Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

mgeni wenu

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2012
Posts
3,664
Reaction score
1,731
Wana JF kutokana na mtandao huu wa kijamii kuibua na kueneza siri za Serikali Wabunge wa CCM wameridhia Mtandao huo ufungwe kama ilivyokuwa Ze Utamu na Mtoa Hoja ni Mchungaji Getrude Lwakatale, Leo pia kapeleka swali lake Bungeni.

Waziri kaitetea JF na kuwashauri wabunge kuwa ni chombo cha habari cha kijamii.

UPDATE:

 

ndio maana wanaomba viti maalum vifutwe? 330,000/= kuuliza mmiliki wa JF OMG!!!!
 
Msekwa alijaribu, huenda wakafanikiwa
 
Mkuu karibu hapa JF, mimi naitwa only83..JF ni zaidi ya uijuavyo..hata mkuu wa kaya ni member hapa na uwa anafaidika na mawazo ya wanaJF.. wazo la kuwa JF ni ya CDM nadhani ni ule muendelezo wenu wa kutumia kufikiria kwa kutumia *Masaburi*

Kama vijana na wanachama wa magamba hawajui umuhimu wa kutumia mitandao kama sehemu ya kujijenga msisingizie JF kuwa ni ya CDM..Hakuna uhusiano wa JF na CDM isipokuwa member wengi wa JF wanaweza kuwa ni wanachama wa CDM, japo sina uhakika sana na hili.
 

Lwakatale ni tapeli, mwizi wa roho za watu wenye shida. Anawadanganya kuwa shida zao zitaisha. Ikitokea kuwa na forum za kumwambia ukweli anakuwa mbogo. Anawadanganya watu wasio na matumaini, kama waliokosa watoto/uzazi, mahanisi (wanaume, magonjwa yasiyotibika eti kwa kuwaombea watapona.

Uongo hakuna atakayezaa na umri wa miaka 60 mwanamke!!! anampa hope eti ana nguvu za kumwombea akazaa. Ukiwafumbua macho kwa uongo kama huo ndani ya JF tukufu, anapeleka bungeni ufungwe!1 Shame!!
 
JF Founder/team ilienda bungeni mwaka jana kama uzee haujafuta kumbukumbu zangu, huyo Mh Mchungaji Dr Mama Rwakatare siku hiyo hakuwepo bungeni?
 
Kama kuna siku magamba watakua wamekosea step ni kufunga JF maana kitakochokuja kitakuwa moto zaidi ya JF.

Kwa nini kitakachofuata kiwe moto zaidi? Ina maana JF ni kwa ajili gani au wengine hatujui? Mimi ninanvyojua JF upo kwa ajili ya ku-interchange views, kutoa mawazo yenye tija kwa maendeleo ya taifa na mambo mengine kama hayo. So naamini uamuzi wowote wenye kutaka kufunga JF utakuwa umefanyiwa tafiti za kutosha na kujiridhisha kuwa mtandao huu hauna tija kwa maslahi ya taifa.
 
Nahisi maamuzi ya kufunga jf hayatakuwa sahihi sana kwa sababu kwa kufanya hivyo kunapunguza fursa kwa wanajamii kutoa mawazo yao juu ya mambo mbalimbali yanayotokea ktk jamii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…