JUMANJI - 1
-
Mwandishi Deo kitasa -
Umewahi Kusikia Kuhusu mchezo wa Jumanji? Umewahi Kusoma Kitabu Cha Jumanji?
Jumanji!! Welcome To The Jungle "Karibu Msituni" Ndio Kauli Mbiu Yake.
Mchezo Huu umepelekea mpaka kutolewa kwa movie mbili zenye matukio ya kufanana.
-
Kwa wale wanaofuatilia movie Bila Shaka umekwisha kupitia movie ya Jumanji ya Desemba 15 mwaka 1995, pamoja na ile ya tarehe 5 Desemba mwaka 2017 huku tukitegemea ujio wa Jumanji 3 mwaka huu tarehe 12 Desemba.
-
Turudi Kwenye Mada Yetu,
Jumanji ni Michezo Ya kimiujiza au yenye kuhusisha masuala ya Giza (Black Magic). Jumanji ni neno la kizulu lenye maana ya "madhara mengi" Kwa Kimombo "Many Effects".
-
Jumanji Ni miongoni mwa michezo hatari pamoja na Ule Wa Ouija.
Ni mfano wa mchezo wa Draft ila huu Una Husisha kitabu kinachofunguliwa ili mchezo uanze.
-
Kutokana na taarifa za siri sana kutoka vyama vya siri inadaiwa kuwa Jumanji ni zao la watu wawili, hawa ni waaguzi na wachawi wawili Wenye daraja la juu sana Kwenye Uchawi. -
Mmoja ni kutoka Afrika na mwingine ni Muingereza, Ilikua katikati ya miaka ya 1800. Hawa jamaa walikuwa ni mashabiki na wapenzi sana wa masuala ya kishetani. Na walitamani kutengeneza kitu ili iwe kama ukumbusho wa mapenzi yao kwenye fani ya nguvu za giza. -
Pia walipewa nguvu na msukumo mkubwa ulitokana na ile hali ya wazungu kupenda kutembea maporini na misitu mikubwa ali maarufu kama Safaris ndani ya falme za kiafrika kwa wakati huo.
-
Mambo Yalikua Hivi, mwanzoni nia yao ilikuwa njema kwani walitaka kuwazungusha tu mwisho wapoteze hamu ya kuja tena Afrika, Lakini Matokeo Yakawa Tofauti, baadae mchezo ukawa ni wa kuleta hata kifo na ulemavu.
-
Ingawa wao ndio waliokuwa kama Mfano (Sample) ya kujaribu mchezo huo ila matokeo yakawa hasi kwani ndio Ulikuwa Mwisho wa Uhai Wao, Wote Walikufa.
Mwanzoni walitamani pia wapate maisha ya milele wakiwa ndani ya mchezo huo.
Yaani inasemekana wamekwisha kufariki ila katika huo mchezo wapo hai.
-
ITAENDELEA -