OMBUDSMAN mtoto
Member
- Sep 28, 2012
- 87
- 32
Makavu Makavu kwa CHAKUUWAWA
CHAKUUWAWA ndicho CHAma cha KUukaburu Umri wa WAtu WAzima ambacho kimeasisiwa na January Makamba na mwenzake Zitto Kabwe.
1. Hawa waasisi wa huu upuuzi walilewa sifa zetu (wazee kwa vijana) kuwaona kuwa wanajitahidi katika medani za siasa ama kwa kuonekana kuwa ni watetezi wa wanyonge au ni wabunifu. Walijisahau na kujiona kuwa kilichowafikisha walipofika ni umri wao wa kuzaliwa baada ya uhuru wa nchi yetu!CHAKUUWAWA- Kiuwawe!
2. Hawa ni makaburu wa umri maana wanadhani kuwa wao walipata hati milki ya kuamrisha uogeleaji wa mbegu za baba zao na urutubishaji wa mayai ya mama zao ili mimba zao zitungwe kabla ya uhuru! CHAKUUWAWA- Kiuwawe!
3. January, hujui kuwa kwa kuwabagua watu wazima katika jamii kwa kejeli kuwa hawafai kugombea unatufanya tufikirie kwa upya kama kweli ulifaulu vyema shule yako uliyosoma katika kozi ya maridhiano na ujenzi wa amani, ICAR George Mason University, US. Kwani badala ya kutangaza amani unatangaza ubaguzi uletao matabaka na vita. Katika utangulizi wa tovuti yako, (January Makamba.com), mwishoni umekiri kuwa I will finish by admitting that my last name (i.e. MAKAMBA) has helped me because of the ready-made network of willing helpers.
Kwa hiyo jina la Makamba liliweza kukubeba pengine ukaingia Foreign Affairs na kuwa karibu na Waziri JK na ukapata fursa ya kuwa katika Kampeni za JK (2005) na kuleteleza kuitwa Ikilu na kuzawadiwa wadhifa nyeti wa (Personal Assistant to the President Special Duties) na kusababisha Rais, Ikulu na CCM (T) kwa ujumla kukupa shavu katika Kampeni yako ya pesa ndefu na msukumo mkubwa kama inavyoonekana kule Bumbuli, (Bumbuli songa - by Jobiso - YouTube) na kama ilivyotegemewa ugagawiwa Unaibu-Waziri tena Wizara kama injini ya maendeleo ya nchi Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia. Je ambao hawana majina ya (ready- made network) ya kuwabeba kwa nini unawazuia wasitumie umri wao mrefu wa maisha yao ya kuwatumikia watanzania ili Wananchi wapate kuamua kama waliridhishwa na huduma zao au la? Kwa nini mnatatulazimisha tuwashindanishe watu kwa kiashirio cha usasa wa mimba iliyomzaa mgombea? Kwa nini uliamua bila aibu kupanda mbegu ya unyanyaswaji wa kiumri pale UDSM.CHAKUUWAWA- Kiuwawe!
4. Zitto kwa kuwabagua watu wazima, unatekelezaje kwa vitendo, mafunzo uliyopata katika Module 2 ya MLB hapo Bucerius Law School, Germany(accredited in 2000) au nawe umesoma kwa correspondence bila kuzama na kupata ufahamu wa mada husika e.g the topics of relevance of values and human rights maana ulisoma (2009 - 2010), wakati wewe tayari ulishakuwa Mbunge (fulltime work) toka 2005.
Kwa siku za hivi karibuni wananchi hatuhitaji kingamuzi kukusoma kuwa wewe kijana aka Prezo hakika ni mtu wa namna gani. Kama mwenzako mmelewa sifa na umejidhihirisha uwanachama mapacha wako (dual membership) ndani ya CHADEMA & CCM kwa kuleta mtafaruku mkubwa BAVICHA kwa kumtukana Dr. Slaa kuwa ni ki-Babu na kujinyanyua kwa kiburi kuwa wewe ndiye unafaa. Kamwe huwezi kujilinganisha na Dr. Slaa hata ungetafuta ubashiri wa nyota toka kwa Marehemu Yahya (check kura ya maoni hapa https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/298724-kura-ya-maoni-zitto-vs-dr-slaa-3.htm. Zito una 25% wakati Dr. Slaa ana 85% ya kura zote. Mwaga kipunga dakika za mwisho yule moderator anayekutetea kila mara achakachue uonekane wewe ndie uko juu kama ulivyozoea kucheza na media, bado hutaweza kumkaribia Dr. Slaa kwa kila vigezo vya uongozi bora. Kiukweli hata tungeweka kura ya maoni kati yako na Mnyika au Mdee utapigwa chini kwa kiasi kikubwa. Hata huko CCM kamwe hutapata nafasi yeyote kwa jinsi ulivyodharau watu wazima na wazee waliokufundisha siasa akiwemo rafiki yako Salim A. Salim ambaye naye alizaliwa kabla ya Uhuru na mbaya zaidi ni mchezo wako wa uanachama pacha ambao wewe ni janga la vyama vya upinzani. CHAKUUWAWA- Kiuwawe!
Naweza sema, kheri mzee mwadilifu, mwenye uwezo na uzoefu wa uongozi bora kuliko kijana kihuluku sadifu cha kifisadi; CHAKUUWAWA- Kiuwawe! Wakati ukifika, Wananchi waachwe, wataamua wagombea wenye sifa za uongozi bora ambazo ni zaidi sana ya birthday zao!
