Maisha in safari,Marufuku kukata tamaa,nafasi yako bado ipo

MMASSY

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
290
193
Ogopa sana kushindana na mtu aliyepoteza mwelekeo wa maisha....mtu huyo ni hatari sana kwani hana cha kupoteza wala hana mpango wowote na maisha yake ya baadaye kutokana na kujikatia tamaa.....
Mtu aliyepoteza mwelekeo wa maisha ni yule asiyeweza kusimamia mambo yake na kujali mambo yake na familia yake bali hutumia muda wake mwingi kufuatilia maisha ya watu wengine akiwa na lengo la kupotosha na kuchafua watu.Ni yule anayefuatilia madhaifu au mapungufu ya watu na kuyashikilia na kueneza mabaya ya watu kuliko mema yao kwa sababu anatamani na wengine wapoteze mwelekeo kama yeye........

Ni vyema kuwa makini na mtu wa aina hii na tumia hekima ya kutomsikiliza huku ukijiendeleza kufikia malengo yako ili uwe bora kuliko jana.Usikubali maneno yake yajenge kiota kwenye kichwa chako na usikubali moyo wako uumie kwa sababu yake maana shetani anamtumia kama chombo cha kukukatisha tamaa ili ushindwe kufika kwenye hatima yako iliyotukuka.

Kumbuka Bibiblia inasema siku zetu za kuishi si nyingi,tumia nafasi uliyopewa na Mungu kulifanya kusudi lake na fanikisha malengo yako!!

"Maisha ni safari,Marufuku kukata tamaa,nafasi yako bado ipo"

Kwanini usinipe jina kabisa nikakuwekea kitabu chako chenye kichwa hicho cha habari hapo juu? Usikose madini haya

Jerome Mmassy

Mwandishi Mwandamizi na Mkurugenzi Mtendaji.

Holy Hands Book Project

+255758673441
 
Mimi nasikitikia Pesa nilizotupa nilipoziingiza kwenye biashara kwa lengo jema, nikapata matokeo nisiyategemea yakaniletea majuto.Heri nisingewekeza
 
Mimi nasikitikia Pesa nilizotupa nilipoziingiza kwenye biashara kwa lengo jema, nikapata matokeo nisiyategemea yakaniletea majuto.Heri nisingewekeza
Hii imewahi nitokea, hakika ililikuwa ni kipindi kigumu sana ktk maisha yangu maana niliwekeza fedha nyingi
 
Maisha Lau yangalikua na fomula ingekua pw Sana graduate wengi mtaani tumepoteza matumaini ya kesho, ila shukran kwa ujumbe huu muhimu asubuhi hii, ubarikiwe Sana
Marufuku kukata tamaa mkuu.Mwenyewe nilikaa 5 years mtaani lakini mwisho wa siku mikatoka na bado napambana kutoka zaidi.Jiamini,usikae tu,jitese kidogo utafanikiwa.Maisha ni mapambano.Endelea kumwamini Mungu
 
Hii imewahi nitokea, hakika ililikuwa ni kipindi kigumu sana ktk maisha yangu maana niliwekeza fedha nyingi
Mkuu siku zote usiwekeze fedha nyinhi kwa kitu ambacho ndio unaanza,wekeza mtaji kidogo ili huo mradi ujiendeshe.Usianze kwa gia kubwa,anza kidogokidogo mwishoni utapanda na kuwa bilionea.
 
Mimi nasikitikia Pesa nilizotupa nilipoziingiza kwenye biashara kwa lengo jema, nikapata matokeo nisiyategemea yakaniletea majuto.Heri nisingewekeza
Biashara au ujasiamali ni pamoja na kutake risk pia mkuu.Usiogope,ukitaka kuwekeza anza kidogokidogo,wekeza fedha kidogo na simamia mradi,ukishaona unaweza kufanikiwa jiongezee kamtaji kidogokidogo.Usikate tamaa,bado upo safarini na amini nafasi yako bado ipo.
 
Mkuu siku zote usiwekeze fedha nyinhi kwa kitu ambacho ndio unaanza,wekeza mtaji kidogo ili huo mradi ujiendeshe.Usianze kwa gia kubwa,anza kidogokidogo mwishoni utapanda na kuwa bilionea.
Sure! nilijifunza mkuu maana ilifikia kipindi badala mradi ujiendeshe wenyewe nikawa natoa tena hela mfukoni kuokoa mradi usianguke lakini bado sikufua dafu
 
Marufuku kukata tamaa mkuu.Mwenyewe nilikaa 5 years mtaani lakini mwisho wa siku mikatoka na bado napambana kutoka zaidi.Jiamini,usikae tu,jitese kidogo utafanikiwa.Maisha ni mapambano.Endelea kumwamini Mungu
Pamoja Sana mkuu.
 
Biashara au ujasiamali ni pamoja na kutake risk pia mkuu.Usiogope,ukitaka kuwekeza anza kidogokidogo,wekeza fedha kidogo na simamia mradi,ukishaona unaweza kufanikiwa jiongezee kamtaji kidogokidogo.Usikate tamaa,bado upo safarini na amini nafasi yako bado ipo.
Ni jumuishi ya hasara ya uwekezo wote,nilizofanya sikuambulia kitu,mda ilikuwa changamoto, nadharia haikuwa sawa na hali halisi.
 
Ni jumuishi ya hasara ya uwekezo wote,nilizofanya sikuambulia kitu,mda ilikuwa changamoto, nadharia haikuwa sawa na hali halisi.
Sawa,umakini na maandalizi ya kina ni muhimu ili kuepuka hasara zinazoweza kujitokeza.Wako baadhi ya watu wameanzisha biashara na wamekuwa na mafanikio makubwa sana.Usiamini katika kushindwa tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom