Kada wa chama cha Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Sengerema , Alex Manji amekanusha uvumi unaonezwa dhidi yake kuwa amerejea kwenye chama chake zamani , Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
"Nilijiondoa CHADEMA baada ya kuona na kuridhika na mipangilio ya utekelezaji wa ahadi za serikali ya CCM kwa kuleta maendeleo,ikiwemo miundombinu ya barabara. Kwa kweli kazi nzuri zimefanyika na nyingi ya ahadi zimetimizwa".Alisema Manji.
Aliendelea kusema "Hao wanaoeneza uongo kwamba nimerejea CHADEMA wana nia ovu dhidi yangu hivyo wananchi na wana CCM wawapuuze na siasa zao chafu na majitaka.
Mimi bado ni mwana-CCM safi".Alisema anafahamu chanzo cha kuenezwa kwa uvumi huo ni baada ya kuonesha nia ya kuwania ubunge , lakini akadai ni baada ya kuangalia na kubaini jimbo lipi ambalo maendeleo yake ni duni sababu ya mbunge kushindwa kutimiza ahadi , huko ndiko atajitosa ili awatumikie wananchi.
Source: Majira
"Nilijiondoa CHADEMA baada ya kuona na kuridhika na mipangilio ya utekelezaji wa ahadi za serikali ya CCM kwa kuleta maendeleo,ikiwemo miundombinu ya barabara. Kwa kweli kazi nzuri zimefanyika na nyingi ya ahadi zimetimizwa".Alisema Manji.
Aliendelea kusema "Hao wanaoeneza uongo kwamba nimerejea CHADEMA wana nia ovu dhidi yangu hivyo wananchi na wana CCM wawapuuze na siasa zao chafu na majitaka.
Mimi bado ni mwana-CCM safi".Alisema anafahamu chanzo cha kuenezwa kwa uvumi huo ni baada ya kuonesha nia ya kuwania ubunge , lakini akadai ni baada ya kuangalia na kubaini jimbo lipi ambalo maendeleo yake ni duni sababu ya mbunge kushindwa kutimiza ahadi , huko ndiko atajitosa ili awatumikie wananchi.
Source: Majira