Makosa yanayofanywa katika ndoa changa

Makosa yanayofanywa katika ndoa changa

Himidini

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2013
Posts
5,534
Reaction score
4,190
^^
Kumtafuta mtu unaetaka siku moja uungane nae katika maisha yako yote yaliyobakia ni jambo moja na kumudu kuishi nae ni jambo lingine linalojitegemea,
Inatokea mara nyingi sana wawili hawa wanapoingia ktk ndoa wanashangaa kuona mambo yako tofauti na matarajio yao.
...
Ukiwa katika uchumba au mwanzoni mwa maisha ya ndoa,ukumbuke kuepuka lawama hizi ambazo unaziita lawama
...
NDOA NI MAISHA UCHUMBA NI MAPENZI
Inatokea mara nyingi unashangaa ghafla au taratibu yale uliozoea ktk uchumba mf. Kutumiana text sms dia uko wapi? I love U cwtie mara tatu kwa siku,outing kila weekend n.k Yanapotea upesi,,basi ujue hapo ulipo mapenzi yamechukua mkondo wa maisha.
...
KAZI IMEISHA KILA JAMBO LITAKUWA SAWA
Wapo wanaodhani kuwa ukiolewa au hata ukioa basi,mambo yameisha na kila kitu kitaenda upendavyo La! Hili ni kosa,hapo ndipo kazi imeanza,kujaliana kushauriana kuwa na akili ya kutazama mbele imeanza
...
AMEANZA KUNIAMRISHA AU KUNIPANGIA
Unaweza kujikuta yule ambae alikuwa anakubembeleza kwanza ndo ufanye jambo fulani,mf. Dia please naomba unisaidie kufua,Switi mi ugali kila siku thakiii na mengineyo Leo hii anakuambia fanya hivi acha lile,nimeishiwa nguo ninunulie
Haina maana kuwa hakupendi tena ila ndoa imechukua mkondo wa TIMIZA WAJIBU KWANZA
...
Je unajua siku 14 mpaka 31 ulizoanza nazo ktk ndoa ndizo zitaongoza maisha yako yote ya ndoa?
Ndoa inapokuwa changa kwa siku hizo kila mmoja hutaka kuchukua mamlaka na utawala wa nyumba.
Cheza akili yako vizuri kuhakikisha unamiliki vizuri nafasi inayokustahili..ukichukua ya mwenzio utaikumbuka methali ya wahenga isemayo
AJAE KISIMANI WA KWANZA HUNYWA MAJI MAENGE
^^
 
nice thread Himidini ,kama wote tukiyafahamu haya ndoa kuvunjika zitapungua.haya ni mambo madogo lakini ni muhimu sana yasipuuzwe
 
Last edited by a moderator:
Kimsingi ndoa ni taasisi kama zilivyo taasisi nyinginezo...
Huwa kuna mtwa na mtwana.
 
Hapa umenena kaka!
Hapa nakubaliana na Eiyer aliposema 'kumpenda mtu tu, isiwe kigezo cha ndoa!' Tabia na mitazamo ni vizuri kuzingatiwa! Ili hizo changes ziendane na tabia + mitazamo!!!!!
 
Katika ndoa za sasa nyingi mmoja kati ya wana ndoa ndio hujitahidi kuhakikisha ndoa inasimama mwingine ni muamrishaji tu!!
 
Mmmmmmmmmmmm! Mambo ya ndoa yanatisha si utani! Utazani mko vitani!
 
Mkuu Himidini sijaelewa hapo uliposema NDOA NI MAISHA UCHUMBA NI MAPENZI,inamaana watu wanapooana mapenzi hakuna tena?elaboration please!!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Himidini sijaelewa hapo uliposema NDOA NI MAISHA UCHUMBA NI MAPENZI,inamaana watu wanapooana mapenzi hakuna tena?elaboration please!!

^^
Yapo lakini hufika mahali pa kutegeana migongo,kulala mzungu wa nne,kila mtu kuwa na kitanda chake Mambo ambayo hayapo katika uchumba.Kila mmoja anapaswa kuwa na nidhamu na bidii ya kuleta upya wa penzi
^^
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom