Makundi haya mawili yanaweza kumsaliti Rais Samia muda wowote

Acceptable

Senior Member
Oct 7, 2020
153
302
Mama ameingia na upepo mzuri sana kwa kutoa matumaini kwa Watanzania kupitia maneno tu watu wamefurahi na kusubiri vitendo sasa.

Inaonekana kuna kundi kubwa sana la watu walikuwa na majonzi na simanzi katika nchi yao kwa muda mrefu sana. Kama tunavyojua au kuaminishwa kwamba maneno huumba lakini yanaweza kuumba kitu kizuri au kibaya.

Ninachokiona hapa watu wanamsifu sana mama ila napenda kutoa angalizo kwa wasaidizi wa mama wamwambie; Mama asipokuwa makini nae watamchukia kama walivyokuwa wanamchukia Anko. Sababu zitakazofanya watu wa mchukie ni zilezile zilizofanya watu wamchukie Anko. Lakini kuna makundi makuu mawili haya yanashauku kubwa sana ya kupata unafuu wa maisha nayo ni:

Kundi la vijana waliomaliza vyuo wana matumaini kwamba wataajiriwa na mama baada ya kula msoto wa kukaa nyumbani kwa zaidi ya miaka 4. Huku wenye connection na bahati za mitende wakipata nafasi za kazi kwa kudonoa donoa.

Kama ikitokea Mama asiwaajiri vijana waliohitimu vyuo mbalimbali lazima watamgeuzia kibao kama walivyofanya kwa Anko, watamchukia kwasababu hakutakuwa na tofauti yoyote kati yao.

Kundi la wafanyakazi ambao kwa miaka mitano hawajapata nyongeza ya mishahara. Natumaini yao kwasasa yapo kwa Mama kwamba atawaongezea mishahara yao. Kama itatokea Mama akashindwa na yeye kuwaongezea mishahara basi na yeye watamchukia kama walivyokuwa wanamchukia Anko.

Muda utaamua kwamba nafuu na afadhali ipi ni bora kuliko nyingine.
 
Upo serious kweli, kama unategemea serikali kuajiri graduates wote unaota ndoto za mchana. Nchi kubwa na zenye viwanda vya kutosha zimeshindwa kumaliza tatizo la ajira. Labda huyo mama yako awaajiri mashambani kama shamba boyz and girls ndio anaweza kumaliza tatizo la graduates kukosa ajira.
 
Upo serious kweli, kama unategemea serikali kuajiri graduates wote unaota ndoto za mchana. Nchi kubwa na zenye viwanda vya kutosha zimeshindwa kumaliza tatizo la ajira. Labda huyo mama yako awaajiri mashambani kama shamba boyz and girls ndio anaweza kumaliza tatizo la graduates kukosa ajira.
Kama graduates wana mawazo hayo kwakweli itabidi wasahau ngumu sana.
 
Mama hawezi ajiri wote Ila walau iwe Kama awamu ya kikwete baadh ya kada ziliajiriwa kilingana na umuhimu mfano afya na elimu kilimo na ufugaji

Lakn Magufuli mdwanzi jinga dikteta lofa mshamba aliziminya kabisa badala yake uvccm ndio iligeuka utumishi

Jaman vijana huku mtaan wanateseka na wanafrustration mitaj hawana wafanye nn
 
Upo serious kweli, kama unategemea serikali kuajiri graduates wote unaota ndoto za mchana. Nchi kubwa na zenye viwanda vya kutosha zimeshindwa kumaliza tatizo la ajira. Labda huyo mama yako awaajiri mashambani kama shamba boyz and girls ndio anaweza kumaliza tatizo la graduates kukosa ajira.
...!
 
Ili kutatua tatizo la ajira kwa GRADUATES tusitegemee kuwa SASHA atalitengua kwasababu hili tatizo root cause yake ni aina ya Elimu tunayotoa vyuoni!! Vijana wanasomea taaluma ambayo haiendani na matakwa ya wale wanaojiri!!! The education curriculum must be geared towards the satisfaction of the market demand.
 
