Makahaba walipwe kujiepusha na biashara ya ngono Tanzania?

Daniel Mbega

JF-Expert Member
Mar 20, 2013
338
180
machangu.jpg
machangudoa2.jpg

KUPIGWA, kubakwa na msururu wa wanaume bila kupata chochote ni baadhi tu ya madhila yanayowakumba wasichana na wanawake wanaofanya biashara ya ukahaba katika mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, ambako kelele nyingi zimepigwa kuhakikisha biashara hiyo inakomeshwa.

Kutokana na kelele hizo, tayari Serikali imetangaza kampeni ya kuwakamata makahaba wote pamoja na wateja wao, zoezi ambalo baadhi ya wadadisi wamesema halitafanikiwa kwa sababu mnyororo wake ni mrefu.

Uchunguzi wa FikraPevu umebaini kuwa ukahaba ambao umekuwepo kwa miaka mingi duniani, siyo suala la kukamata watu mara moja na kuwaweka ndani, bali unatakiwa kutafuta kiini chake na kutafuta ufumbuzi badala ya kutumia nguvu.
SOMA ZAIDI...
 
Walipwe au wawezeshwe ili kupata ajira zingine ama kujitegemea?

Sasa wawe wanalipwa kwa kazi gani? Mpaka lini?

Hlf nakushauri zaidi ukamweleze Ummy Mwalimu haya.
 
KWa kuwa wamesema wanakamatwa na wateja wao ( Uchumi wao uko juu) hao ndio wapigwe faini iende kuanzisha trust fund ili waweze anzisha miradi. Aidha wanahitaji counseling ili kurudia maisha ya kawaida. Wengi nadhani hujihusisha kwa sababu ya shida!
 
Hilo la counseling umenena, wanahitaji msaada wa hali ya juu kama nilivyosoma maisha yao kwa kweli yanasikitisha.

Zitengenezwe center zao na kufundishwa kazi au kupewa ajira kwa watakao kubali kujiunga iwe option sio lazima.

Lazima kutakuwa na baadhi ya wanawake ambao watakubali mpango huo kwa kuondokana na kadhia hii, halafu wengine taratibu watafuata wakiona mabadiliko ya wenzao.
 
Serikali wawatafutie eneo kila wilaya then wawa toze kodi hili serikali wajipatie pato .mie naona itakuwa bora sana kwa sababu tumecherewa na kama hili taifa tungefwata sharia za kislamu ingekuwa sawa tungeweza
 
Back
Top Bottom