Mambo 5 ya kustaajabisha kuhusu Nanjilinji

Mambo 5 ya kustaajabisha kuhusu Nanjilinji

Ruangwa nako kuna nanjilinji kama kilwa???
 
kukaa na hela sawa kwa sababu hawana benki ila si kiasi kikubwa kama ulivyosema
 
Nanjilinji ni kijiji kilichopo wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi yafuatayo ni maajabu 5 ya kijiji hiki; 1. Nanjilinji ni kijiji cha msimu hutokea wakati wa mavuno tu 2.Nanjilinji wakazi wake ni wafanyabiashara tu 3. Wafanyabiashara hupeleka mpaka unga wa sembe tani 70 kwa mwaka na yote huisha kijijini hapo 4. Watu wa kijiji hiko huweka mpaka milioni 100 ndani ya nyumba bila kupeleka benki 5. Ni kijiji kinachotajwa mara nyingi zaidi na watu, kinatajwa zaidi ya mara laki tano kwa siku katika mazungumzo ya kawaida.

Nanjilinji ipo Kilwa, sema kijiografia ipo karibu sana na wilaya ya Ruangwa kihuduma za jamii kuliko Kilwa. Mfano Hospitali, Kituo cha Polisi, Soko kubwa, vyote wanahudumiwa Ruangwa, kwani kutoka Ruangwa hadi Nanjilinji ni km 60 lakini kutoka Kilwa Masoko hadi Nanjilinji kupitia Nakiu ni zaidi ya km 200 hivyo hupelekea watu kudhani ile ni wilaya ya Ruangwa lakini si kweli. Mengine yote ni kweli na upande wa hela ni zaidi ya m 100 wanahifadhi kila mfanyabiashara.
 
Unataka niambia kpnd ambacho c cha mavuno hakuna anaeish huko?? Hata mmoja?
 
Ina maana wale jamaa wa 'nguvu za masikini ni mtaji wake mwenyewe' pande hizo wanaogopa kutia timu.

Kwani hakuna mabenki huko?
 
Aisee ntafunga safari nikapaone Nanjiliji!
Mmetaja Ruangwa, mmenikumbusha rafiki yangu mmmmh mtoto yule wa Kimwera!!! hapana chezea kabisa!
 
Nanjilinji ni kijiji kilichopo wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi yafuatayo ni maajabu 5 ya kijiji hiki; 1. Nanjilinji ni kijiji cha msimu hutokea wakati wa mavuno tu 2.Nanjilinji wakazi wake ni wafanyabiashara tu 3. Wafanyabiashara hupeleka mpaka unga wa sembe tani 70 kwa mwaka na yote huisha kijijini hapo 4. Watu wa kijiji hiko huweka mpaka milioni 100 ndani ya nyumba bila kupeleka benki 5. Ni kijiji kinachotajwa mara nyingi zaidi na watu, kinatajwa zaidi ya mara laki tano kwa siku katika mazungumzo ya kawaida.
Nanjilinji iko wilaya ya Kilwa, mkoa wa Lindi na siyo Ruangwa. Pia ni kijiji cha kudumu na siyo cha msimu, hakiki taarifa kabla ya kuzitoa.
 
Ukiona mtu mzima anajitoa ufahamu na kulazimisha Nanjilinji ipo Ruangwa na siyo Kilwa pamoja na wadau kama nyie kutoa ufafanuzi mujarabu ujue kuna kitu
kinatafutwa hapo Mkuu IROKOS.
 
Shwadaktaaa, hivi huyu mzee bado ni mwenyekiti wa halmashauri ya Kilwa?

Mkuuu mapinduzi makubwa yaliyo fanyika Lindi na Mtwara haya kumwacha salama mwenyekiti wa wenyeviti wa ccm mikoa yote Tanzania kapoteza udiwani sasa cuf wana ongoza nanjilinji
 
Ruangwa si ndo anakotokea mhe. Majaaliwa k. Majaaliwa?
 
Nanjilinji ni kijiji kilichopo wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi yafuatayo ni maajabu 5 ya kijiji hiki; 1. Nanjilinji ni kijiji cha msimu hutokea wakati wa mavuno tu 2.Nanjilinji wakazi wake ni wafanyabiashara tu 3. Wafanyabiashara hupeleka mpaka unga wa sembe tani 70 kwa mwaka na yote huisha kijijini hapo 4. Watu wa kijiji hiko huweka mpaka milioni 100 ndani ya nyumba bila kupeleka benki 5. Ni kijiji kinachotajwa mara nyingi zaidi na watu, kinatajwa zaidi ya mara laki tano kwa siku katika mazungumzo ya kawaida.

Mdau kwanza nikurekebishe,Nanjilinji ni kijiji kilichopo wilaya ya Kilwa na si ya Ruangwa,isipokuwa kinapakana na Wilaya ya Ruangwa.Me nililima ufuta kule, kwa kweli kuna mambo yalinistaajabisha sana hasa hili la watu kutembea na maburungutu ya hela bila woga.Pia kuna gesti mbili tu na zote wakat wa msimu hujaa,nilikua nalala kwa mwenyej ambae alinistiri tu.Na si kweli kwamba wakaz wake ni wafanya biashara tu,wapo ambao hawafanyi biashara ya aina yeyote wao huishia kulima au kuwa vibarua kwenye mashamba.Sijafanya utafiti juu ya kutajwa sana,ila nadhan wakat wa msimu ndio hutajwa sana,jambo lingine uwapo nanjilinji itakupata uamke saa 9 kuwah usafiri wa basi la kukupeleka Dar es Salaam.
Cc Kipilipili
 
Last edited by a moderator:
Milion 100 hapana mkuu

Hili la milioni 100 ni la kweli mdau wala halina shaka,wakat wa msimu wa ununuz wa ufuta matajiri hutuma mawakala ambao ni wakaz wa ukanda huo kununua ufuta au mbaazi,sio ajabu kumkuta kijana ana mil 100 au zaid kwa ajili ya kukusanya mzigo,na haijawah tokea uhalifu,maana hakuna bank na wala hakuna kituo cha polisi,na mtandao unaopatikana kule ni Voda tu
 
Back
Top Bottom