Wasomi wenye upeo mdogo ndio kama huyu mleta hii mada! Wewe bado unafikiria mambo ya kuajiriwa na kuongezewa mishahara ?! Dunia hiyo ilishapitwa na wakati ndugu! ( Soma kitabu cha Robert Kiyosaki: Four Quadrants)!
Watu wenye akili wanapigania mazingira mazuri ya "wealth creation"!
 
Wasomi wenye upeo mdogo ndio kama huyu mleta hii mada! Wewe bado unafikiria mambo ya kuajiriwa na kuongezewa mishahara ?! Dunia hiyo ilishapitwa na wakati ndugu! ( Soma kitabu cha Robert Kiyosaki: Four Quadrants)!
Watu wenye akili wanapigania mazingira mazuri ya "wealth creation"!
Je Tanzania tumejitosheleza watumishi wa Afya, Elimu, na sekta zingine hadi tushindwe kuajiri na kusema kwamba changamoto ya ajira ni dunia nzima? Kufananisha changamoto za ajira za developed countries na sisi developing countries ni ukichaa!


Kama tunataka kumaliza tatizo la ajira basi tubadili mfumo wa elimu yetu.
 
Muda ni mwalim mzuri mzigo alionao ni mzito hasa ajira kuongeza mshahara ujenzi miradi mikubwa yote mfumuko bei kurudisha hela sekta binafsi na mtaani serikali kuacha kufanya business ......kazi ngu.u pia kudhibiti wasaka tonfe awamu 5
 
Graduates wanatakiwa wajiajili, na sio lazima wajiajiri kupitia taaluma walizosomea, watakuwa hawana akili kama wote watategemea kuajiriwa na serikali
 
Ili kutatua tatizo la ajira kwa GRADUATES tusitegemee kuwa SASHA atalitengua kwasababu hili tatizo root cause yake ni aina ya Elimu tunayotoa vyuoni!! Vijana wanasomea taaluma ambayo haiendani na matakwa ya wale wanaojiri!!! The education curriculum must be geared towards the satisfaction of the market demand.
Na hilo jambo la mitaala pia mama Samia amelisemea ngoja tuone kama wizara itakuja na mitaala inayoeleweka!
 
Mama ameingia na upepo mzuri sana kwa kutoa matumaini kwa Watanzania kupitia maneno tu watu wamefurahi na kusubiri vitendo sasa.

Inaonekana kuna kundi kubwa sana la watu walikuwa na majonzi na simanzi katika nchi yao kwa muda mrefu sana. Kama tunavyojua au kuaminishwa kwamba maneno huumba lakini yanaweza kuumba kitu kizuri au kibaya.

Ninachokiona hapa watu wanamsifu sana mama ila napenda kutoa Wangalizo kwa wasaidizi wa mama wamwambie; Mama asipokuwa makini nae watamchukia kama walivyokuwa wanamchukia Anko. Sababu zitakazofanya watu wa mchukie ni zilezile zilizofanya watu wamchukie Anko. Lakini kuna makundi makuu mawili haya yanashauku kubwa sana ya kupata unafuu wa maisha nayo ni:

Kundi la vijana waliomaliza vyuo wana matumaini kwamba wataajiriwa na mama baada ya kula msoto wa kukaa nyumbani kwa zaidi ya miaka 4. Huku wenye connection na bahati za mitende wakipata nafasi za kazi kwa kudonoa donoa.

Kama ikitokea Mama asiwaajiri vijana waliohitimu vyuo mbalimbali lazima watamgeuzia kibao kama walivyofanya kwa Anko, watamchukia kwasababu hakutakuwa na tofauti yoyote kati yao.

Kundi la wafanyakazi ambao kwa miaka mitano hawajapata nyongeza ya mishahara. Natumaini yao kwasasa yapo kwa Mama kwamba atawaongezea mishahara yao. Kama itatokea Mama akashindwa na yeye kuwaongezea mishahara basi na yeye watamchukia kama walivyokuwa wanamchukia Anko.

Muda utaamua kwamba nafuu na afadhali ipi ni bora kuliko nyingine.
Watu wanauelewa mkubwa Sana,huwezi wadanganya pia Rais ni taasisi
 
Back
Top Bottom