Mama wa Taifa Hili ni Nani?

Mama wa Taifa Hili ni Nani?

Nasikia kuna issue ya mababa wa mataifa, lakini sijawahi kusikia ma-Mama wa mataifa, Mbona hakuna Gender Balance. Mama wa taifa hili ni nani?:spy:

Samahani kama nimewaudhi, akina mama
Kama alivyosema Aristotle,hapa Tanzania mtu akiuliza 'Mama wa Taifa ni nani,huyu mtu hataki kuelimishwa,huyu mtu anataka kuanzisha ugomvi''
 
Kama alivyosema Aristotle,hapa Tanzania mtu akiuliza 'Mama wa Taifa ni nani,huyu mtu hataki kuelimishwa,huyu mtu anataka kuanzisha ugomvi''
Hawa watu mi sijui wako vipi. Maana nawaeleze mambo ya kufanya gender balance, wao wanaleta utani. Wamesahau Berlin Conference. Au kama walishindwa kutafsine neno Founder of the Nation kwa kiswahili waseme tu.
 
Huu uzi wa kichokozi sana kuna watu wataingia lupango muda si mrefu.
 
Nasikia kuna issue ya mababa wa mataifa, lakini sijawahi kusikia ma-Mama wa mataifa, Mbona hakuna Gender Balance. Mama wa taifa hili ni nani?:spy:

Samahani kama nimewaudhi, akina mama

huwezi kuwa BABA wa Taifa kama hujafanya jambo kubwa nchi yako kama wakina Mandela , Nyerere, Kwame na wengineo, sasa ni kina mama wangapi ambao walikubari kuwekwa ndani na kuteswa ili kupiganiaa uhuru wa Afrika mimi siwafaamu kama kuna mtu anawafahamu naomba anijuze.
 
Bibititi Mohamed
I think some of you guys are either nincompoops or are idle and loves to trivialize issues or have very poor sense of humour when it comes serious issues. If you cant contribute intelligently why not become a reader and learn from people like mwanakijiji???
 
Nasikia kuna issue ya mababa wa mataifa, lakini sijawahi kusikia ma-Mama wa mataifa, Mbona hakuna Gender Balance. Mama wa taifa hili ni nani?:spy:

Samahani kama nimewaudhi, akina mama
Ni kweli kabisa ni vigumu kusikia kina mama wa taifa. kutosikia kwetu haimaanishi kuwa hawapo.
Kwanza tuanze na maana ya mama au baba wa taifa maana yake nini? jee ni lazima awe mkuu wa nchi????
kutakuwa na majibu mengi tofauti lakini kwa mtazamo wangu ni kuwa baba/mama wa taifa ni mtu aliye inspire wananchi wenzake into nationalhood wakati wakiwa kwenye kipindi cha suppression bila kujali athari zinazotoka na activities hizo.

Bibi Titi ambaye alizaliwa 1926, alikuwa kiongozi shupavu katika kipindi cha kudai uhuru. Huyu mama [wa pwani] alivunja miko kwa kujitoa hadharani kama mhanga wa mapambano ya kudai uhuru tangu mwanzoni mwa miaka 1953. Aliwahamasha wanaume na wanawake katika kudai uhuru maeneo yote kuanzia pwani hadi bara [katika kipindi ambacho mwanamke alionekana kama binadamu daraja la pili] Mama huyu bila kujali ndoa yake maadili ya dini yake, mila na utamaduni wa jamii yake alijitosa kuliko viongozi wengi ukiondoa mwalimu. Yeye ndiye chimbuko la UWT na ule msemo wa WANAWAKE NA MAENDELEO. Kama mwalimu alikuwa anazungumzwa [mwanamume] basi bibi titi kwa kina mama alikuwa hivyo.
Bahati mbaya hakusoma sana nadhani aliishia darasa la nne hivi lakini, aliwatoa kamasi wasomi ndani ya TANU na nje ya TANU.
Huyu mama alikuwa mwanamapinduzi halisi na kama kuna mwanamama anayestahili kuitwa mama wa taifa basi ninaamini yeye anastahili kuitwa hivyo.
 
mama wa taifa ni uchumi uliokaa vizuri tena ulio endelevu kuweza kuwatunza na kuwalea wananchi wake na kuwakuza.
 
Back
Top Bottom