Taifa Digital Forum
Member
- Jun 4, 2022
- 68
- 184
Ameeleza Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa.
1. Kupunguza muda wa meli kukaa nangani kutoka siku 5 kwa sasa mpaka masaa 24. Hii itapunguza gharama za utumiaji wa Bandari yetu.
2. Kuongeza idadi ya meli zitazokuja Bandari ya Dar es Salaam kutoka meli 1,569 zilizohudumiwa mwaka 2021/22 mpaka kufikia takriban meli 2,950 ifikapo mwaka 2032/33;
3. Kupunguza muda wa ushushaji wa makontena kutoka siku 4.5 mpaka siku 2
4. Kupunguza muda wa uondoshaji mizigo kutoka masaa 12 mpaka saa 1 kutokana na uboreshaji Wa mifumo yạ TEHAMA;
5. Kupunguza gharama ya usafirishaji wa shehena kutoka nchi za nje kwenda nchi za jirani, kwa mfano kutoka US$ 12,000 mpaka kati ya US$6,000 na US$7,000 kwa kasha linalokwenda nchi ya
Malawi, Zambia au DRC. Hii italeta Watumiaji wengi kwenye Bandari ya Dar es Salaam;
6. Kuongezeka kwa shehena inayohudumiwa kutoka_tani milioni 18.41 za mwaka 2021/22 hadi kufikia tani 47.57 mwaka 2032/33 sawa na ongezeko la asilimia 158,
7. Kuongezeka kwa Mapato ya Serikali yatokanayo na Kodi ya Forodha inayokusanywa katika shehena inayopitishwa bandarini kutoka Shilingi Trilioni 7.76 za mwaka 2021/22 hadi Shilingi Trilioni 26.70 za mwaka 2032/33, sawa na ongezeko la asilimia 244;
8. Kuongezeka kwa ajira zinazotokana na shughuli za bandari kutoka 28,990 mwaka 2021/22 hadi 71,907 ifikapo mwaka 2032/33, sawa na ongezeko la asilimia 148;
9. Maboresho ya magati ya kuhudumia Majahazi na Abiria ikiwa ni pamoja na kushawishi uingiaji wa meli kubwa za kitali zitakazo ongeza idadi ya watalii nchini na kuongeza pato la Taifa;
10. Mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wa TPA katika Bandari zote (knowledge and skills transfer);
11. Uanzishaji wa maeneo huru ya kiuchumi na kuchochea ukuaji wa sekta zingine za kiuchumi zikiwemo: Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi; Utali; Viwanda na Biashara;
12. Kuchagiza ukuaji wa sekta ndogo za usafirishaji kwa njia ya reli (SGR, TAZARA na MGR) na barabara; na kujenga mahusiano ya kidiplomasia.
Taifa Digital Forum
Mtazamo Halisi, Ufumbuzi wa Kweli.
10 Juni, 2022.
1. Kupunguza muda wa meli kukaa nangani kutoka siku 5 kwa sasa mpaka masaa 24. Hii itapunguza gharama za utumiaji wa Bandari yetu.
2. Kuongeza idadi ya meli zitazokuja Bandari ya Dar es Salaam kutoka meli 1,569 zilizohudumiwa mwaka 2021/22 mpaka kufikia takriban meli 2,950 ifikapo mwaka 2032/33;
3. Kupunguza muda wa ushushaji wa makontena kutoka siku 4.5 mpaka siku 2
4. Kupunguza muda wa uondoshaji mizigo kutoka masaa 12 mpaka saa 1 kutokana na uboreshaji Wa mifumo yạ TEHAMA;
5. Kupunguza gharama ya usafirishaji wa shehena kutoka nchi za nje kwenda nchi za jirani, kwa mfano kutoka US$ 12,000 mpaka kati ya US$6,000 na US$7,000 kwa kasha linalokwenda nchi ya
Malawi, Zambia au DRC. Hii italeta Watumiaji wengi kwenye Bandari ya Dar es Salaam;
6. Kuongezeka kwa shehena inayohudumiwa kutoka_tani milioni 18.41 za mwaka 2021/22 hadi kufikia tani 47.57 mwaka 2032/33 sawa na ongezeko la asilimia 158,
7. Kuongezeka kwa Mapato ya Serikali yatokanayo na Kodi ya Forodha inayokusanywa katika shehena inayopitishwa bandarini kutoka Shilingi Trilioni 7.76 za mwaka 2021/22 hadi Shilingi Trilioni 26.70 za mwaka 2032/33, sawa na ongezeko la asilimia 244;
8. Kuongezeka kwa ajira zinazotokana na shughuli za bandari kutoka 28,990 mwaka 2021/22 hadi 71,907 ifikapo mwaka 2032/33, sawa na ongezeko la asilimia 148;
9. Maboresho ya magati ya kuhudumia Majahazi na Abiria ikiwa ni pamoja na kushawishi uingiaji wa meli kubwa za kitali zitakazo ongeza idadi ya watalii nchini na kuongeza pato la Taifa;
10. Mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wa TPA katika Bandari zote (knowledge and skills transfer);
11. Uanzishaji wa maeneo huru ya kiuchumi na kuchochea ukuaji wa sekta zingine za kiuchumi zikiwemo: Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi; Utali; Viwanda na Biashara;
12. Kuchagiza ukuaji wa sekta ndogo za usafirishaji kwa njia ya reli (SGR, TAZARA na MGR) na barabara; na kujenga mahusiano ya kidiplomasia.
Taifa Digital Forum
Mtazamo Halisi, Ufumbuzi wa Kweli.
10 Juni, 2022.