Maigizo ya Edward Lowassa yazidi kugonga mwamba!

Maigizo ya Edward Lowassa yazidi kugonga mwamba!

Ng'wamapalala

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2011
Posts
6,811
Reaction score
6,506
Wahenga walisema, Bahati haiji mara mbili.

Huwezi kutumia mbinu zile zile za mapambano mara mbili kwa adui huyo huyo ukategemea kupata ushindi hasa ikichukuliwa aliyekuwa mpiganaji mwenzako kwa sasa ndiye adui yako.

Mbinu anazozitua Lowassa kwa sasa ni zile zile ambazo alizitumia katika mchakato wa mgombea Urais mwaka 2005 uliomwingiza Ikulu Rais Kikwete lakini ukaacha majeraha makubwa ndani ya CCM.

Mbinu hizi kwa sasa CCM wamezistukia na mbaya zaidi, anawakaanga wapambe wake kwa kutumia hizo hizo mbinu zake za zamani.

Ni siku mbili zimepita ambapo tulisikia kwenye vyombo vya habari kelele nyingi zikisema madiwani zaidi ya 18 wametimkia CHADEMA kwa sababu ya kile kinachosemwa, kupinga maamuzi yaliyofanywa Dodoma na wana CCM katika kumpata mgombea Urais kwa tiketi ya CCM.

Hawa Madiwani walikuwa ni kama mbuzi wa kafara ili kuitisha na kuitingisha CCM ili impigie magoti Lowassa wapambe wake.

Kuzifahamu vizuri mbinu za Lowassa pitia thread hii,

Baadhi ya Madiwani, wamegundua kama wanachuuzwa na kwa maana hiyo, wengine wamerudi CCM haraka ili kuchukua fomu za Udiwani.

Mzee mwenye kile tuliaminishwa maamuzi magumu yuko kimya wakati wapambe wake hawafahamu hata hatima zao za kisiasa na kimaslahi. Jeshi lake lililokuwa vitani kwa nguvu ya pesa limesambaratishwa na Wazee wa CCM wakati kwa sasa kamanda wao hajulikani aliko!

Wapambe wake wanashindwa nini kuelewa? Lowassa alishasema, hawezi kuondoka CCM!

Kwa habari zaidi, ungana na ITV Local News,
Hali ya kisiasa kati ya CCM na Chadema katika wilaya ya Monduli imegubikwa na sinto fahamu na kuwachanganya wananchi wasijue pakuelekea baada ya madiwani kumi kati ya kumi na nane wa CCM waliyo daiwa kuhamia Chadema kusema bado wapo CCM na tayari wamesha chukua na kurudisha fomu za kutetea nafasi zao huku wananchi wakiwataka wanasiasa waache kuwachanganya kwa kuwafanya wajinga.

Wakizungumza na ITV baadhi ya madiwani waliyo daiwa kuondoka CCM wamesema kauli hizo hazikuwa za kweli kwakuwa baadhi yao walikuwa hawaja hafiki mpango huo na kwamba wanaendelea kuheshimu taratibu za chama chao huku wakidai wanatetea nafasi zao kupitia CCM.

ITV ilimtafuta mwekiti wa madiwani waliyo hama aliyekuwa diwani kata ya Lepurko Julias Kalanga ambaye amesema kilichopo ni baadhi ya watu kukosa kujiamini katika jambo wanalolifanya na kwamba wanataka kuficha moto usiyo fichika na kuwachanganya wananchi lakini siku ikifika ukweli utajulikaka huku katibu wa CCM mkoa wa Arusha Alphonce Kinamhala akithibisha madiwani hao kuchukua fomu za kugombea kupitia CCM na kwamba hizo zilkuwa mbinu za watu kuichafua CCM.

ITV ilizungumza na wakazi wa Monduli ambao wameonesha kusikitishwa na hatua ya wanasiasa kutokuwa wakweli na kuwataka wasiwachanganye kwani wananchi wa sasa siyo wa miaka ya nyuma pamoja na yote lakini watafanya maamuzi yenye maslahi kwao na siyo vinginevyo.

