amba.nkya
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 446
- 131
Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kimetangaza kuwa kitaandaa mkutano wa faragha kwa viongozi wa vyama vya siasa vyenye wabunge na kuwaalika watu mashuhuri ili kutafakari hali na mwenendo wa Bunge Maalum la Katiba na kutafuta suluhu kabla halijaingia awamu ya pili ya majadiliano.
Bunge hilo lilikumbwa na mgawanyiko Aprili 16, mwaka huu baada ya wajumbe kutoka Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wake na kile walichosema upendeleo na uchakachuaji wa Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Kauli hiyo ilitolewa na Makamu Mwenyekiti wa TCD, Philip Mangula, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana kuhusu kikao cha TCD kilichofanyika Jumapili iliyopita kwa lengo la kujenga maelewano katika Bunge Maalum la Katiba.
Mangula ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, alisema kamati ya ufundi (TC) ya TCD ilipendekeza uandaliwe mkutano wa faragha wa siku mbili ili kutafakari hali na mwenendo wa Bunge hilo ambalo linatarajia kukutana tena katika awamu ya pili na ya mwisho kwa siku 60 kuanzia Agosti 5, mwaka huu.
Mangula alisema ilipendekezwa na TC ya TCD katika faragha hiyo wangealikwa pia baadhi ya watu mashuhuri nchini wajumuike na wajumbe wa TCD katika kupata maridhiano kuhusu mwenendo wa Bunge hilo kwa nia ya kulinusuru.
"Ni katika kupata ufumbuzi wa mwenendo mzima wa ushiriki wa vyama vyote vya siasa ambavyo ndiyo wadau wakuu na muhimu wa mchakato huu kabla Bunge la katiba halijaingia awamu ya pili ya majadiliano ambayo yataanza Agosti," alisema Mangula.
Alibainisha kuwa hatua hiyo ilichukuliwa baada ya baadhi ya vyama kususia Bunge hilo na kutoka nje ya Bunge Maalum la Katiba.
Wajumbe wa Ukawa waliosusia Bunge hilo ni kutoka vyama vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi. Hata hivyo, baadhi ya wajumbe wa vyama vingine nje ya Ukawa walisusia bunge hilo.
Miongoni mwao ni Mwenyekiti wa United Democratic (UDP), John Cheyo; Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila na Mwenyekiti wa National League for Democracy (NLD), Dk. Emmanuel Makaidi.
Mangula alisema lengo na madhumuni ya majadiliano hayo ni kuona sababu zilizowafanya baadhi ya washiriki wa Bunge hilo kususia.
Kwa mujibu wa Mangula wajumbe wa TCD walishindwa kukamilisha maandalizi ya mkutano huo kutokana na kutokuwapo wawakilishi wa vyama vya Chadema na CUF ambao hawakuhudhuria ili kupata maelezo fasaha kuhusu sababu zilizowalazimisha kususia Bunge Maalum la Katiba licha ya kuwapo kanuni na taratibu za kutatua matatizo na kutokuelewana katika Bunge hilo.
"TCD ni kama imepasuka, tunataka kutanzua vyama sita vilitoka vyama 16 vilibaki na vyama vitatu vilirudi na hawa waliorudi wanasema walipotoka, walidhani ilikuwa kwa muda tu na wamerudi kuendelea," alisema na kuongeza:
"Ndiyo maana walirudi … tunataka njia nzuri ya kujenga na kuendeleza umoja wa kitaifa katika nchi yetu."
Kadhalika, Mangula alisema wajumbe pia walikubaliana kuitisha kikao cha Baraza la taifa la vyama vya siasa litakalojumuisha vyama vyote 22 vyenye usajili wa kudumu ili kuendelea kutafakari mchakato wa awamu ya pili ya Bunge Maalum la Katiba.
TCD inaundwa na vyama vyenye wabunge ambavyo ni CCM, Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, UDP na TLP.
Wakati TCD inasaka mwafaka, CCM kilishatangaza kwamba hakitakuwa tayari kwa ajili ya mazungumzo na Ukawa wala kuiruhusu serikali yake kuwabembeleza wajumbe wa umoja huo kurejea bungeni.
Uamuzi huo ulifikiwa na Kamati Kuu (CC) ya chama hicho mwezi uliopita na kwamba hatua inayofuata ni kwa viongozi wake nao kwenda kwa wananchi kuwaeleza ukweli kama Ukawa wanavyofanya.
Sababu kubwa iliyowafanya Ukawa kususia Bunge hilo ni uamuzi wa CCM kukataa mapendekezo ya rasimu ya Tume ya Jaji Joseph Warioba sura ya kwanza na ya sita kuhusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na muundo wa Muungano.
Rasimu hiyo inapendekeza kuitwa Shirikisho na muundo wa serikali tatu, mapendekezo ambayo CCM inayapinga.
Akitangaza uamuzi wa Ukawa kujiengua kwenye Bunge hilo, Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba, alisema kuwa wamechoshwa na ubaguzi na uchakachuaji wa Rasimu ya Katiba kwa maana hiyo wanajiondoa bungeni ili kuwaacha ‘Nterahamwe' kuendelea na ubaguzi wao.
