george aloyce
JF-Expert Member
- Aug 22, 2017
- 1,221
- 1,883
Nimeolewa, ndoa yangu ina miaka 10 sasa, na sasahivi nina ujauzito wa miezi 8. Mimi na mume wangu tuko vizuri. Kwa sababu niliambiwa nisisafiri, mama mkwe wangu amekuja kunihudumia uzazi. Si mtu mzima sana, ana kama miaka 55.
Kuna kitu sikielewi, mpaka nahisi kuwa labda mimi ndiyo nina matatizo. Mama mkwe wangu tunaongea vizuri, lakini shida iko katika kuvaa. Yaani, yeye anaweza kuvaa nguo fupi mpaka akiinama, chupi inaonekana. Akikaa, bila kujali kama mimi nipo au la, mapaja yake yanaonekana nje.
Wakati mwingine, anaweza kuvaa nguo za ndani tu, akafunga khanga. Mume wangu yupo, sasa wakati wa kurekebisha khanga, akaifungua mpaka chupi inaonekana tena mbele ya mume wangu bila kujali.
Mimi ndiyo naona aibu, kaka, na sijui ni kwa namna gani namuambia mume wangu kuwa si kitu kizuri. Jana, alivaa nguo ya kulalia ambayo inaonyesha mpaka rangi ya chupi, na juu hakuvaa sidiria, hivyo matiti yake yanaonekana, na wala hajali kuwa mume wangu yupo.
Kuna siku nikiwa chumbani, natoka, namkuta kakaa na mume wangu, amepandisha miguu juu kwenye kochi, mapaja yake yote yanaonekana nje, chupi inachungulia. Kuniona, ndiyo ameshusha miguu tu, na kuniongelesha kama vile hakuna kitu kimetokea.
Kaka, nashindwa kuelewa. Hivi ni kwamba mimi ndiyo mshamba, labda huu ni uzungu, au kuna shida hapa? Mume wangu kwao wako wawili, ana dada yake ambaye naye anakuja mara kwa mara.
Ila cha ajabu, dada yake akija, mama mkwe wangu anavaa vizuri tu. Sijamuona akivaa hivi wakati wifi yangu akiwepo. Nishauri, kaka, ni mimi nina shida, au kuna tatizo hapa?
Kuna kitu sikielewi, mpaka nahisi kuwa labda mimi ndiyo nina matatizo. Mama mkwe wangu tunaongea vizuri, lakini shida iko katika kuvaa. Yaani, yeye anaweza kuvaa nguo fupi mpaka akiinama, chupi inaonekana. Akikaa, bila kujali kama mimi nipo au la, mapaja yake yanaonekana nje.
Wakati mwingine, anaweza kuvaa nguo za ndani tu, akafunga khanga. Mume wangu yupo, sasa wakati wa kurekebisha khanga, akaifungua mpaka chupi inaonekana tena mbele ya mume wangu bila kujali.
Mimi ndiyo naona aibu, kaka, na sijui ni kwa namna gani namuambia mume wangu kuwa si kitu kizuri. Jana, alivaa nguo ya kulalia ambayo inaonyesha mpaka rangi ya chupi, na juu hakuvaa sidiria, hivyo matiti yake yanaonekana, na wala hajali kuwa mume wangu yupo.
Kuna siku nikiwa chumbani, natoka, namkuta kakaa na mume wangu, amepandisha miguu juu kwenye kochi, mapaja yake yote yanaonekana nje, chupi inachungulia. Kuniona, ndiyo ameshusha miguu tu, na kuniongelesha kama vile hakuna kitu kimetokea.
Kaka, nashindwa kuelewa. Hivi ni kwamba mimi ndiyo mshamba, labda huu ni uzungu, au kuna shida hapa? Mume wangu kwao wako wawili, ana dada yake ambaye naye anakuja mara kwa mara.
Ila cha ajabu, dada yake akija, mama mkwe wangu anavaa vizuri tu. Sijamuona akivaa hivi wakati wifi yangu akiwepo. Nishauri, kaka, ni mimi nina shida, au kuna tatizo hapa?