Mama Kilango Malecela alitumbuliwa haraka sana, ila Makonda mmmmh

falcon mombasa

JF-Expert Member
Mar 5, 2015
9,159
9,241
Ni jambo la kushangaza ama kuvunja nguvu mno watanzania wanaposhuhudia baadhi ya viongozi wakitumbuliwa haraka sana kwa tuhuma za kutokuwa makini kazini tena bila hata kujitetea.

Ila inastajaabisha zaidi serikali hiyo hiyo ya rais huyo huyo wa chama hiko hiko anamuacha mkuu wa mkoa wa dar es salaam mwenye kashfa kubwa zaidi ya kukosa sifa za kielimu lakini bado yupo ofisini tena akiwa na majibu ya kishujaa kabisa dhidi ya tuhuma hizo.

Huu si wakati wa kuburuzwa ni muda sahihi serikali kueleza sababu za msingi za kuendelea kumbakisha huyu mwenye kashfa madarakani.

Ni jambo la fedheha mno kuona taasisi kubwa kama ikulu kujibu tuhuma ambazo si za kweli kwakuita vyombo vya habari na kukana taarifa fulani za uzushi kuwa si kweli, lakin inashangaza zaidi kuona huyu mwenye kashfa kubwa zaidi ya kudhalilisha serikali nchi na aliyemteua bado anadunda ofisini kama vile hakuna mwingine mwenye sifa kuwa mkuu wa mkoa Dar es salaam

Mitaani maneno yameanza kuibuka kuwa huenda yupo kwa ajili ya kumnufaisha aliyemteua, wengine wakihoji huenda sababu wote wametoka kanda moja. lakini kama suala ni kuchagua wa kanda moja mbona wako wengi wenye sifa.

Kwakweli ni wakati maalum kwa chama kujitathmin kama 2020 kinapaswa kuendelea kung'ang'ania nafasi hiyo ya urais

My take:

Tanzania ni ya watanzania wote sio ya mtu fulani au kabila fulani
 
Huyu ng'ombe sijui kwa nn ni mkuu wa mkoa coz karibuni ataliingizia taifa hasara kubwa......
-Alimpiga Warioba tumekaa kimya
-Kaja kumtukana dada wa watu hadharani kwenye mkutano Dar tunamuangalia tu
-Kawasema sirro na RPC wamechkua rushwa ya shisha tumekaa kimya
-Anawataja watz hadgarani kuwa wanauza madawa ya kulevya na kuwadharirisha tupo tu. Anataja hata viongozi wa dini bila hata ushahidi
-Anatumia vyombo vya dola vibaya
-Ameitwa na bunge amekataa tumekaa kimya
-Ameitwa mahakamani amekataa

KWELI ccm INAWENYEWE
anatembea na limsafara likubwa hilo utafurahi
 
Wanahubiri wasicho kitenda wao. Kwani huyo Kilango saivi yuko wapi....hata daudi akitumbuliwa nae atapatiwa nafasi nyingine tu........ ebu wewe leo kamatwa na vyeti feki uone
mi sina nafasi ya kuajiriwa. mimi ni mfanyabiashara napambana na kodi za bandarini zinavyopanda hovyo hovyo
 
Bado kidogo utashangaa tunatumbua Nape na Mwigulu kijana anapeta (rejea usanii wa Nyerere msanii)
 
Hata yeye binafsi hii kashfa kama ni ya kweli angebaki na heshima kiasi kama angejiuzulu mwenyewe bila kutolewa na mwenye nchi.
 
Ila jamani kuna watu wana roho ngumu! Hivi kweli anajijua ana tuhuma ya kutokuwa na cheti halafu amejikausha utafikiri hasikii! Yani kabisa yuko ofisini....macho ya watu yanavyomwangalia yeye yuko sawa tu!
 
akiondoka yeye nani atamsifia mkulu,mawaziri wengine wte hawatakai kumsifia hawezi kumuondoa ni upepo wa kisiasa utapita tu
 
Kwa Bashite mtasubiri sana. Mkulu hawezi mtumbua Bashite kisa uhalali Wa cheti Chake. Anahisi huo ni mwanzo Wa kuhoji uhalali wa PhD yake. Atamlinda kwa nguvu zote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom