Malipo ya dhuluma: Benjamin Sitta uliingia kimafia utang'olewa kimafia

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,772
218,394
Hakuna asiyefahamu kwamba 2015 ccm ilikataliwa Jijini Dar es Salaam , madiwani wengi na wabunge wengi wa Upinzani walichaguliwa na wananchi , Meya wa Manispaa ya Kinondoni akatokana na wapinzani , Meya wa Ilala vivyo hivyo ikiwa ni pamoja na Meya wa Jiji .

Mengi yalitokea ikiwa ni pamoja na ccm kuleta madiwani mamluki kutoka Mchambawima na Kisiwandui ili kuja kuongeza idadi ya wapiga kura za kuchagua Meya wa jiji , hata hivyo wakaangukia pua , ili maneno yasiwe mengi ngoja nijikite Kinondoni , baada ya CCM kushindwa Kinondoni ikaamua kupanga njama za kuigawa Manispaa hiyo kwenye makundi mawili , huu mpango ulikuwepo ila uliharakishwa kwa makusudi maalum ili kuibeba CCM, pamoja na kuigawanya Kinondoni lakini bado kura za CCM zikawa hazitoshi pande zote mbili , ndipo ukafanyika umafia wa kuwahamisha kibabe madiwani wa Upinzani waliokuwa na haki ya kubaki kinondoni na kuwapeleka Ubungo , wakaletwa na mamluki wa kuteuliwa ili kuiongezea nguvu CCM na Hatimaye Benjamin Sitta akawa Meya kwa njia ya dhuluma iliyoacha manung'uniko makubwa sana .

Labda kwa ajili ya kuweka kumbukumbu vizuri ni kwamba ccm ililazimisha umeya wa Kinondoni ili kuongeza wigo wa wizi na upigaji , ushahidi ni hili la Kinondoni la kujenga Coco Beach kwa Bil 14 , huu ni wizi wa mchana , sasa hili ni moja vipi kuhusu miradi mingine ?

Benjamin Sitta ulipewa Umeya kimafia kwa huruma ya baba yako , hukuwa na uwezo wowote na wala hukuwahi kuwa na uwezo kokote ulikopita , Sasa wamekutumia na wanajiandaa kukung'oa ili kuua soo .

Kila lenye mwanzo halikosi mwisho .
 
Ataenda kuroga kule alikopewa urozi Tulia
 
Wamepangana kwiba tu. Mpaka inatia aibu. Kila chenye mwanzo hakikosi kuwa na mwisho. Ujanja ujanja na wizi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…