Malisa akataa ubunge

Malisa akataa ubunge

Alfu Lela Ulela

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2010
Posts
1,255
Reaction score
77
Rais wa serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha SAUT Mwanza Bw. Malisa Godlisten amenukuliwa na gazeti la Mwananchi la tar.13/03/2013 kuwa hana mpango wa kugombea ubunge mwaka 2015.

Gazeti hilo ambalo lilifanya mahojiano na Malisa na kuandika makala ndefu kuhusu maisha yake ya uongozi, alisema anaweza kufikiria kugombea udiwani nafasi itakayompa fursa ya kugombea umeya wa manispaa ya Moshi.

Alisema sababu kubwa ya kugombea umeya ni kutaka kuifanya Moshi kuwa manispaa ya mfano katika maendeleo. Aidha aliwaasa wasomi waache kukimbilia zaidi ubunge na wawaze zaidi kufanya mabadiliko katika serikali za mitaa kwanza.

Chanzo: MWANANCHI.
 
we KIKOKOTOZI cha kuuzia nyanya tu!huwezi kutumika kosolve trig!!!
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli Meya ana nafasi kubwa na nzuri ya kuwasaidia wananchi wake katika shughuli za maendeleo kuliko mbunge,meya ana budget na ana uwezo wa kukusanya kodi,fees etc na kuzitumia vizuri kwa wananchi wake...ana idea nzuri ya kuwasaidia mangi wenzake,keep it up!!
 
Kama ni jimbo la Ndesa pesa anjua hawezi pata asitucheze shere...
Rais wa serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha SAUT Mwanza Bw.Malisa Godlisten amenukuliwa na gazeti la Mwananchi la tar.13/03/2013 kuwa hana mpango wa kugombea ubunge mwaka 2015. Gazeti hilo ambalo lilifanya mahojiano na Malisa na kuandika makala ndefu kuhusu maisha yake ya uongozi, alisema anaweza kufikiria kugombea udiwani nafasi itakayompa fursa ya kugombea umeya wa manispaa ya Moshi. Alisema sababu kubwa ya kugombea umeya ni kutaka kuifanya Moshi kuwa manispaa ya mfano katika maendeleo. aidha aliwaasa wasomi waache kukimbilia zaidi ubunge na wawaze zaidi kufanya mabadiliko katika serikali za mitaa kwanza. SOURCE: MWANANCHI.
 
moshi bwana kila mchaga anataka kuwa kiongozi kazi ipo

Here we GO... Wachagga ni zaidi ya Makabila 20 na lunga tofauti 22 sasa sijui Unaongelea nini... Umeona wanautaka Urais Zaidi ya KIKWETE na Benard Membe???
 
Nadhani ya pili ndo sahihi zaidi.

Naam,

Maana nilivyoona heading nikajua kuna Mtanzania kateuliwa na rais Kikwete kuwa mbunge akaamua kukataa.

Nikataka kujua zaidi.

Kumbe mtumtu tu "kakataa" ubunge kama mie "nilivyokataa" kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa?
 
Naam,

Maana nilivyoona heading nikajua kuna Mtanzania kateuliwa na rais Kikwete kuwa mbunge akaamua kukataa.

Nikataka kujua zaidi.

Kumbe mtumtu tu "kakataa" ubunge kama mie "nilivyokataa" kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa?
Kiranga acha kupiga watu matongo!!

Kwa hiyo huju jamaa anatuletea ile hadithi ya sungura aliyejifanya mjanja pale inaposema,
Sizitaki mbichi hizi" Sungura akagumia,
Naona nafanya kazi, bila faida kujua",
Yakamtoka machozi matunda akalilia,
Matunda akalilia, Sungura nakuambia.

Sio kama hakutaka, sasa nakupasulia,
Matunda aliyataka, ndiyo kisa akalia
Tunajua hakufika, alichoka kurukia,
Alichoka kurukia, Sungura nakuambia.

Nafikiri anadhani watu hatufahamu kama kuna wengine mpaka wanatoa kafara na matambiko pamoja na kwamba wana pesa za kuhonga ili tu kuupata ubunge.

Ubunge kwa Tanzania ni sawa na mshindi wa Mega millions dollar jackpot.
 
Hata akigombea Udiwani ataambulia patupu make Moshi hawawezi kupitisha Gamba.
 
Heading za kiudaku,
hlf hawa jamaa wanaotoka vyuo vya kata mara wanataka urais (yule wa sebastian korowa) mara ubunge,
waendelee kuota mchana na usiku,
 
Here we GO... Wachagga ni zaidi ya Makabila 20 na lunga tofauti 22 sasa sijui Unaongelea nini... Umeona wanautaka Urais Zaidi ya KIKWETE na Benard Membe???

kaka mbona unakua mkali,...pambana kwa hoja
 
Rais wa serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha SAUT Mwanza Bw. Malisa Godlisten amenukuliwa na gazeti la Mwananchi la tar.13/03/2013 kuwa hana mpango wa kugombea ubunge mwaka 2015.

Gazeti hilo ambalo lilifanya mahojiano na Malisa na kuandika makala ndefu kuhusu maisha yake ya uongozi, alisema anaweza kufikiria kugombea udiwani nafasi itakayompa fursa ya kugombea umeya wa manispaa ya Moshi.

Alisema sababu kubwa ya kugombea umeya ni kutaka kuifanya Moshi kuwa manispaa ya mfano katika maendeleo. Aidha aliwaasa wasomi waache kukimbilia zaidi ubunge na wawaze zaidi kufanya mabadiliko katika serikali za mitaa kwanza.

SOURCE: MWANANCHI.


Kupitia chama gani?
 
Back
Top Bottom