Mama ameamua kunitesa kwenye mahusiano na Baba anaunga mkono

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,471
23,744
" Mimi ni kijana wa miaka 32 nimeajiriwa namshukuru Mungu kipato changu kipo vizuri sina matatizo toka miaka miwili iliyopita nilimpata dada mmoja ambaye niliridhia awe mke wangu mtarajiwa.alikuwa akisoma nikampa muda amalize chuo ili baada ya hapo tuanze michakato ya ndoa.

Nlimpeleka kwa wazazi wangu baba alikuwa nje ya nchi kwa muda mrefu hivyo mama ndiye aliyefanikiwa kupata muda wa kumwona na kuongea naye baadaye alipomaliza chuo nilienda kwa mama kumwambia sasa ni wakati muafaka nataka kujitambulisha kwao huyo msichana cha kustaajabisha mama alibadilika sana na kusema huyo msichana yeye hajampenda.

Tulikuwa na maongezi marefu sana nikitaka kujua kwa nini hajampenda hakuweza toa sababu yoyote ile zaidi ya kusema hajamwingia moyonibsuala hili nilikuja kumshirikisha baba alipotoka safari alionekana kulikubali lakini alipoenda kuongea na mama alirudi amebadilika naye anaunga mkono anachosema mama ingawa hajawai mwona huyo msichana hata siku moja.

Siku zikaenda mgogoro ukiwa mkubwa mpaka siku moja ya kikao mama akaja kunambia yeye kuna binti ambaye ndo anapendekeza nimwoe akanitajia huyo binti ambaye ni mtoto wa rafiki yake kiukweli namfahamu huyo binti na toka nimemwona sikuwahi kujenga naye hisia hata siku moja sikuwahi mfikiria kuwa hata mpenzi au kusema kuwa kuna siku nitakuwa na hamu ya kusex naye nilimwambia mama kuwa huyo binti mimi sijamuafiki.

Mama aliendelea kusisitiza kuwa huyo ndiye chagua sahihi lakini nachowaza kuwa ni chaguo sahihi kwake si kwangu nami nahitaji mtu ambaye awe sahihi kwangu kama mapungufu basi yasemwe yaliyopo ya huyu wasiyemtaka lakini pia hata mimi nina mapungufu yangu kwanini wasinambie kwanza ya huyo msichana ili nipime halafu niamue mwenyewe?

Zaidi ya mwaka sasa tumekuwa na ukinzani huo bahati mbaya sana baba ni msomi na mama ni msomi pia maisha yao yoote wanaishi mjini na wamefanikiwa kutembea hata nchi za nje kwanini waje na mawazo haya ya kizamani?binafsi nimefikia hatua nasema pengine nisije kuoa kabisa au niondoke nikaanze maisha yangu peke yangu na huyo dada nikikata mawasiliano nao kabisa.

Maana mama anasisitiza kuwa nikimwona huyu yeye hatofika hata nyumbani kwangu ni kama ametengeneza chuki naye ambayo siielewi inatoka wapi kaamua kumchukia kabisa na kusingizia mengi kuwa huyo binti familia yake ni wachawi wakati huyo dada familia yake ipo mbali na jiji la dar unapita mikoa mingine kadhaa kufika huo uchawi ni upi?

Ok kama anasema kuwa binti huyu ana madhaifu mbona nikimwambia yeye au baba wanitajie hawataji lolote zaidi ya kusema tu hawamtaki? ni jambo ambalo limenitesa nimefikia hatua mbayo sielewi mwisho wake ni nini maana ni mgogoro wa kifamilia ambao unanifanya nianze hata kuwachukia wazazi wangu maana ni kama wamedhamiria kunitesa,kuniumiza pasipo sababu.

Nipo njia panda nawaza niondoke nyumbani nikaanze maisha sehemu isiyojulikana kwao?nikate mawasiliano nao kabisa?mimi binafsi niende huko kwa wazazi wa huyu binti nikajitambulishe na kuanza akufuata process nyingine zote pasipo wazazi wangu?au ndo niamue kabisa kuachana na habari za kuoa niishi tu bila mke? maana huyu dada katika uhusiano wetu wa zaidi ya miaka miwili tumefanya mengi sana tumesaidiana mengi kiasi kwamba ni ngumu leo hii kumwacha nianze maisha mapya na mwanamke mwingine.

Na yeye ameshakataa kwao wachumba zaidi ya watano akiamini mimi naye tutaoana nifanye nini katika jambo hili ndugu zanguni nimekata tamaa sana na sitamani kuendelea kuteseka katika jambo hili."

msaada wa maoni na ushauri kwa kijana mwenzenu.
 
Wazazi wengine bana kazi kutia wanao ktk nyakati ngumungumu.

