Makampuni ya simu tusaidieni kuweka huduma hii muhimu

Bila bila

JF-Expert Member
Dec 20, 2016
21,495
37,787
Huduma za upigaji na upokeaji simu zinaendelea kuboreshwa siku hadi siku. Miongoni mwa huduma inayofurahiwa kwa sasa ni ile ya baadhi ya makampuni kuwezesha mteja aliyepigiwa simu ikiwa offline kupata ujumbe kwamba fulani alikutafuta muda fulani. Huduma hii imesaidia katika mambo mengi ikiwemo kuokoa maisha, kuepusha mafumanizi nk.

Huduma nyingine inayofurahiwa ni ile ya kuruhusu simu kuingia wakati mtu anaongea na simu nyingine. Ili kuiboresha huduma hii binafsi naomba iwekwe option ya mtu anayepigiwa simu ya pili kuwa na uwezo wa kukata mawasiliano na anayeongea naye ili apokee simu mpya inayoingia kutokana na umuhimu.

Mfano mtu anaongea habari ya Simba na Yanga ghafla inaingia simu ya Bosi wake, awe na uwezo wa kukata mawasiliano yasiyo ya lazima ili kupokea simu muhimu.
 
Nadhani hilo linaenda beyond operator's capacity; linagusa hadi phone manufacturers. Tusubirie Ulaya na Marekani wakiona lina umuhimu watatengeneza simu zinazo support hiyo kitu and eventually zitatufikia tu Boss kama tunavyosubiria 5G.
 
Sijaelewa mbona mimi simu yangu nikizima kama mtu alipiga nikiwasha mbona naona wote walionipigia simu ilipokuwa imezimwa?
 
Huduma za upigaji na upokeaji simu zinaendelea kuboreshwa siku hadi siku. Miongoni mwa huduma inayofurahiwa kwa sasa ni ile ya baadhi ya makampuni kuwezesha mteja aliyepigiwa simu ikiwa offline kupata ujumbe kwamba fulani alikutafuta muda fulani. Huduma hii imesaidia katika mambo mengi ikiwemo kuokoa maisha, kuepusha mafumanizi nk.
Huduma nyingine inayofurahiwa ni ile ya kuruhusu simu kuingia wakati mtu anaongea na simu nyingine. Ili kuiboresha huduma hii binafsi naomba iwekwe option ya mtu anayepigiwa simu ya pili kuwa na uwezo wa kukata mawasiliano na anayeongea naye ili apokee simu mpya inayoingia kutokana na umuhimu. Mfano mtu anaongea habari ya Simba na Yanga ghafla inaingia simu ya Bosi wake, awe na uwezo wa kukata mawasiliano yasiyo ya lazima ili kupokea simu muhimu.
Nadhani hilo linaenda beyond operator's capacity; linagusa hadi phone manufacturers. Tusubirie Ulaya na Marekani wakiona lina umuhimu watatengeneza simu zinazo support hiyo kitu and eventually zitatufikia tu Boss kama tunavyosubiria 5G.
Sasa lipi ambalo halipo kwenye simu?
Ukiacha la ujumbe simu inapokuwa imezimwa, yaliyobaki ni uwezo wa simu na yapo kwenye simu tangu enzi za nokia toch

Mfano hio suala la simu kuingia wakati unaongea na simu nyingine ni suala la simu yako kuiset sio kazi ya oparator (mtoa huduma). Inaitwa call waiting ipo kwenye simu zote tangu mimi naanza kutumia simu yangu ya kwanza 2001.