CHAKUUWAWA ndicho CHAma cha KUukaburu Umri wa WAtu WAzima ambacho kimeasisiwa na January Makamba na mwenzake Zitto Kabwe.
1. Hawa waasisi wa huu upuuzi walilewa sifa zetu (wazee kwa vijana) kuwaona kuwa wanajitahidi katika medani za siasa ama kwa kuonekana kuwa ni watetezi wa wanyonge au ni wabunifu. Walijisahau na kujiona kuwa kilichowafikisha walipofika ni umri wao wa kuzaliwa baada ya uhuru wa nchi yetu!CHAKUUWAWA- Kiuwawe!
2. Hawa ni makaburu wa umri maana wanadhani kuwa wao walipata hati milki ya kuamrisha uogeleaji wa mbegu za baba zao na urutubishaji wa mayai ya mama zao ili mimba zao zitungwe kabla ya uhuru! CHAKUUWAWA- Kiuwawe!
3. January, hujui kuwa kwa kuwabagua watu wazima katika jamii kwa kejeli kuwa hawafai kugombea unatufanya tufikirie kwa upya kama kweli ulifaulu vyema shule yako uliyosoma katika kozi ya maridhiano na ujenzi wa amani, ICAR George Mason University, US. Kwani badala ya kutangaza amani unatangaza ubaguzi uletao matabaka na vita. Katika utangulizi wa tovuti yako, (January Makamba.com), mwishoni umekiri kuwa I will finish by admitting that my last name (i.e. MAKAMBA) has helped me because of the ready-made network of willing helpers.
Kwa hiyo jina la Makamba liliweza kukubeba pengine ukaingia Foreign Affairs na kuwa karibu na Waziri JK na ukapata fursa ya kuwa katika Kampeni za JK (2005) na kuleteleza kuitwa Ikilu na kuzawadiwa wadhifa nyeti wa (Personal Assistant to the President Special Duties) na kusababisha Rais, Ikulu na CCM (T) kwa ujumla kukupa shavu katika Kampeni yako ya pesa ndefu na msukumo mkubwa kama inavyoonekana kule Bumbuli, (Bumbuli songa - by Jobiso - YouTube) na kama ilivyotegemewa ugagawiwa Unaibu-Waziri tena Wizara kama injini ya maendeleo ya nchi Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia. Je ambao hawana majina ya (ready- made network) ya kuwabeba kwa nini unawazuia wasitumie umri wao mrefu wa maisha yao ya kuwatumikia watanzania ili Wananchi wapate kuamua kama waliridhishwa na huduma zao au la? Kwa nini mnatatulazimisha tuwashindanishe watu kwa kiashirio cha usasa wa mimba iliyomzaa mgombea? Kwa nini uliamua bila aibu kupanda mbegu ya unyanyaswaji wa kiumri pale UDSM.CHAKUUWAWA- Kiuwawe!
4. Zitto kwa kuwabagua watu wazima, unatekelezaje kwa vitendo, mafunzo uliyopata katika Module 2 ya MLB hapo Bucerius Law School, Germany(accredited in 2000) au nawe umesoma kwa correspondence bila kuzama na kupata ufahamu wa mada husika e.g the topics of relevance of values and human rights maana ulisoma (2009 - 2010), wakati wewe tayari ulishakuwa Mbunge (fulltime work) toka 2005.
Kwa siku za hivi karibuni wananchi hatuhitaji kingamuzi kukusoma kuwa wewe kijana aka Prezo hakika ni mtu wa namna gani. Kama mwenzako mmelewa sifa na umejidhihirisha uwanachama mapacha wako (dual membership) ndani ya CHADEMA & CCM kwa kuleta mtafaruku mkubwa BAVICHA kwa kumtukana Dr. Slaa kuwa ni ki-Babu na kujinyanyua kwa kiburi kuwa wewe ndiye unafaa. Kamwe huwezi kujilinganisha na Dr. Slaa hata ungetafuta ubashiri wa nyota toka kwa Marehemu Yahya (check kura ya maoni hapa https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/298724-kura-ya-maoni-zitto-vs-dr-slaa-3.htm. Zito una 25% wakati Dr. Slaa ana 85% ya kura zote. Mwaga kipunga dakika za mwisho yule moderator anayekutetea kila mara achakachue uonekane wewe ndie uko juu kama ulivyozoea kucheza na media, bado hutaweza kumkaribia Dr. Slaa kwa kila vigezo vya uongozi bora. Kiukweli hata tungeweka kura ya maoni kati yako na Mnyika au Mdee utapigwa chini kwa kiasi kikubwa. Hata huko CCM kamwe hutapata nafasi yeyote kwa jinsi ulivyodharau watu wazima na wazee waliokufundisha siasa akiwemo rafiki yako Salim A. Salim ambaye naye alizaliwa kabla ya Uhuru na mbaya zaidi ni mchezo wako wa uanachama pacha ambao wewe ni janga la vyama vya upinzani. CHAKUUWAWA- Kiuwawe!
Naweza sema, kheri mzee mwadilifu, mwenye uwezo na uzoefu wa uongozi bora kuliko kijana kihuluku sadifu cha kifisadi; CHAKUUWAWA- Kiuwawe! Wakati ukifika, Wananchi waachwe, wataamua wagombea wenye sifa za uongozi bora ambazo ni zaidi sana ya birthday zao!