Mambo madogo 5 yatakayokupa amani

Mambo madogo 5 yatakayokupa amani

Peter Mwaihola

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2022
Posts
289
Reaction score
489
Usiwe mtu wa kuishi maisha na ndoto za wengine, vaa uhalisia wa maisha yako, vaa kiatu cha ndoto yako na uipambanie itakupunguzia msukumo wa mawazo ya kuwaza mambo yasiyokuhusu na yaliyo nje ya uwezo wako.

Ishi vizuri na kila mtu, wenye kukusema vibaya usipambane nao endelea kufanya mazuri ambayo yatawashawishi wakuone mtu bora zaidi ya jana. Usisahau kuwa Mungu hawezi kuruhusu jaribu ambalo hauwezi kulishinda.

Heshimu muda, panga mambo yako vizuri itakusaidia usichelewe kutekeleza malengo yako na kuepuka hofu ya kuwa nyuma ya wakati, hivyo kila jambo liwe na wakati wake.

Usiwe na matarajio makubwa kuliko juhudi zako, jibidishe kisha umuombe Mungu ndipo mafanikio yatakuja hata hivyo baada ya hayo usikose subira na uvumilivu.

Kila siku tambua kuwa baada ya Mungu na wazazi wako mtetezi na mpigania haki yako anayefuata ni wewe mwenyewe, hivyo jipe kipaumbele katika kujipambania wengine wafuate baadae kukupa msaada.

"Huenda wewe sio mkubwa kwa macho lakini ukubwa wako upo kwenye ndoto yako ukisimama imara utang'ara mbeleni"

[emoji2398] Peter Mwaihola
 
Usiwe mtu wa kuishi maisha na ndoto za wengine, vaa uhalisia wa maisha yako, vaa kiatu cha ndoto yako na uipambanie itakupunguzia msukumo wa mawazo ya kuwaza mambo yasiyokuhusu na yaliyo nje ya uwezo wako.

Ishi vizuri na kila mtu, wenye kukusema vibaya usipambane nao endelea kufanya mazuri ambayo yatawashawishi wakuone mtu bora zaidi ya jana. Usisahau kuwa Mungu hawezi kuruhusu jaribu ambalo hauwezi kulishinda.

Heshimu muda, panga mambo yako vizuri itakusaidia usichelewe kutekeleza malengo yako na kuepuka hofu ya kuwa nyuma ya wakati, hivyo kila jambo liwe na wakati wake.

Usiwe na matarajio makubwa kuliko juhudi zako, jibidishe kisha umuombe Mungu ndipo mafanikio yatakuja hata hivyo baada ya hayo usikose subira na uvumilivu.

Kila siku tambua kuwa baada ya Mungu na wazazi wako mtetezi na mpigania haki yako anayefuata ni wewe mwenyewe, hivyo jipe kipaumbele katika kujipambania wengine wafuate baadae kukupa msaada.

"Huenda wewe sio mkubwa kwa macho lakini ukubwa wako upo kwenye ndoto yako ukisimama imara utang'ara mbeleni"

[emoji2398] Peter Mwaihola
Sawa kikolo,huo ndio ukweli katika maisha!
 
Usiwe mtu wa kuishi maisha na ndoto za wengine, vaa uhalisia wa maisha yako, vaa kiatu cha ndoto yako na uipambanie itakupunguzia msukumo wa mawazo ya kuwaza mambo yasiyokuhusu na yaliyo nje ya uwezo wako.

Ishi vizuri na kila mtu, wenye kukusema vibaya usipambane nao endelea kufanya mazuri ambayo yatawashawishi wakuone mtu bora zaidi ya jana. Usisahau kuwa Mungu hawezi kuruhusu jaribu ambalo hauwezi kulishinda.

Heshimu muda, panga mambo yako vizuri itakusaidia usichelewe kutekeleza malengo yako na kuepuka hofu ya kuwa nyuma ya wakati, hivyo kila jambo liwe na wakati wake.

Usiwe na matarajio makubwa kuliko juhudi zako, jibidishe kisha umuombe Mungu ndipo mafanikio yatakuja hata hivyo baada ya hayo usikose subira na uvumilivu.

Kila siku tambua kuwa baada ya Mungu na wazazi wako mtetezi na mpigania haki yako anayefuata ni wewe mwenyewe, hivyo jipe kipaumbele katika kujipambania wengine wafuate baadae kukupa msaada.

"Huenda wewe sio mkubwa kwa macho lakini ukubwa wako upo kwenye ndoto yako ukisimama imara utang'ara mbeleni"

[emoji2398] Peter Mwaihola
kuna mwaka niliwahi kutafuta amani ya moyo kwa njia nyingi sana, pesa nilizipata ila sikuipata ile amani, awali nilifikiri nimeipata kume sikuwa najua nini maana ya amani, wanawake nilikuwa nao wengi kutafuta furaha na amani nakadhalika. ila kuna siku, nilitafuta uso wa Mungu, kwa kusoma Neno la Mungu na kusikiliza mahubiri ya mtumishi mmoja hivi, Dlerick Prince kwa wale wanaomjua, alikuja kutaja "Damu ya Yesu" na sikujua ile nguvu ilitoka wapi, iliupasua moyo wangu, nikahisi utulivu ambao sijawahi kuuona, nikahisi furaha ambayo sijawahi kuiona, nikahisi amani ambayo sijawahi kuiona, utulivuuuu?

Hiyo pia ilikuja kunipata nilipojazwa Roho Mtakatifu, that moment, hapo ndipo nikajua kuwa kuna amani ambayo ulimwengu huu unaitoa, hiyo ni maua asubuhi yanatokeza mchana yamenyauka na haiokoi. ila kuna amani toka kwa Mungu, hiyo yapita akili zote, haijalishi hajala, hauna pesa, unapita kwenye shida gani, ukiwa na amani hiyo, wala hautajali. utulivu wa ndaniii, amani ya ndani ambayo haielezeki (beyond description). nikaja kusoma mistari hii hapa nikagundua Biblia imeshasema Yesu Kristo ndiye Mfalme wa Amani, amani atupatiayo yeye akiwa mioyoni mwetu yapita akili zote, matatizo yote na kila tamaa ya dunia.

Isaya 9:6 Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.

Yohana 14:27 Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.

kuna wakati unaweza kuwa na kila kitu, pesa, kazi, kila kitu cha dunia hii, lakini kichwa chako kikawa kimejaa huzuni na mahangaiko, huna amani hata kufurahia hivyo vitu, nakushauri mkimbilie Yesu, yeye ni Mfalme wa amani. jaribu tu kama ukienda kwa Yesu kwa moyo wako wote na usione badiliko, basi huyo atakuwa sio Mungu ninayemuabudu, yeye ni mwaminifu, akiahidi huwa anatenda na hasemi uongo. amesema amani niwapayo mimi sio kama ile uwapao ulimwengu, ni unique. na yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe, haijalishi umeua, umezini, umefanya dhambi gani, uwepo wako hai leo ni opportunity Mungu amekupa ubadilishe maisha na utengneeze maisha naye, kabla haujafa kwasababu haujui ni lini utaondoka. ungalipo hai, mrudie Mungu kwa njia ya kuokoka.
 
Back
Top Bottom