Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 17,589
- 28,570
Kuna clip inatembea mitandaoni kuhusiana na mkutano wa RC Makonda jijini pamoja na wadau wa barabara za Dar es salaam.
Makonda anaonekana kuwakemea Makandarasi wawili, Dek Monte na Skol kwa kusababisha barabara kujengwa chini ya viwango Jijini.
Anaonekana Makongda akiwaambia kwa ukali" KAA CHINI", hao makandarasi wakijaribu kujieleza.
Mbaya Zaidi anwaambia kuwa katika mkoa wake wasipewe kandarasi aina yoyote ile na kuwaagiza Wakurugenzi aione kuwapa hao kazi Jinjini Dar.
Mi nafikiri maoni ya Makonda hayana kina cha kitaalam na hayana msingi wa uchunguzi wa utendaji kitaalam na kimikataba.
Jijini Dar es salaam na Halmashauri ningi kuna matatizo mukbwa yafuatayo
Yapo mengi sana yanayo wakuta makandarasi kazini.
Cha kujiuliza na chenye mantiki, mbona TANROADS wameyapunguza sana matatizo ya kiutendaji katika miradi?
Halmashauri haiwezi kutenda kazi za ujenzi wa barabara kwa misingi hafifu sana ya kitaalam iliyopo.
Kwa hiyo Makonda atafukuza wengi mkoani kwake bial kujua matatizo yanayoyakabili ujenzi wa barabara koani kwake.
Wasalaam Muwakilishi wa Rais, RC Paul Makonda.
Makonda anaonekana kuwakemea Makandarasi wawili, Dek Monte na Skol kwa kusababisha barabara kujengwa chini ya viwango Jijini.
Anaonekana Makongda akiwaambia kwa ukali" KAA CHINI", hao makandarasi wakijaribu kujieleza.
Mbaya Zaidi anwaambia kuwa katika mkoa wake wasipewe kandarasi aina yoyote ile na kuwaagiza Wakurugenzi aione kuwapa hao kazi Jinjini Dar.
Mi nafikiri maoni ya Makonda hayana kina cha kitaalam na hayana msingi wa uchunguzi wa utendaji kitaalam na kimikataba.
Jijini Dar es salaam na Halmashauri ningi kuna matatizo mukbwa yafuatayo
- Rushwa-si uongo kuwa kazi za ujenzi za Halmashauri zote nchini zinaongoza kwa kuwa na rushwa kubwa. Wafaidika wakiwa watendaji na Madiwani. Ukiona mtu anafanya kazi za Halmashauri, ujue kimemtoka kitita. Kufidia hasara ndo tunaona kazi mbovu, Zege la mifuko 6 sement inaisha kuwekwa mifuko 3!
- Utaalam mdogo kihandisi Halmashauri- Wahandisi wengi Halmashauri hawana Technical back up yaani kazi ziatolewa kwamisingi ya estimates tu na hakuna upembuzi wa kitaalam unafanywa. Michoro ya kai hakuna!
- Hakuna usimamizi wa Kitaalam- karibu kazi zote za Halmashauri usimamizi hakuna kutokana na kukosa kitu inaitwa a "Complete Project Package". Project package ina maana Design, Michoro, Msimamizi, Maabara ya ku control viwango vya kazi yenyewe.
- Miradi huwa haina Fedha-Ni jambo la kawaida kabisa kuwa miradi mingi ya Halmashauri huwa haina kabisa fedha za utekelezaji. Na kama zikiwapo hizo fedha zinakodolewa macho na huwa hazimfikii mkandarasi kwa wakati unaostahili. Hivyo kazi kusua sua na kuchelewa kukamilishwa. Ni watu wajinga tu ati wanategemea mkandarasi akakope benki kwa riba ya 25% ili akamilishe kazi, wakati hakuna kipengele cha kufidiwa hasara ya mkopo.
- Miradi kuingiliwa na wanasiasa-wengiwana omba omba vifusi, michango ya lazima kwa vyama vya siasa, kazi kwa watoto wao n.k.
Yapo mengi sana yanayo wakuta makandarasi kazini.
Cha kujiuliza na chenye mantiki, mbona TANROADS wameyapunguza sana matatizo ya kiutendaji katika miradi?
Halmashauri haiwezi kutenda kazi za ujenzi wa barabara kwa misingi hafifu sana ya kitaalam iliyopo.
Kwa hiyo Makonda atafukuza wengi mkoani kwake bial kujua matatizo yanayoyakabili ujenzi wa barabara koani kwake.
Wasalaam Muwakilishi wa Rais, RC Paul Makonda.