Mambo mawili yatakayoitokea CHADEMA baada ya 25 Oktoba

Mambo mawili yatakayoitokea CHADEMA baada ya 25 Oktoba

maramia

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2015
Posts
2,029
Reaction score
1,345
Mambo mawili makubwa ambayo bila ubishi wowote lazima yatakitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo, kiwe kimeshinda ama kimeshindwa katika uchaguzi mkuu wa 25 Oktoba 2015 kwa mujibu wa mtazamo na mwonekano wa mwenendo wa chama hicho ni kama ifuatavyo:

1. Kama Chadema itashinda ktk uchaguzi mkuu wa mwaka huu utakaofanyika 25 Oktoba, kutaibuka mgogoro mkubwa wa kiuongozi wa siasa za kimakundi utakaotokana na mgawanyo wa madaraka ndani ya serikali. Hali hiyo itatokana na wakubwa wa chama na serikali kuwa na makengeza na ubabe ktk kuteua viongozi wa kuongoza wizara, idara, taasisi na mashirika mbali mbali.

Kutakuwa na makundi mawili makubwa yatakayotaka kulazimisha watu wao wateuliwe, kundi la Lowassa na wahamiaji wake na kundi la Chadema asili. Makundi haya yatakivuruga sana chama hicho na Lowassa na kundi lake litataka kuwaacha makada wa Chadema nje halitakubali kutii amri ya yeyote na kama mkuu wa nchi Lowassa atakuwa na maamuzi yake na hii itapelekea atimliwe ktk chama na serikali ya Chadema itaishia hapo.

2. Jambo la pili ambalo ni la hatari kubwa kama litatokea ni pale Chadema itakaposhindwa kuchukua dola tarehe 25 Oktoba. Hali hii ikitokea, Chadema itakuwa historia masikioni mwa watanzania, hakutakuwa na Mbowe wala Lowassa katika siasa za nchi hii, huo utakuwa mwisho wao kisiasa na haitakuja itokee Chadema ishike dola ktk miaka ya karibuni labda kwa uchache iwe baada ya miaka 50 mbeleni.
Anayebisha asubiri na atenge miaka yake mitano mbele atayakubali maneno yangu.
Na wakati tukisubiri kuyaona haya tumwombee Dk Slaa awe na afya yake naye ayashuhudie.
 
Mambo mawili makubwa ambayo bila ubishi wowote lazima yatakitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo, kiwe kimeshinda ama kimeshindwa katika uchaguzi mkuu wa 25 Oktoba 2015 kwa mujibu wa mtazamo na mwonekano wa mwenendo wa chama hicho ni kama ifuatavyo:

1. Kama Chadema itashinda ktk uchaguzi mkuu wa mwaka huu utakaofanyika 25 Oktoba, kutaibuka mgogoro mkubwa wa kiuongozi wa siasa za kimakundi utakaotokana na mgawanyo wa madaraka ndani ya serikali. Hali hiyo itatokana na wakubwa wa chama na serikali kuwa na makengeza na ubabe ktk kuteua viongozi wa kuongoza wizara, idara, taasisi na mashirika mbali mbali.

Kutakuwa na makundi mawili makubwa yatakayotaka kulazimisha watu wao wateuliwe, kundi la Lowassa na wahamiaji wake na kundi la Chadema asili. Makundi haya yatakivuruga sana chama hicho na Lowassa na kundi lake litataka kuwaacha makada wa Chadema nje halitakubali kutii amri ya yeyote na kama mkuu wa nchi Lowassa atakuwa na maamuzi yake na hii itapelekea atimliwe ktk chama na serikali ya Chadema itaishia hapo.

2. Jambo la pili ambalo ni la hatari kubwa kama litatokea ni pale Chadema itakaposhindwa kuchukua dola tarehe 25 Oktoba. Hali hii ikitokea, Chadema itakuwa historia masikioni mwa watanzania, hakutakuwa na Mbowe wala Lowassa katika siasa za nchi hii, huo utakuwa mwisho wao kisiasa na haitakuja itokee Chadema ishike dola ktk miaka ya karibuni labda kwa uchache iwe baada ya miaka 50 mbeleni.
Anayebisha asubiri na atenge miaka yake mitano mbele atayakubali maneno yangu.

hata viti maalum si waligombana mpk basi
 
CDM bring back our doctor
 

Attachments

  • 1440804821681.jpg
    1440804821681.jpg
    58.8 KB · Views: 798
Baada ya tarehe 25 oktoba Zitto atakuwa na uwanja mpana kujenga upinzani. Harakati zitaanza upya kabisa. Tutazamie miaka 20 baadaye
 
hakuna marefu yasiyokuwa na ncha ipo sku utafka mwisho wao hao magamba
 
Migogoro ni sehemu ya maisha kwa kila kiumbe hai,yai hupasuka kwa ndani ili kuleta uhai upya,hata kuzaliwa kwako kulitokea kwa mgogoro mkubwa na mwisho hata kutembea kwako ni kwa sababu ya mgogoro baina ya mguu kwa mguu na miguu na ardhi.Kumbuka yai likipasuka kwa nje halina uhai na hayo yanaikumba CCM!!
 
Lini umeanza utabiri?ila huu utabiri wako umetabiri ukitokea chooni
 
Binadam nyinyi wa ajabu Sana. Watanzania wamechoka ongeleeni hali hiyo. si ishu ya cdm au ccm
 
Mkuu tumekuelewa lakini hiyo namba mbili hujaitolea ufafanuzi kwanini itokee hivyo.
 
mkuu mbona hujagusia washirika wengine wa ukawa
 
mbona mnatumia nguvu sana kutengeneza fitna mbona hujaandika mambo hayo upande wa pili muwe mnabalance story siyo mahaba yawaongoze.
 
Ni kweli kabisa, kwani kansa imeanza kwani tayari viongozi mashuhuri wa.... wamefungwa midomo, ndio maana Dr. Slaa ameona ni busara kukaa pembeni. Mwl. Nyerere aliwahi kusema hawezi kugeuka jiwe, na Dr. ni msomi mwerevu kugeka jiwe kwake yeye si muafaka.
 
Tuanze na CCM baada ya october 25 mambo makubwa yatakayotokea ni msururu wa viongozi na wanachama kuhamia chadema ili wapate angalao hifadhi kwa kisingizio kuwa walibaki ccm ili waweze kuendesha mapambano ya kuingoa wakiwa ndani.tukio jingine ni baadhi ya walioapa kuwa Lowasa akiingia ikulu watahama nchi kuorganise maandamano ya kumpongeza Lowasa kwa ushindi wa kishindo.kina lodi lofa na genge lake watamsifia na watakuwa wanapishana kwenye vyombo vya habari kuelezea uchapakazi na uthubutu wa kufanya maamuzi magumu wa Lowasa.ni mengi.mwishoni CCM itazikwa rasmi na masalia yake kuwekwa kwenye jumba la makumbusho la taifa
 
Back
Top Bottom