Wakati wa Bunge la bajeti wabunge wa CHADEMA isipokuwa Shibuda waligoma kuchukua posho za vikao, katika maswali ya papo kwa papo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipoulizwa kuhusu suala la posho kusitishwa alisema ni la kisheria na wapo wabunge wa CHADEMA wanaozitolea macho na wanataka ziongezwe, CHADEMA wakabwata kweli, lakini jana yametimia kwa Mbunge wa Rombo, Selasini kutamka waziwazi bungeni kwamba posho haitoshi.