Chanzo: Nipashe - 11/06/2014
Bunge hilo lilikumbwa na mgawanyiko Aprili 16, mwaka huu baada ya wajumbe kutoka Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wake na kile walichosema upendeleo na uchakachuaji wa Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Kauli hiyo ilitolewa na Makamu Mwenyekiti wa TCD, Philip Mangula, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana kuhusu kikao cha TCD kilichofanyika Jumapili iliyopita kwa lengo la kujenga maelewano katika Bunge Maalum la Katiba.
Mangula ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, alisema kamati ya ufundi (TC) ya TCD ilipendekeza uandaliwe mkutano wa faragha wa siku mbili ili kutafakari hali na mwenendo wa Bunge hilo ambalo linatarajia kukutana tena katika awamu ya pili na ya mwisho kwa siku 60 kuanzia Agosti 5, mwaka huu.
Mangula alisema ilipendekezwa na TC ya TCD katika faragha hiyo wangealikwa pia baadhi ya watu mashuhuri nchini wajumuike na wajumbe wa TCD katika kupata maridhiano kuhusu mwenendo wa Bunge hilo kwa nia ya kulinusuru.
"Ni katika kupata ufumbuzi wa mwenendo mzima wa ushiriki wa vyama vyote vya siasa ambavyo ndiyo wadau wakuu na muhimu wa mchakato huu kabla Bunge la katiba halijaingia awamu ya pili ya majadiliano ambayo yataanza Agosti," alisema Mangula.
Alibainisha kuwa hatua hiyo ilichukuliwa baada ya baadhi ya vyama kususia Bunge hilo na kutoka nje ya Bunge Maalum la Katiba.
Wajumbe wa Ukawa waliosusia Bunge hilo ni kutoka vyama vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi. Hata hivyo, baadhi ya wajumbe wa vyama vingine nje ya Ukawa walisusia bunge hilo.
Miongoni mwao ni Mwenyekiti wa United Democratic (UDP), John Cheyo; Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila na Mwenyekiti wa National League for Democracy (NLD), Dk. Emmanuel Makaidi.
Mangula alisema lengo na madhumuni ya majadiliano hayo ni kuona sababu zilizowafanya baadhi ya washiriki wa Bunge hilo kususia.
Kwa mujibu wa Mangula wajumbe wa TCD walishindwa kukamilisha maandalizi ya mkutano huo kutokana na kutokuwapo wawakilishi wa vyama vya Chadema na CUF ambao hawakuhudhuria ili kupata maelezo fasaha kuhusu sababu zilizowalazimisha kususia Bunge Maalum la Katiba licha ya kuwapo kanuni na taratibu za kutatua matatizo na kutokuelewana katika Bunge hilo.
"TCD ni kama imepasuka, tunataka kutanzua vyama sita vilitoka vyama 16 vilibaki na vyama vitatu vilirudi na hawa waliorudi wanasema walipotoka, walidhani ilikuwa kwa muda tu na wamerudi kuendelea," alisema na kuongeza:
"Ndiyo maana walirudi … tunataka njia nzuri ya kujenga na kuendeleza umoja wa kitaifa katika nchi yetu."
Kadhalika, Mangula alisema wajumbe pia walikubaliana kuitisha kikao cha Baraza la taifa la vyama vya siasa litakalojumuisha vyama vyote 22 vyenye usajili wa kudumu ili kuendelea kutafakari mchakato wa awamu ya pili ya Bunge Maalum la Katiba.
TCD inaundwa na vyama vyenye wabunge ambavyo ni CCM, Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, UDP na TLP.
Wakati TCD inasaka mwafaka, CCM kilishatangaza kwamba hakitakuwa tayari kwa ajili ya mazungumzo na Ukawa wala kuiruhusu serikali yake kuwabembeleza wajumbe wa umoja huo kurejea bungeni.
Uamuzi huo ulifikiwa na Kamati Kuu (CC) ya chama hicho mwezi uliopita na kwamba hatua inayofuata ni kwa viongozi wake nao kwenda kwa wananchi kuwaeleza ukweli kama Ukawa wanavyofanya.
Sababu kubwa iliyowafanya Ukawa kususia Bunge hilo ni uamuzi wa CCM kukataa mapendekezo ya rasimu ya Tume ya Jaji Joseph Warioba sura ya kwanza na ya sita kuhusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na muundo wa Muungano.
Rasimu hiyo inapendekeza kuitwa Shirikisho na muundo wa serikali tatu, mapendekezo ambayo CCM inayapinga.
Akitangaza uamuzi wa Ukawa kujiengua kwenye Bunge hilo, Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba, alisema kuwa wamechoshwa na ubaguzi na uchakachuaji wa Rasimu ya Katiba kwa maana hiyo wanajiondoa bungeni ili kuwaacha ‘Nterahamwe' kuendelea na ubaguzi wao.
Chanzo: Nipashe - 11/06/2014