mmmuhumba
JF-Expert Member
- Nov 8, 2017
- 491
- 476
1. Kumpa uhuru wa kuhoji na kukushauri katika maisha yako.
Asiwe kama mlinzi wa getini, kila kitu ni honi na muda wa kujua sasa ni saa 6 natakiwa kwenda kula na chochote akutacho kuta hana haki ya kuhoji ni kula ama aache. Mpenzi mwenye kupewa uhuru wa kuhoji na kushauri huwa na imani ya leo na kesho nawe.
2. Kumshirikisha katika mfumo wako wa utafutaji.
Wanaume wengi hawapendi wanawake zao wajue wanachopata, kwa mtu mwenye malengo naye ni jambo jema akijua unakazi gani, biashara gani, au unakitu gani cha kukuingizia. Nafasi hii uonyesha uko naye kwa malengo ya familia endelevu.
3. Kujali watu wake wa karibu iwe marafiki, ndugu na familia.
Unapomwambia unampenda na unachukia familia yake, huu ni uongo na hata ikiwa ni kijitabia, basi ujue una choyo acha. Kuwapenda watu wa karibu ni kumaanisha, upo tayari kumtetea na kumlinda na maisha yake.
4. Kumtambua hulka zake.
Itakufanya usimshangae mabaya na mazuri yake, usipomtambua huwezi ishi kwa mipaka naye na hata inapotokea amekukosea ni ngumu kujua namna ya kuthibiti hasira yako. Ni rahisi kufanya muauzi na baadae kujilaumu.
5. Kumjali kihisia na kimazingira.
Choyo, ubinafsi, kujitia uoni, huna hamu na kitu au jambo fulani. Pindi unapokuwa na mwenza upaswi kuishi nayo hayo. Ni lazima uishi katika wingi wa sisi, kujali hisia za mwenzio na mahitaji yake ya kimazingira.
6. Kumsamehe na kuyapuuza mengine yasio tija.
Unaishi na binadamu siyo malaika, tegemea pande zote za shilingi, kununa nuna, kukumbushia makosa, kuyatazama yaliyopita na kuwa na moyo mgumu wa kusamehe huku utaki aende, ni kuishi katika penzi lisiloweza kukua.
7. Kuacha kumchunguza
Kumchunga mtu mzima ni kama kuchezea nyeti zako, kama anaamua kutulia atatulia ila akiamua kuuwasha moto basi atauwasha, la msingi mueleze wazi usichopenda na mkemee pale unapoona anakuwa kinyume nawe. Mwenye akili na utayari ataelewa unachomaanisha, mtu mzima kuchungwa ni ishu.
8. Kujiongeza na kuwa romantiki.
Acha kupenda kila kitu kuombwa ombwa, kila jambo ukumbushwe kumbushwe, kila jambo mpaka uwe na shida wewe ndiyo uone tija. Msome uliyenaye na mtambue.
9. Kumheshimisha Kwa marafiki, ndugu na familia yako.
Mbaya kuambiwa unapendwa alafu hata akiondoka hujui utampatia wapi wala hujui utamuuliza nani juu yake. Unaposhindwa kutatua jambo naye hujui pia mtu wa kwenda kumshtakia na mwenye kuweza kumuita. Ni tatizo
10. Kuzitambua ndoto zake.
Maendeleo ni ya wote, kushikana mikono ni tija na jambo kubwa la kujenga mapenzi bora. Hivyo, una malengo basi zingatia hayo, mmngine matokeo muachie Mungu.
Asiwe kama mlinzi wa getini, kila kitu ni honi na muda wa kujua sasa ni saa 6 natakiwa kwenda kula na chochote akutacho kuta hana haki ya kuhoji ni kula ama aache. Mpenzi mwenye kupewa uhuru wa kuhoji na kushauri huwa na imani ya leo na kesho nawe.
2. Kumshirikisha katika mfumo wako wa utafutaji.
Wanaume wengi hawapendi wanawake zao wajue wanachopata, kwa mtu mwenye malengo naye ni jambo jema akijua unakazi gani, biashara gani, au unakitu gani cha kukuingizia. Nafasi hii uonyesha uko naye kwa malengo ya familia endelevu.
3. Kujali watu wake wa karibu iwe marafiki, ndugu na familia.
Unapomwambia unampenda na unachukia familia yake, huu ni uongo na hata ikiwa ni kijitabia, basi ujue una choyo acha. Kuwapenda watu wa karibu ni kumaanisha, upo tayari kumtetea na kumlinda na maisha yake.
4. Kumtambua hulka zake.
Itakufanya usimshangae mabaya na mazuri yake, usipomtambua huwezi ishi kwa mipaka naye na hata inapotokea amekukosea ni ngumu kujua namna ya kuthibiti hasira yako. Ni rahisi kufanya muauzi na baadae kujilaumu.
5. Kumjali kihisia na kimazingira.
Choyo, ubinafsi, kujitia uoni, huna hamu na kitu au jambo fulani. Pindi unapokuwa na mwenza upaswi kuishi nayo hayo. Ni lazima uishi katika wingi wa sisi, kujali hisia za mwenzio na mahitaji yake ya kimazingira.
6. Kumsamehe na kuyapuuza mengine yasio tija.
Unaishi na binadamu siyo malaika, tegemea pande zote za shilingi, kununa nuna, kukumbushia makosa, kuyatazama yaliyopita na kuwa na moyo mgumu wa kusamehe huku utaki aende, ni kuishi katika penzi lisiloweza kukua.
7. Kuacha kumchunguza
Kumchunga mtu mzima ni kama kuchezea nyeti zako, kama anaamua kutulia atatulia ila akiamua kuuwasha moto basi atauwasha, la msingi mueleze wazi usichopenda na mkemee pale unapoona anakuwa kinyume nawe. Mwenye akili na utayari ataelewa unachomaanisha, mtu mzima kuchungwa ni ishu.
8. Kujiongeza na kuwa romantiki.
Acha kupenda kila kitu kuombwa ombwa, kila jambo ukumbushwe kumbushwe, kila jambo mpaka uwe na shida wewe ndiyo uone tija. Msome uliyenaye na mtambue.
9. Kumheshimisha Kwa marafiki, ndugu na familia yako.
Mbaya kuambiwa unapendwa alafu hata akiondoka hujui utampatia wapi wala hujui utamuuliza nani juu yake. Unaposhindwa kutatua jambo naye hujui pia mtu wa kwenda kumshtakia na mwenye kuweza kumuita. Ni tatizo
10. Kuzitambua ndoto zake.
Maendeleo ni ya wote, kushikana mikono ni tija na jambo kubwa la kujenga mapenzi bora. Hivyo, una malengo basi zingatia hayo, mmngine matokeo muachie Mungu.