Daktari wa Meno
JF-Expert Member
- Sep 5, 2019
- 509
- 1,617
Hellow Tanzania, Hellow JF.
Naomba kutoa dukuduku langu kuhusu hawa wanaojiita/kuitwa majaji wa BSS. Mimi siyo mtazamaji sana wa mashindano hili ila mara kadhaa huwa naona video clip za washiriki mbalimbali kwenye Instagram Page ya BSS.
Sipendi namna ambavyo hawa majaji wanavyojishaua mbele ya washiriki pale ambapo mtu kafanya kitu ambacho hakijawabariki. Mfano: mshiriki akiboronga utaona namna wanavyomsakama kwa kejeli mbalimbali ambazo hazina maana yoyote, naona ni vyema kusema umejitahidi au sijapenda ulichofanya kuliko kuanza kujishaua mkijiona mnajua sana muziki kuliko wengine.
Kumbukeni nyodo ambazo mlizionesha kwa Harmonize wakati akishiriki shindano hilo miaka kadhaa iliyopita, kwenu alionekana hawezi ila kijana aliamini katika yeye mwenyewe. Acheni kujifanya nyie ni wakosoaji wazuri wa wenzenu kitu ambacho siyo. Madame Rita sidhani kama ana uwezo hata wa kuandika muziki achilia mbali kuimba ila akianza kujichekesha na kukejeli washiriki utasema ni latest version ya Beyonce kumbe hakuna chochote ajuacho.
Master Jay hivyohivyo naye kaambukizwa ushambenga wa wanawake na kuanza kuwa kama wao.
Tujifunze kupitia wenzetu ambao wako mbali na sisi kwenye muziki, je wanafanya kama sisi au ni style yenu wenyewe? Kama ni style yenu kwangu mimi naona mnawapa washiriki hofu, wanaenda jukwaani wakijua wakikosea watachekwa na kukejeliwa.
Mtanzania ukimpa tu kinafasi cha kukosoa mwenzake atajifanya ni mtu kutoka mbingu/sayari nyingine kwa namna ambavyo anajiona anajua.
Naomba kutoa dukuduku langu kuhusu hawa wanaojiita/kuitwa majaji wa BSS. Mimi siyo mtazamaji sana wa mashindano hili ila mara kadhaa huwa naona video clip za washiriki mbalimbali kwenye Instagram Page ya BSS.
Sipendi namna ambavyo hawa majaji wanavyojishaua mbele ya washiriki pale ambapo mtu kafanya kitu ambacho hakijawabariki. Mfano: mshiriki akiboronga utaona namna wanavyomsakama kwa kejeli mbalimbali ambazo hazina maana yoyote, naona ni vyema kusema umejitahidi au sijapenda ulichofanya kuliko kuanza kujishaua mkijiona mnajua sana muziki kuliko wengine.
Kumbukeni nyodo ambazo mlizionesha kwa Harmonize wakati akishiriki shindano hilo miaka kadhaa iliyopita, kwenu alionekana hawezi ila kijana aliamini katika yeye mwenyewe. Acheni kujifanya nyie ni wakosoaji wazuri wa wenzenu kitu ambacho siyo. Madame Rita sidhani kama ana uwezo hata wa kuandika muziki achilia mbali kuimba ila akianza kujichekesha na kukejeli washiriki utasema ni latest version ya Beyonce kumbe hakuna chochote ajuacho.
Master Jay hivyohivyo naye kaambukizwa ushambenga wa wanawake na kuanza kuwa kama wao.
Tujifunze kupitia wenzetu ambao wako mbali na sisi kwenye muziki, je wanafanya kama sisi au ni style yenu wenyewe? Kama ni style yenu kwangu mimi naona mnawapa washiriki hofu, wanaenda jukwaani wakijua wakikosea watachekwa na kukejeliwa.
Mtanzania ukimpa tu kinafasi cha kukosoa mwenzake atajifanya ni mtu kutoka mbingu/sayari nyingine kwa namna ambavyo anajiona anajua.

