Mambo 7 ya Msingi Kufanya ukiwa Single

Mambo 7 ya Msingi Kufanya ukiwa Single

mitale na midimu

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2015
Posts
10,419
Reaction score
17,758
Hakuna mtu ambae atakuja kuishi maisha yako kama usipoyajali sasa.Umri kabla haujaoa ni umrifursa...

1:Kwa wale waamini Mungu, ni kipindi cha kujifunza kwa kina na Mambo ya Mungu ili kukuandaa kwa ajili ya changamoto maishani hapo baadae. Maandiko yanasema "Lakini wale wamjuao Mungu watakuwa hodari na watafanya mambo makuu"

2:Ni kipindi cha kuchagua role model/Mentor wako katika mambo unayoyapenda.
watu wengi maisha Yetu yamekuwa yakurukaruka bila mwelekeo wa maana kama popcon jikoni kwa sababu hatujui tunakwenda na tunatoka wapi.

3:Ni wakati wa kuweka mawazo na ideas zako katika vitendo. jaribu vitu vingi kadili uwezavyo, endeleza vipaji vyako huu ndio muda muafaka sio muda wa kutangatanga bila muelekeo au kuburuzwa na makundi rika.

4:Ni kipindi cha kujenga tabia na mwelekeo wa maisha.Ni muda wa kuchagua LIFESTYLE yako.

5:Ni kipindi cha kujifunza jinsi ya kufanya maamuzi sahihi. Maamuzi yako ndio maisha yako.

6:Ni kipindi cha kuanza kujifunza kuwajibika na kupambana na changamoto.Kumbuka kile ambacho hutaweza kukitakua ukiwa kama SINGLE utakutana nacho pia kwenye ndoa wakati mwingine.

7:Ni kipindi cha kuijifunza jinsi na jinsia tofauti na wewe. una maarifa kiasi gani kuhusu jinsi na jinsia tofauti itakusaidia kupunguza migogoro isiyo ya lazima ktk maisha.

na,
MITALE NA MIDIMU
PROJECT 7777777
 
maisha hayajawahi kuwa sawa hata wakati mmoja, unaweza kujifunza hayo yote na ukaishia kufeli.
mimi kabla ya kuoa nilitamani sana maisha ya ndoa, baada kuoa changamoto ninazokutanazo natamani maisha yale kabla ya kuoa.
nikikutana na mtu akiniomba ushauri kama nashauri asiikimbilie ndoa.
 
Hivi mtu akiwa single katika umri wa 40 bado afuate hii kanuni au kwa vijana tu wa umri wa miaka 35 - 16
huo ni ushauri kwa wasiokatika ndoa hata hao masinia bachala(tafsiri sisisi) nao wanayo ya kuokota ingawa wanaweza kuwa wamefuzu baadhi ya vitu.
 
maisha hayajawahi kuwa sawa hata wakati mmoja, unaweza kujifunza hayo yote na ukaishia kufeli.
mimi kabla ya kuoa nilitamani sana maisha ya ndoa, baada kuoa changamoto ninazokutanazo natamani maisha yale kabla ya kuoa.
nikikutana na mtu akiniomba ushauri kama nashauri asiikimbilie ndoa.
kuna sababu nyingi mkuu kwa nini watu wapitie matatizo ktk ndoa.
lkn sababu hizo hazibatikishi ushauri hapo juu.
 
Hakuna mtu ambae atakuja kuishi maisha yako kama usipoyajali sasa.Umri kabla haujaoa ni umrifursa...

1:Kwa wale waamini Mungu, ni kipindi cha kujifunza kwa kina na Mambo ya Mungu ili kukuandaa kwa ajili ya changamoto maishani hapo baadae. Maandiko yanasema "Lakini wale wamjuao Mungu watakuwa hodari na watafanya mambo makuu"

2:Ni kipindi cha kuchagua role model/Mentor wako katika mambo unayoyapenda.
watu wengi maisha Yetu yamekuwa yakurukaruka bila mwelekeo wa maana kama popcon jikoni kwa sababu hatujui tunakwenda na tunatoka wapi.

3:Ni wakati wa kuweka mawazo na ideas zako katika vitendo. jaribu vitu vingi kadili uwezavyo, endeleza vipaji vyako huu ndio muda muafaka sio muda wa kutangatanga bila muelekeo au kuburuzwa na makundi rika.

4:Ni kipindi cha kujenga tabia na mwelekeo wa maisha.Ni muda wa kuchagua LIFESTYLE yako.

5:Ni kipindi cha kujifunza jinsi ya kufanya maamuzi sahihi. Maamuzi yako ndio maisha yako.

6:Ni kipindi cha kuanza kujifunza kuwajibika na kupambana na changamoto.Kumbuka kile ambacho hutaweza kukitakua ukiwa kama SINGLE utakutana nacho pia kwenye ndoa wakati mwingine.

7:Ni kipindi cha kuijifunza jinsi na jinsia tofauti na wewe. una maarifa kiasi gani kuhusu jinsi na jinsia tofauti itakusaidia kupunguza migogoro isiyo ya lazima ktk maisha.

na,
MITALE NA MIDIMU
PROJECT 7777777
Namba 7 kwenye JINSI na JINSIA watu wengi ndipo hukosea. Wengi hukimbilia kuoa/kuolewa kisa jamii inayomzunguka inataka hivyo (JINSIA)...... Bila kuangalia masuala ya kibaiolojia kwa mwili wake au mwenza wake (JINSI).
 
Yaani mkuu ingekuwa vyuma havijakaza ningekurushia jero la juisi ya miwa ila kwa kuwa irons are kazed ntakupa like tu. Umeongea cha ptimary (msingi) sana.
 
Back
Top Bottom