Maelfu ya wanawake Jimbo la VUNJO wamejitokeza kumpokea Mama Samia, miongoni mwa wanawake hao wengine wanatoka chadema. Aidha wamemtaka katika serikali yake ajitahidi kuhakikisha anaboresha miundo mbinu jimboni hapo swala ambalo limekuwa ni changamoto ya muda mrefu.
Kwani wanawake waliowanachama wa CHADEMA sio Watanzania, aidha, ulijuaje kuwa wanatoka CHADEMA na sio vyama vingine ? Mbona hapo sioni sare za CDM. Na kwa nini Wagombea wengine wanazuiliwa kutembelea hospitali ilihali yeye anaruhusiwa, Timu ya Kampeni ya CCM safari hii inachangia kupunguza kura za Dr. Magufuli. Kama imezuiliwa wagombea kwenda kwenye taasisi za uuma iwe kwa wote ili mwingine asione kama ananyanyaswa kitu ambacho kinaweza kusababisha apigiwe kura za huruma a.ka, Usamaria Mwema.
Picha za tarakea rombo acha uongo mleta mada muulize Shirima vizur akuambie vunjo ilivyo yeye ndio mgombea Wa ubunge kama vyunjo ccm ata diwani awapati wameshachoka na ccm
Sina picha za vunjo.
Lakini picha hizo akishazipost humu Mr. Chin nafikiri.
Pekua tu thread nzima ipo.
Ni jambo la msingi kutoa taarifa sahihi hapa jukwaani
Picha za tarakea rombo acha uongo mleta mada muulize Shirima vizur akuambie vunjo ilivyo yeye ndio mgombea Wa ubunge kama vyunjo ccm ata diwani awapati wameshachoka na ccm