ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,758
- 9,589
Habarini wadau wote
Natumai mko wazima buheri wa afya na mnaendelea na kazi zenu vyema na wale wanaosoma vilevile
Marafiki zangu imenibidi niongee nanyi haya machache ambayo nimeona mahali fulani kweli yamenifanya nitokwe na machozi na vilevile imenipelekea niweze kuwafunda VIJANA wa kisasa ambao wao kwao
HESHIMA NA ADABU imewapita kando wao wanajiona fahari sana kuwatusi, kuwadharau na kuwabedha
WAZAZI wao hususaniMAMA.
Sijui vijana wameingiliwa na kitu gani yaani vijana sasa wamekuwa kama helkopta wanajiona fahari sana
na wanajiona wana akili nyingi sana kuzidi wazazi wao hasa MAMA, wameshikwa na dharau ya nje nje
hawakumbuki kuwa MAMA alibeba mimba zao miezi 9 akakufyatua duniani ukaiona nchi leo hiii unamwona
takataka asiye na akili asiye na maendeleo.
Hata kama ana gari basi kama si mjuzi wa kiufundi gari linapo haribika basi unaleta dharau hivi kwanini mmekuwa hivyo vijana wenzangu?
Nimeongea haya kwani nimeona sana siku hzi adabu haipo kwa wakubwa na ukitaka kuwakemea na kuwaonya
hayo maneno utakayomwagiwa utaomba ardhi ipasuke udumbukie humo ndani yaani bora tuwafunde hapa
hapa kwani mnakoelekea si kuzuri.
Acheni kuiga mambo ya ughaibuni eti daddy atanifanya nini nami ni kidume kama ayeye nani amekufundisha maadili mabovu kiasi hicho? mbona mimi na daddy yangu watu8 namheshimu sana pamoja na mumy measkron nawaheshimu na kuwapenda vijana badilikeni Mungu hapendezwi na mtu
ambaye yu kinyume na wazazi wake.
Heshima ni kitu chema na ndicho kinakupatia baraka toka kwa Mungu kuipitia hao wazazi wako kwani Mungu alikuwa na makusudi ya kukufyatua wewe uwepo duniani na ni miungu wako hapa duniani.
Kijana hususani VIJANA WA KIUME tambueni hilo na muwe na staha, heshima kwa MAMA zenu hata kama ana elimu kuliko wewe ni mama huyo, hata kama ana sura nzito ni MAMA huyo hatakama si lolote wala chochote kwako hutapata MAMA mwingine kama huyo mmpende, mmheshimu na mtii
ndipo utaona baraka za Mungu zikikukufuata bestito.
Hili ni somo lenu ambalo nimeona niwafunde hasa vijana wakiume mmezidi sana mnadharau BADILIKENI
Wasalaamu.
Ladyf
CCC: Mamndenyi, Passion Lady, charminglady, Kasinde, Lady doctor, mwallu, Christine Denzi, Nivea, The secretary, Munkari, lara1, miss neddy, @Kwantwe, Zinduna, measkron, Kongosho kingasti, Heaven on Earth, sister, Paloma, lady gaga, Madame B, madame A, na marafiki zangu
wote niliowasahau kuwataja hapa karibuni tuongee jambo hili kwani halipendezi kabisa kuwepo kwa watoto wetu
Natumai mko wazima buheri wa afya na mnaendelea na kazi zenu vyema na wale wanaosoma vilevile
Marafiki zangu imenibidi niongee nanyi haya machache ambayo nimeona mahali fulani kweli yamenifanya nitokwe na machozi na vilevile imenipelekea niweze kuwafunda VIJANA wa kisasa ambao wao kwao
HESHIMA NA ADABU imewapita kando wao wanajiona fahari sana kuwatusi, kuwadharau na kuwabedha
WAZAZI wao hususaniMAMA.
Sijui vijana wameingiliwa na kitu gani yaani vijana sasa wamekuwa kama helkopta wanajiona fahari sana
na wanajiona wana akili nyingi sana kuzidi wazazi wao hasa MAMA, wameshikwa na dharau ya nje nje
hawakumbuki kuwa MAMA alibeba mimba zao miezi 9 akakufyatua duniani ukaiona nchi leo hiii unamwona
takataka asiye na akili asiye na maendeleo.
Hata kama ana gari basi kama si mjuzi wa kiufundi gari linapo haribika basi unaleta dharau hivi kwanini mmekuwa hivyo vijana wenzangu?
Nimeongea haya kwani nimeona sana siku hzi adabu haipo kwa wakubwa na ukitaka kuwakemea na kuwaonya
hayo maneno utakayomwagiwa utaomba ardhi ipasuke udumbukie humo ndani yaani bora tuwafunde hapa
hapa kwani mnakoelekea si kuzuri.
Acheni kuiga mambo ya ughaibuni eti daddy atanifanya nini nami ni kidume kama ayeye nani amekufundisha maadili mabovu kiasi hicho? mbona mimi na daddy yangu watu8 namheshimu sana pamoja na mumy measkron nawaheshimu na kuwapenda vijana badilikeni Mungu hapendezwi na mtu
ambaye yu kinyume na wazazi wake.
Heshima ni kitu chema na ndicho kinakupatia baraka toka kwa Mungu kuipitia hao wazazi wako kwani Mungu alikuwa na makusudi ya kukufyatua wewe uwepo duniani na ni miungu wako hapa duniani.
Kijana hususani VIJANA WA KIUME tambueni hilo na muwe na staha, heshima kwa MAMA zenu hata kama ana elimu kuliko wewe ni mama huyo, hata kama ana sura nzito ni MAMA huyo hatakama si lolote wala chochote kwako hutapata MAMA mwingine kama huyo mmpende, mmheshimu na mtii
ndipo utaona baraka za Mungu zikikukufuata bestito.
Hili ni somo lenu ambalo nimeona niwafunde hasa vijana wakiume mmezidi sana mnadharau BADILIKENI
Wasalaamu.
Ladyf
CCC: Mamndenyi, Passion Lady, charminglady, Kasinde, Lady doctor, mwallu, Christine Denzi, Nivea, The secretary, Munkari, lara1, miss neddy, @Kwantwe, Zinduna, measkron, Kongosho kingasti, Heaven on Earth, sister, Paloma, lady gaga, Madame B, madame A, na marafiki zangu
wote niliowasahau kuwataja hapa karibuni tuongee jambo hili kwani halipendezi kabisa kuwepo kwa watoto wetu