 
Last edited by a moderator:
Tunapaswa kutumia akili zetu zaidi na tusikubali kuyunbishwa na wanasiasa. Tusipende kupita kiasi na tusichukie kupita kiasi.
 
Fisadi Lowasa hana jipya na akifanya mchezo tuta-freeze hata hizo accounts zake za benki za kifisadi. Tutamtumia TRA wakampigie mahesabu kwenye biashara zake kuona amekwepa kulipa kodi mabilioni mangapi kama hatafilisika ghafla. Wapambe wake mshaurini atulie asitingishe kiberiti ataumia bure.
 
huyu jamaa Anakaa kama anakwenda ACT,ccm wajipange asije stukiza na wabunge ambao watakua tayari wameteuliwa.
wakae ready na option 2.
 
Fisadi Lowasa hana jipya na akifanya mchezo tuta-freeze hata hizo accounts zake za benki za kifisadi. Tutamtumia TRA wakampigie mahesabu kwenye biashara zake kuona amekwepa kulipa kodi mabilioni mangapi kama hatafilisika ghafla. Wapambe wake mshaurini atulie asitingishe kiberiti ataumia bure.

Hapo ndipo unapoonesha ufisadi wenu ulivyoliangamiza taifa. Ccm hamlipi kodi kwa tiketi ya kushika dola ndio maana mmejaza wahidi magabachori ambayo hayalipi kodi na mengine kukamatwa na masandarusi ya fedhaa. Mshindwe na mlegee. Adhabu yenu october .
 
Hata hao wanne walioondoka bado ni wengi sana! CCM = UKIMWI!

Ukion hivi ni kweli wameondoka wengi ila ni namna gani ya kulielezea jambo hili,lazima tufanye kazi ya ziada.
 
Hapo ndipo unapoonesha ufisadi wenu ulivyoliangamiza taifa. Ccm hamlipi kodi kwa tiketi ya kushika dola ndio maana mmejaza wahidi magabachori ambayo hayalipi kodi na mengine kukamatwa na masandarusi ya fedhaa. Mshindwe na mlegee. Adhabu yenu october .

Mkuu hawa magabacholi ni kweli wamo kwenye system na wamekuwa wakitoa mapesa mengi kwa viongozi wasio waaminifu akiwemo Lowasa. Lowasa ana ushirikiano mkubwa sana na akina Rostam Azizi, Mohammed Dewji, Somaiya wa ShivaCom,, Manji na makaburu wa South Africa ambao hawalipi kodi kisawasawa kwenye biashara. Sasa ujio wa bwana Magufuli ndo mwisho wao. Tutafanya safishasafisha ya nguvu wewe subiri utaona mwenyewe.
 
Lowassa ni mtu hatari sana na sasa nazidi kumuogopa na kuchukua tahadhari kwa wana siasa. Mimi ilibidi nichukue fomu ya udiwani SAA 9 kabla ya muda kuisha kwa kile nilichokuwa nimeamini atatangaza mapema wapi wafuasi wake tunaelekea na sio siri alikuwa na wafuasi wengi sana. Nilirejesha fomu bila hata picha za pasipoti kwa kuwa nilichelewa maandalizi kwa kusubiri tamko la Lowassa!! Sass naamini Lowassa anafahamu madhambi mengi aliyonayo hivyo kutoka CCM chama kilichoyafunika itakuwa mwisho wa maisha yake. Maamuzi magumu ilikuwa falsafa ya uogo na utaperi wa hali ya juu. Shukrani Makonda na Nape kumbe mlifahamu huyu mzee si jasiri wala hana maamuzi yoyote magumu. Mshughulikieni ipasavyo kwa usanii wake. Mtu ambaye naweza kumuamini kuwa ana maamuzi magumu ni Lembeli pekee.
 
Fisadi Lowasa hana jipya na akifanya mchezo tuta-freeze hata hizo accounts zake za benki za kifisadi. Tutamtumia TRA wakampigie mahesabu kwenye biashara zake kuona amekwepa kulipa kodi mabilioni mangapi kama hatafilisika ghafla. Wapambe wake mshaurini atulie asitingishe kiberiti ataumia bure.