Apo ukiacha kuwasikiliza alafu ikatokea mmezenguana utasikia "Tulikuambia sisi,, asosikia la mkuu"...kumbeeeee changamoto nashida tumeumbiwa wanadamu.


Aya ukisema uwasikilize napo.,, utakua umeisaliti nafsi yako ,hisia zako ,nando mwanzo wa kuja kua "Mchepukaji Guru".


Aiseee kama umeona anastahili kua Mke yaaan
Ana polite devotion
TABIA NJEMA (nje na ndani)
MCHA NA MWENYE HOFU NA MUNGU
Mzuri yaan mzuri wa Umbo na sura
Basi
Nakuunga mkono ingawa sikujui na hunijui.

Ila kama hana nayo basi namm naungana naBaba na Mama yako. Kukuambia kua "Ikiwa utafuata Mwili wako na sio akili, Basi BAADAE UTAPATA TABU SANA"


kwaufupi mimi niko katikati maana sitaki kwa hii inshu yako unione Mchawi
 
Tatizo la kwanza nadhani umekuliwa kwa mama zaidi, pili familia haina uhusiano wa kiafrika yaani kumheshimu shangazi, mjomba, Babu nk.Tatu mama ndiye kiongozi wa familia. nne umewekeza sana kwa huyu binti. ukichambua hayo mambo manne unaweza kupata mwanga wa suluhisho la jambo lako. Kumbuka hili jambo ni lako binfsi na maisha yako, jawabu linatakiwa litoke kwako ambalo unaweza kulitekeleza wewe mwenyewe.
 
but huyo mama alipaswa aseme anaona mapungufu gani halafu amwache mtoto aamue. dunia ya sasa si ya kuchaguliana mke hata siku moja.

Wasikilize wazazi wako,lazima mama ako kaona mbali achana na huyo binti na uoe pendekezo la mama ako,ukilazimisha utakuja kujuta bure
 
Mkuu m nlipelekaga mchumba home kumtambulisha,alikaa na maza siku 2 tu lakn mama akasema mwanangu huyu mwanamke hakufai,nka2liza bongo nkaanza kumdadis nikaja nkaprove maneno ya maza,kweli alkua haja2lia hata kidogo,nilimuacha kimya kimya na sikuwahi kumuulza maza ali2mia criteria gani kumpima na kugundua tabia zake.
 
ila mchunguze huyo binti wanaemtaka wao kama yupoje, ujue tabia yake bila yy kujua kama unamchunguza, then fanya comparison na unayemtaka ww.
 
pole we oa tu wao wameshqmaliza majukumu yao ya kukulea hadi ujitambue kwa kuwa hawataishi na ww milele oa huyo unayetarajia kuishi naye milele
 
Mkuu m nlipelekaga mchumba home kumtambulisha,alikaa na maza siku 2 tu lakn mama akasema mwanangu huyu mwanamke hakufai,nka2liza bongo nkaanza kumdadis nikaja nkaprove maneno ya maza,kweli alkua haja2lia hata kidogo,nilimuacha kimya kimya na sikuwahi kumuulza maza ali2mia criteria gani kumpima na kugundua tabia zake.
Kuna wazazi wengine wanahitaji muda mchache tu kugundua tabia za mchumba wako
 
Fungeni ndoa huko mliko maisha yaendelee wazazi wakaribisheni kwenye unstick wa wajukuu zao
 
ni vema ukakaa mahali moyo wako ulipo, ukienda kwa huyo ''chaguo la mama'' hakika hutofurahia maisha nakuambia, siku mbili tatu tu utaanza kujilaumu na kumkumbuka yuleee''chaguo la moyo wako''.....komaa na cinderela wako man ipo siku nao watakuja kukuelewa, ni vema sana kuwasikiliza wazazi wetu lakini sio sahihi kabisa kufuata kila wanachosema hasa kwa umri huu wa 30's ,ukifuata mawazo haya ya bimkubwa ndio ataanza kukupangia idadi ya watoto na lini uanze kuwazaa..hebu waoneshe ukomavu wako kwanza then uwaone wataelewa tu,

Niko upande wako na naunga mkono hoja
 
Usahihi wa wazazi ungekua mkubwa kama wasingekua nwa mwanamke waliyemwandaa. Yani wangesema huyu hakufai halafu wakatulia ili utafute mwingine. Lakini sasa wanakupa mbadala inamana walishapanga hata wazazi wa huyo binti walishawahakikishia kuwa utaoa binti yao,,,


Sasa we waambie huyu kama hamjampenda ntatafuta mwingine, uone jinsi watakavohaha. 😀😀😀

Wao wanataka umuoe wao si kingine
 
Back
Top Bottom