Malezi ya watoto kwenye Teknolojia

Malezi ya watoto kwenye Teknolojia

Display Name

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2014
Posts
423
Reaction score
451
Salamu wakuu,

Maendeleo ya teknolojia yana changamoto zake na pia faida kubwa sana kwenye maisha yetu, hii pia imeonekana kwenye malezi ya watoto na maisha yao kwa ujumla

Je, watoto wanaolelewa kwenye kizazi hiki cha kununua vitu vya kuchezea kimepoteza ubunifu ukilinganisha na kizazi ambacho watoto walikuwa wanatengeneza vitu vya kuchezea wenyewe?

Hapo zamani kidogo mtoto akitaka kucheza mpira itampasa atengeneze mpira mwenyewe kwa vifaa vilivyokuwa vinapatikana kama vile nguo chakavu, vipande vipande vya magodoro na kamba, lakini sasa hivi mtoto huomba anunuliwe mpira dukani

Vile vile, mtoto akitaka mdoli wa kuchezea ilimbidi achukue nguo chakavu na kutengeneza mdoli wake au wenginge walitengeneza kwa kutumia mkungu wa ndizi ila kwa sasa mdoli anapatikana dukani
-
Pia, miaka ya nyuma kidogo watoto walikuwa wakitengeneza magari ya aina tofauti tofauti kwa kutumia makopo au nyaya, kamera kwa kutumia vikopo vilivyoisha mafuta ya kujipaka na hata nyumba ya kutumia maboksi.

Njia hii iliwafanya watoto wa miaka hiyo kuwa wabunifu na wenye kufikiria kwenye sanaa ukiwalinganisha na watoto wanaonunuliwa kila kitu kikiwa kimetengenezwa.

Je, wewe una maoni gani kwenye ukuaji wa teknolojia na mabadiliko haya? Unadhani watoto wa sasa wanapoteza uwezo wa kuwa wabunifu ukilinganisha na miaka ya nyuma?
1136068
1136069
1136070
1136071
 
Ni kweli unachokisema lakini ukiliangalia hili katika angle nyingine utajua kuwa ile ilikuwa ni Traditional world na kwa sasa ni digital world. Ubunifu wa traditional ni tofauti na digital era hivyo, Ni jukumu la wazazi kujifunza soft skills za nyakati zetu ili waweze kuwasaidia watoto kuendana na ulimwengu wao ambao ni more beneficial kuliko hiyo ya kutengeneza mipira ya karatasi ambayo kiuhalisia haikuongeza value yoyote katika future zetu zaidi ya fun. Mtoto akijifunza IT au la tu kuelewa Digital world inafanyaje kazi ni muhimu kwa sasa na kwa maisha yake ya baadae, So, ubunifu upo ila ni wa nyakati tofauti na kwa malengo tofauti
 
Mambo na yanabadilika na unataka tubaki kama enzi za mwaalimu?
Kuhusu ubunifu hata vinavyotengenezwa sahv ni ubunifu kama hyo midoli bado inatengenezwa kwa nguo lakin kwa sasa wamei modernize
 
Back
Top Bottom