Hii ni kudhihirisha kua Serikali ya CCM haina sifa ta kuendelea kuongoza nchi hii kwani mnashindwa kukusanya kodi stahiki kwa Wafanyabiashara wakubwa kwakua tu wanawachangia pesa, kwahiyo TRA inafanya kazi kwa maelekezo ya chama chenu si ndio?
 
Hii ni kudhihirisha kua Serikali ya CCM haina sifa ta kuendelea kuongoza nchi hii kwani mnashindwa kukusanya kodi stahiki kwa Wafanyabiashara wakubwa kwakua tu wanawachangia pesa, kwahiyo TRA inafanya kazi kwa maelekezo ya chama chenu si ndio?

Tunakisafisha chama mkuu. TRA kuanzia uongozi wa awamu ya tano ya Magufuli watafanyakazi zao kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu yeyote. Matatizo yapo hatuwezi kukataa na hata CHADEMA wakiingia yanaweza kuwepo tu maana na wao ni mafisadi tu akina mbowe hao. Mfano mdogo tu Mbowe mwaka jana alimwachisha mbunge wa kuteuliwa wa kike wa CHADEMA safari ya kikazi Marekani iliyogharimiwa na bunge kwa pesa zetu walipa kodi akamwita aende Dubai kufanya naye zinaa na kuacha kazi aliyotumwa, mbaya sana. Kiofisi cha CHADEMA tu pale makao makuu Kinondoni kiko hoi, cha ovyo hakina hadhi, mijamaa inatafuna tu ruzuku na misaada kutoka kwa marafiki zao wa Ujerumani.
 
Tunakisafisha chama mkuu. TRA kuanzia uongozi wa awamu ya tano ya Magufuli watafanyakazi zao kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu yeyote. Matatizo yapo hatuwezi kukataa na hata CHADEMA wakiingia yanaweza kuwepo tu maana na wao ni mafisadi tu akina mbowe hao. Mfano mdogo tu Mbowe mwaka jana alimwachisha mbunge wa kuteuliwa wa kike wa CHADEMA safari ya kikazi Marekani iliyogharimiwa na bunge kwa pesa zetu walipa kodi akamwita aende Dubai kufanya naye zinaa na kuacha kazi aliyotumwa, mbaya sana. Kiofisi cha CHADEMA tu pale makao makuu Kinondoni kiko hoi, cha ovyo hakina hadhi, mijamaa inatafuna tu ruzuku na misaada kutoka kwa marafiki zao wa Ujerumani.
Kabisa mkuu huyu ZERO Ndio tatizo cdm na huyu anasaidiwa na wafuasi uchwara wao ambao hawajui NO kila jambo ni YES kinacho mpelekea DJ huyu kuwa MUNGU MTU CDM
 
Mkuu hawa magabacholi ni kweli wamo kwenye system na wamekuwa wakitoa mapesa mengi kwa viongozi wasio waaminifu akiwemo Lowasa. Lowasa ana ushirikiano mkubwa sana na akina Rostam Azizi, Mohammed Dewji, Somaiya wa ShivaCom,, Manji na makaburu wa South Africa ambao hawalipi kodi kisawasawa kwenye biashara. Sasa ujio wa bwana Magufuli ndo mwisho wao. Tutafanya safishasafisha ya nguvu wewe subiri utaona mwenyewe.

Ndugu, usidanganyike kuhusu ujio wa Magufuli. Hatakuwa na jipya. Hata Kikwete aliingia kwa staili hiyo hiyo. Tujiulize WANAOMWEKA Magufuli mbele kwa kumpamba na kumtetea ndio watakaomfunga KUFULI kwa maslahi yao binafsi. Wa kwanza ni Ben Mkapa,. huyu alipigania kwa nguvu zake zote John Pombe apite. Hili siyo bure. Hawa unaosema atawasafisha safisha ndo wanaochanga pesa kwa CCM ili ashinde kwa makubaliano kuwa atalinda ufisadi wao katika biashara zao halali na haramu......
 
Mimi naona tuhame kwa Edo maana sasa sio tena habari ya mujini
 
Back
Top Bottom