Mungu awafanyie wepesi wenye magonjwa na hali zisizo nzuri haswa kipindi hiki ambacho serikali yetu inachukua tahadhari za msingi katika kupambana na virus vya covid 19
Tunaimani na kazi mnazozifanya haswa katika kuhakikisha serikali yetu inakusanya mapato katika rasilimali zetu za madini ya dhahabu pasi na shaka lolote
Lalamiko langu kuu.
Maafisa madini wilaya ya Chunya mnafunga makarasha bila utaratibu wa msingi unakuta mtu anakosa lakumpa maelekezo pengine bango la kuutambua mwalo kaweka bango la mbao na linaonekana wazi wazi na kalipia tozo sitahiki za kuutambua mwalo na yupo kisheria lakini mnamsimamisha kazi alipe faini.
Tunaomba mtufungie kwa utaratibu na mwenye haki muaacheni
MABANGO YA CHUMA yanavunjwa usiku watu wanaenda kupima na kuuza chuma chakavu
Tunaomba sisi ni watanzania wawekezaji kama hao wanaotoka nchi zingine kwanini msifate misingi ya utumishi ili tuishi kwa amani
Ankol nakusalimu kwa jina la Gold...Utaratibu wavibao vya utambuzi wa mialo na maduara ni mzuri sana ila nadhani mngeshinikizwa namba zionekane na sio aina ya vibao vutumikavyo...Kwetu tunatumia mbao pana nzuri na rangi nyekundu na maafisa madini wamevifurahia viko poa....Hao w atakua na jambo lao...Vip marudio (Kanyero) lipo la kutosha tuje tuchenjue