Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari kwa wananchi na wanaotumia usafiri wa majini kufuatia kuwapo kwa upepo mkali

Kampuni ya Azam Marine na Kilimanjaro Fast Ferries kwa kupitia Mamlaka ya Usafiri Baharini (ZMA) pamoja na taarifa kutoka Mamlaka Ya Udhibiti wa Hali ya Hewa (Zanzibar) inapenda kuwatangazia abiria wake wote wanaosafiri baina ya Dar es Salaam na Zanzibar kwa kutumia vyombo vya kilimanjaro kwamba usafiri huo umesitishwa kwa leo tarehe 23/10/2018 kutokana na hali ya hewa mpaka itakaporuhusiwa na mamlaka husika pamoja na hali baharini kutulia. Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana nasi ama tembelea office zetu.

======

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari kwa wananchi na wanaotumia usafiri wa majini kufuatia kuwapo kwa upepo mkali.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne Oktoba 23, 2018, Samwel Nguya kutoka kituo kikuu cha utabiri cha TMA amesema watu wawe makini na mamlaka zinazoshughulika na usafiri wa majini ziwe makini kwa kuchukua tahadhari kuhakikisha hakuna maafa yanayoweza kutokea.

Amesema upepo huo unatokana na kuimarika kwa hali ya hewa kwenye eneo la Kusini Mashariki mwa Bara la Afrika na mfumo wa upepo wa Kusini.

Nguya amesema upepo huo mkali utavuma kwa siku tatu kwenye Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi na maziwa yote makuu ikiwamo Nyasa, Viktoria na Tanganyika na mikoa yote iliyopakana na maeneo hayo, ikiwamo na mikoa ya kanda ya kati.

“Tunaendelea kufuatilia mwenendo wa upepo huo na kutoa tahadhari kila inapolazimika kufanya hivyo, wanaotumia vyombo vya maji wachukue hatua ikiwamo mamlaka zinazohusika na usafiri wa majini,” amesema Nguya.
haya. ndio tunayotaka kuyaona sio kukurupuka tu
 
Angalizo usiegeshe gari katika miti iliyo na umri mkubwa hasa kama ile maeneo ya IFM utalia inavunjika vunjika na kuangukia kausafiri kako bure!
 
Kampuni ya Azam Marine na Kilimanjaro Fast Ferries kwa kupitia Mamlaka ya Usafiri Baharini (ZMA) pamoja na taarifa kutoka Mamlaka Ya Udhibiti wa Hali ya Hewa (Zanzibar) inapenda kuwatangazia abiria wake wote wanaosafiri baina ya Dar es Salaam na Zanzibar kwa kutumia vyombo vya kilimanjaro kwamba usafiri huo umesitishwa kwa leo tarehe 23/10/2018 kutokana na hali ya hewa mpaka itakaporuhusiwa na mamlaka husika pamoja na hali baharini kutulia. Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana nasi ama tembelea office zetu.

======

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari kwa wananchi na wanaotumia usafiri wa majini kufuatia kuwapo kwa upepo mkali.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne Oktoba 23, 2018, Samwel Nguya kutoka kituo kikuu cha utabiri cha TMA amesema watu wawe makini na mamlaka zinazoshughulika na usafiri wa majini ziwe makini kwa kuchukua tahadhari kuhakikisha hakuna maafa yanayoweza kutokea.

Amesema upepo huo unatokana na kuimarika kwa hali ya hewa kwenye eneo la Kusini Mashariki mwa Bara la Afrika na mfumo wa upepo wa Kusini.

Nguya amesema upepo huo mkali utavuma kwa siku tatu kwenye Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi na maziwa yote makuu ikiwamo Nyasa, Viktoria na Tanganyika na mikoa yote iliyopakana na maeneo hayo, ikiwamo na mikoa ya kanda ya kati.

