lost Crown prince
Member
- Jun 12, 2015
- 58
- 24
Habari wa kuu,
Nakumbuka kitambo siku moja nilikuwa napiga story na shangazi Yangu kuhusu maswala ya ndoa ndipo akaniuliza kuwa ninapenda kuoa mwanamke wa namna gani, nikamwambia ninapenda mwanamke mzuri sana ndio awe mke wangu,lakini yeye akaniambia namnukuu "wanawake wazuri kwa muonekano wengi wanamatatizo sana.
Wengi huwa hawana malengo na hawawezi kuvumilia shida,ukiwapa ugali wa dona na chips yai lazima watachagua chips yai kwa sababu wanapenda vitamu na siyo vitu vyenye faida,wanawake wazuri wanavitimbi ambavyo wanaume wengi hawawezi kuvumilia, mwanangu oa mwanamke mwenye uzuri wa moyo na matendo upate kuyafurahia maisha ya ndoa, achana na mwanamke mzuri sana kwa sura na umbo atakutesa nafsi yako."
Hayo maneno aliniambia miaka 7 iliyopita hapa katikati nilifanikiwa kuwa na wasichana wazuri sana kwa sura na maumbo katika mahusiano lakini wote niliachana nao kutokana na kutokuwa waminifu, sasa nashukuru mungu nimepata msichana wa kawaida ananipenda sana na hivi sasa tupo kwenye utaratibu wa kufunga ndoa, sio siri huyu dada ananipenda sana na ananiheshimu sijawahi kupendwa hivi tangu nizaliwe. Maneno ya shangazi yametimia"mwanangu oa mwanamke mwenye uzuri wa moyo na matendo upate kufurahia maisha ya ndoa".
Nadhani mtakuwa mmejifunza
Nakumbuka kitambo siku moja nilikuwa napiga story na shangazi Yangu kuhusu maswala ya ndoa ndipo akaniuliza kuwa ninapenda kuoa mwanamke wa namna gani, nikamwambia ninapenda mwanamke mzuri sana ndio awe mke wangu,lakini yeye akaniambia namnukuu "wanawake wazuri kwa muonekano wengi wanamatatizo sana.
Wengi huwa hawana malengo na hawawezi kuvumilia shida,ukiwapa ugali wa dona na chips yai lazima watachagua chips yai kwa sababu wanapenda vitamu na siyo vitu vyenye faida,wanawake wazuri wanavitimbi ambavyo wanaume wengi hawawezi kuvumilia, mwanangu oa mwanamke mwenye uzuri wa moyo na matendo upate kuyafurahia maisha ya ndoa, achana na mwanamke mzuri sana kwa sura na umbo atakutesa nafsi yako."
Hayo maneno aliniambia miaka 7 iliyopita hapa katikati nilifanikiwa kuwa na wasichana wazuri sana kwa sura na maumbo katika mahusiano lakini wote niliachana nao kutokana na kutokuwa waminifu, sasa nashukuru mungu nimepata msichana wa kawaida ananipenda sana na hivi sasa tupo kwenye utaratibu wa kufunga ndoa, sio siri huyu dada ananipenda sana na ananiheshimu sijawahi kupendwa hivi tangu nizaliwe. Maneno ya shangazi yametimia"mwanangu oa mwanamke mwenye uzuri wa moyo na matendo upate kufurahia maisha ya ndoa".
Nadhani mtakuwa mmejifunza