wa ndani (Internal factors)
  • Viongozi waliowekwa au kutegemewa na maslahi ya nje.
  • Rushwa na udhaifu wa taasisi—hata kiongozi mzuri anashindwa bila mfumo imara.
  • Kutojenga uchumi wa ndani, viwanda, na ubunifu.
  • Migawanyiko ya kikabila, kidini na kisiasa inayotumika kutawala watu kwa kuwagawa.
  • Kutojifunza kutoka kwa nchi zilizofanikiwa.
Kwa kifupi:

Mchawi sio mtu mmoja. Ni muunganiko wa mifumo ya nje + unyonge wa ndani.
Afrika iling’olewa meno ikapewa nafasi ya kula nyama.

Suluhu ni tatu:
  1. Kujenga taasisi imara kuliko watu.
  2. Kubadili uchumi kutoka kuuza malighafi kwenda kuzalisha bidhaa.
  3. Kuwekeza sana kwenye elimu ya sayansi, teknolojia, viwanda na utafiti.
 
Toka ccm imeanza kutawala kwa shuruti, huyu ni baadhi ya wanahabari wachache walioamua kuandika ukweli kwa maana ya ukweli. Nadhani mtu kama Balile ukweli huu anaujua vyema, lakini maslahi yake binafsi ni muhimu kuliko ukweli huu. Ccm ifahamu ukweli unafahamika, lakini walio wengi wanaogopa kuusema maana ni hatari kwao.
 
Chawa Balile na yule Prof. wa jalalani wakiona andiko hili sijui itakuwaje. Manyerere anaweza kufutiwa ithibati!

View attachment 3509124
Bora yeye anaakili anaongea na wana ccm wenzake huko mafichoni.

Nchi hii haina wana habari ni makada wa ccm wanaandikiwa habari na ccm wanaambiwa waweke vichwa vya habari na vina kuwa edited na ccm.

Ndio maana unakuta magazeti yooote nchini yana habari na picha zinafanana kasoro vichwa vya habari zao tofauti kidogo.

Ni mjinga tu anaweza kupoteza pesa kununua vifungashio vya miogo ya kuchoma, ukiita gazeti.

Mtu una simu unawezaje kujipumbaza unasoma, gazeti tanzania?

Hao kina manyerere wanapima upepo tu wote ccm, tafuta vi blog vyao utaona vimejaa mapicha picha ya samuya, uwt na uvcc.

Msikubali shetani akawa mwalimu wa neno la Mungu na mkamuita sijui nani.

Uozo ni uozo haijalishi ni keki au taka taka zingine, likivunda lime vunda.
 
Back
Top Bottom