“Tunaendelea kufuatilia mwenendo wa upepo huo na kutoa tahadhari kila inapolazimika kufanya hivyo, wanaotumia vyombo vya maji wachukue hatua ikiwamo mamlaka zinazohusika na usafiri wa majini,” amesema Nguya.
Unaitwa weledi
 
Bora walivyositisha jana wakati nakuja dar hali ilikua mbaya sana,abiria wote waliokaa ghorofa ya juu waliroa ilibidi nikae tayar tayar.
 
October 23, 2018
Hali ya hewa matarajio masaa 48 yajayo
Pwani yote Tanzania ya bahari Hindi & Maziwa Makuu ya Victoria Tanganyika


Source : millard ayo
 
Upepo wa Kusi huo na mara nyingi unazamisha samaki kwahiyo si rahisi kuvuliwa na wavuvi na hivyo wiki hii bei ya samaki itapanda mara dufu.
Jana nimenunua samaki bei hadi nikalaani uroho wangu wa samaki. Wakaniambia wanauza bei ya juu sababu bahari imechafuka samaki wamepatikana kidogo
 
Aisee wengine tulitaka kuja Dar kwa ferry, ila ule upepo wa jana si mchezo...
Ni kheri safari zilihairishwa jana, chopa nauli ndefu daah
 
ukae karibu na maboya na vifaa vya uokoaji.na ujiandae kwa lolote.

Wote tukikaa karibu na maboya kuna sehemu zitabaki tupu na chombo hakita balance, hatari zaidi.

Huku kwetu Afrika raia wanaambiwa wachukue tahadhari. Nchi za wenzetu hata kuwaambia wenye vyombo wachukue tahadhari hakuna.

Tayari makanuni na ma SOP yaliyo risachiwa yameandikwa tayari, kwamba, kukiwa na mvua milimita kadha bin kadha hakuna kuruka wala kutua ndege, kukiwa ma upepo knots kadhaa ngalawa lazima irudi pwani unless iko umbali wa maili kadhaa na kina cha futi kadhaa.

Watu wachukue tahadhari, tahadhali gani, waje wameshiba ili waokoane?
 
Kampuni ya Azam Marine na Kilimanjaro Fast Ferries kwa kupitia Mamlaka ya Usafiri Baharini (ZMA) pamoja na taarifa kutoka Mamlaka Ya Udhibiti wa Hali ya Hewa (Zanzibar) inapenda kuwatangazia abiria wake wote wanaosafiri baina ya Dar es Salaam na Zanzibar kwa kutumia vyombo vya kilimanjaro kwamba usafiri huo umesitishwa kwa leo tarehe 23/10/2018 kutokana na hali ya hewa mpaka itakaporuhusiwa na mamlaka husika pamoja na hali baharini kutulia. Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana nasi ama tembelea office zetu.

======

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari kwa wananchi na wanaotumia usafiri wa majini kufuatia kuwapo kwa upepo mkali.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne Oktoba 23, 2018, Samwel Nguya kutoka kituo kikuu cha utabiri cha TMA amesema watu wawe makini na mamlaka zinazoshughulika na usafiri wa majini ziwe makini kwa kuchukua tahadhari kuhakikisha hakuna maafa yanayoweza kutokea.

Amesema upepo huo unatokana na kuimarika kwa hali ya hewa kwenye eneo la Kusini Mashariki mwa Bara la Afrika na mfumo wa upepo wa Kusini.

Nguya amesema upepo huo mkali utavuma kwa siku tatu kwenye Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi na maziwa yote makuu ikiwamo Nyasa, Viktoria na Tanganyika na mikoa yote iliyopakana na maeneo hayo, ikiwamo na mikoa ya kanda ya kati.

“Tunaendelea kufuatilia mwenendo wa upepo huo na kutoa tahadhari kila inapolazimika kufanya hivyo, wanaotumia vyombo vya maji wachukue hatua ikiwamo mamlaka zinazohusika na usafiri wa majini,” amesema Nguya.
Tahadhari hii ilitakiwa itoke wiki iliyopita, watabiri nao wako nyuma yetu kwani sisi tulikwishajulishana tangu wiki iliyopita wao walikuwa wapi?
 
Back
Top Bottom