Hilo la pili, ukiwa umeweka call waiting, simu nyingine ikiingia unaweza kuipokea na ile nyingine ikasubirishwa au uka opt kuikata kabisa ukaendelea na call mpya. Sio jambo jipya lipo na simu zote zina uwezo huo hata vitoch
 
Huduma za upigaji na upokeaji simu zinaendelea kuboreshwa siku hadi siku. Miongoni mwa huduma inayofurahiwa kwa sasa ni ile ya baadhi ya makampuni kuwezesha mteja aliyepigiwa simu ikiwa offline kupata ujumbe kwamba fulani alikutafuta muda fulani. Huduma hii imesaidia katika mambo mengi ikiwemo kuokoa maisha, kuepusha mafumanizi nk.
Huduma nyingine inayofurahiwa ni ile ya kuruhusu simu kuingia wakati mtu anaongea na simu nyingine. Ili kuiboresha huduma hii binafsi naomba iwekwe option ya mtu anayepigiwa simu ya pili kuwa na uwezo wa kukata mawasiliano na anayeongea naye ili apokee simu mpya inayoingia kutokana na umuhimu. Mfano mtu anaongea habari ya Simba na Yanga ghafla inaingia simu ya Bosi wake, awe na uwezo wa kukata mawasiliano yasiyo ya lazima ili kupokea simu muhimu.
Hizi huduma zipo zaidi ya miaka kumi. Unatumia mtandao gani?
 
Huduma nyingine inayofurahiwa ni ile ya kuruhusu simu kuingia wakati mtu anaongea na simu nyingine. Ili kuiboresha huduma hii binafsi naomba iwekwe option ya mtu anayepigiwa simu ya pili kuwa na uwezo wa kukata mawasiliano na anayeongea naye ili apokee simu mpya inayoingia kutokana na umuhimu. Mfano mtu anaongea habari ya Simba na Yanga ghafla inaingia simu ya Bosi wake, awe na uwezo wa kukata mawasiliano yasiyo ya lazima ili kupokea simu muhimu.
Huu utoto uwe na line mbili moja ya kiofisi au kizazi ingine ya umbeya ikiita ya bosi unakata ya umbeya unapokea ya bosi au uwe na simu mbili ya umbeya na ya ofisi
 
Hiyo ipo kwenye operating system ya simu, mfano OS ya Android inaruhusu kumuweka mtu onhold ili kupokea simu nyingine, na anaambiwa kabisa kwamba simu yako imesubirishwa
 
Ok kumbe Bongo hakuna hiyo kitu?We call it Voicemail light.
 
Sasa lipi ambalo halipo kwenye simu?
Ukiacha la ujumbe simu inapokuwa imezimwa, yaliyobaki ni uwezo wa simu na yapo kwenye simu tangu enzi za nokia toch

Mfano hio suala la simu kuingia wakati unaongea na simu nyingine ni suala la simu yako kuiset sio kazi ya oparator (mtoa huduma). Inaitwa call waiting ipo kwenye simu zote tangu mimi naanza kutumia simu yangu ya kwanza 2001.

Hilo la pili, ukiwa umeweka call waiting, simu nyingine ikiingia unaweza kuipokea na ile nyingine ikasubirishwa au uka opt kuikata kabisa ukaendelea na call mpya. Sio jambo jipya lipo na simu zote zina uwezo huo hata vitoch
Ni kweli tangu miaka 14 ilopita huduma hiyo ipo,
 
Miongoni mwa huduma inayofurahiwa kwa sasa ni ile ya baadhi ya makampuni kuwezesha mteja aliyepigiwa simu ikiwa offline kupata ujumbe kwamba fulani alikutafuta muda fulani. Huduma hii imesaidia katika mambo mengi ikiwemo kuokoa maisha, kuepusha....binafsi naomba iwekwe option ya mtu anayepigiwa simu ya pili kuwa na uwezo wa kukata mawasiliano na anayeongea naye ili apokee simu mpya inayoingia kutokana na umuhimu.

HUDUMA ZOTE HIZO zipo ndani ya simu,nakumbuka miaka hiyo hata simu za kugusa hazikuwepo; nilikuwa na siemens A50, ilikuwa nikipigiwa simu kama sitakikupokea nabonyeza namba 5 inenda kwa mwingine niliyempanga apokee.
 
Back
Top Bottom