Binafsi nimefurahishwa na maelezo mliyoyatoa pale jangwani(CHADEMA SQURE) sasa tunawaomba M4C ifike jimbo la RORYA kwani jimbo hili halina maendeleo yakuridhisha achilia mbali mwl.nyerere alijitahidi kuleta miundombinu ya maji na kuisambaza kutoka ziwani mpaka ochuna na marasibora sehemu ya ndani kabisa ya jimbo hilo,lakini cha kushangaza wabunge wote waliopata ubunge kwenye jimbo hili hakuna hata mmoja ambaye ameendeleza miundombinu hiyo ya maji,hata mashine zilizokua zinatumika kusukuma maji zimechakaa zimekua viota vya panya,wananchi wamekua wakisumbuka kutafuta maji mwendo mrefu maji hakuna sasa hii ni haki kweli? Huyu mbunge wa sasa nashindwa kumwelewa ameshindwa kufufua mashine ili jimbo zima lipate maji na kuondokana na shida ya maji lkn mambo ni tofauti kabisa amekalia kupiga kampeni za kujenga kwa wenzake huku kwake kunaporomoka.hivyo naomba makamanda muje RORYA muandae jimbo hili kwenda CHADEMA 2015.Nawasilisha.